JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Mdau wa JamiiForums analalamika kuwa alitumia dawa za kutibu Ugonjwa wa Malaria zinazoitwa EKELFIN ambazo baadaye zilimsababishia kupatwa na mchubuko sehemu za siri na midomoni. Anashangaa kwanini Serikali haitoi taarifa kwa watumiaji juu ya madhara ya dawa hizi kwa binadamu. Ni kweli kuwa dawa hizi zinaweza kusababisha athari tajwa?
Katika mitandao mbalimbali ya kijamii ikiwemo katika jukwaa la JamiiForums.com, kumekuwa na majadiliano na maswali yanahoji au kutoa taarifa ambazo wengi hawana uthibitisho nazo kuhusu dawa za kuzuia maambukizi ya VVU ambazo muhusika anatakiwa kutumia ndani ya masaa 72. Je, hili lina ukweli? Na inakuaje kwa muhitaji ambaye si muhanga, na gharama zake zikoje? Je, kuna ukweli kwenye hili?
Wakuu, Kuna video nilikutana nayo huko mtandaoni (nimeangalia sijaiona), huyo dada alikuwa anasimulia jinsi rafiki yake alivyokufa baada ya kung'atwa chura. Chura huyo alikuwa ndani ya kiatu chake, wakati anavaa hakumuona, basi huyo chura akamng'ata kwenye kidole baada ya kushtuka (unajua jinsi wadada tunaogopa wadudu) akamtoa kwenye kiatu na kuvaa na kuendelea na kazi zake. Baada ya siku mbili yule dada akaumwa, homa kali ikamshika kumpeleka hospitali ndio ikaonekana ni hiyo sumu ya chura, na imeshambaa mwilini kiasi ambacho hakuna msaada tena. Mwisho dada alikuwa anakoroma kama chura (kama vile inavyotokea mtu aking'atwa na mbwa mwenye kichaa) mwishowe akafa. Sasa wakuu mimi nauliza, hawa chura tunaopishana nao majumbani ndio...
Huwa navutiwa sana Historia za wanamke shupavu ambao walifanya mambo ya kuacha alama kwenye jamii zao na kukumbukwa mpaka sasa. Katika pitapita zangu kwenye machapisho nikavutiwa na historia ya mtawala kutoka katika kabila la Waha wa Jamii ya Kitutsi, ukanda wa Kasulu sehemu za Heru Juu. Imezoeleka kuwa wanaume ndio huwa machifu katika jamii mbalimbali za Kitanzania kabla na baada ya Uhuru. Sikuwahi kusikia mwanamke yeyote kuwa Chifu wa jamii fulani tofauti na Theresa Ntare. Tukiachana na Chifu Hangaya ambaye ni Chifu wa Heshima wa kabila la Wasukuma, naweza kuhitimisha kwa kusema Chifu Theresa Ntare ni Chifu pekee mwanamke katika historia ya nchi yetu Tanzania. Mwami Theresa Ntare
Nimeona taarifa mtandaoni ikisema watumishi wa Umma na Binafsi ambao wamechangia kwa zaidi ya miezi 108 yaani miaka 9 katika NSSF au PSSSF sasa rukhsa kutumia michango yao kama dhamana ya kuchukulia mkopo wa kujenga, kuboresha au kununua nyumba nchini Tanzania. Kanuni namba 141 za Mwaka 2024 zimeanza kazi tangu Machi 8, 2024. JamiiCheck tusaidieni kujua ukweli wake.
Salaam Wakuu, Nimekutana na stori mtaani zinadai kwamba mnamo mwaka 1990 Bondia Maarufu Muhamedi Ali alienda nchini Iraq kuzungumza na rais wa nchi hiyo wakati huo Sadam Hussein kuwaachia mateka wa Marekani na kufanikiwa. Je, kuna ukweli wowote kuhusu sakata hili? Tunaombeni ufafanuzi ====== Muhammad Ali alizaliwa mnamo 17 Januari 1942 na alifariki 3 Juni 2016. Muhammad Ali alikuwa mwanamasumbwi kutoka nchini Marekani. Awali alijulikana kama Cassius Clay, lakini alibadilisha jina lake baada ya kujiunga na jumuia ya Kiislamu ya Nation of Islam mnamo mwaka wa 1964. Baadaye akabadilisha dini na kuwa Mwislamu kunako mwaka wa 1975 Ndipo alipobadili jina na kuanza kufahamika kama Muhammad Ali. Alipata kuwa bingwa wa uzito wa juu mara...
Matumizi ya tumbaku ni moja ya maafa ya afya ya umma yanayojulikana sana. Licha ya ripoti nyingi kuhusu afya ya umma, matumizi ya tumbaku yanazidi kuongezeka katika nchi zinazoendelea na zilizoendelea. Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), takriban watu Bilioni 1.3 duniani wanavuta sigara ambapo 80% kati yake wanatoka kwenye nchi zenye uchumi mdogo na uchumi wa kati. Aidha, takriban watu Milioni 7 hupoteza maisha kutokana na athari za moshi wa sigara unaotokana na kuvuta sigara moja kwa moja au pia kuvuta moshi uliotolewa na mvutaji wa Sigara. Tumbaku huathiri karibu kila kiungo na mfumo katika mwili, ikisababisha matatizo mbalimbali kama vile saratani, Magonjwa ya mfumo wa upumuaji, Ugonjwa wa Mishipa ya Moyo, Kiharusi...
Leo nimesoma mtandaoni kuwa Vidonda vya tumbo(Ulcers) huweza kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine. Naomba kujua kama ni kweli maana siku zote mie najua vidonda vya tumbo huvipata mtu kutokana na mtindo wake wa maisha(kutokula) au kwa kutumia baadhi ya dawa ambazo zinaweza kuchubua utumbo. Sasa hii ya kuambukiza kwangu imekuwa mpya sana, tena mwandishi alifafanua zaidi kuwa eti iwapo mwenza wako ana ulcers basi uwezekano wa wewe kuupata ni mkubwa maana anaweza kukuambukiza.
Back
Top Bottom