kumekuwepo na chapisho lililosambazwa na mtumiaji wa mtandao wa Facebook likidai kuwa meli ya kivita ya Marekani, USS George H. W. Bush, inapitia katika Bahari ya Hindi. Kwa mujibu wa Marine Finder, meli hiyo inadaiwa kuwa iko karibu na mpaka wa Tanzania na Kenya, ikielekea Mashariki ya Kati kwa lengo la kuimarisha uwepo wa kijeshi wa Marekani katika eneo hilo.
Inadaiwa pia kuwa Marekani imelazimika kutumia njia ndefu zaidi kuelekea Mashariki ya Kati ili kuepuka Bahari ya Shamu (Red Sea), hususan katika eneo la Yemen, kutokana na hofu ya kushambuliwa na waasi wa Houthi.
je ni upi uhalisia wa chapisho hilo ?