Mwanamke asipo mnyonyesha mtoto kwa zaidi ya siku moja maziwa yake huchacha na kuharibika.
Wanawake hushauriwa kumwachisha mtoto ziwa ili asidhurike kwa sababu maziwa hayo hukosa tena sifa ya kutumiwa na mtoto.
Ukweli upoje?
Kumekuwepo na mijadala inayoendelea kwenye mitandao ya kijamii ikizungumzia uondolewaji wa tozo kwenye miamala ya kielekroniki.
Baadhi ya watu wamekuwa wakidai kuwa tozo hizi zimefutwa kila sehemu huku wengine wakidai kuwa zimeongezeka tofauti na awali.
Ukweli wa suala hili upoje?
Huu Muungano ni chenga kabisa una kero nyingi mno, naona kwa Zanzibar wao ni raha kwenda mbele.
Sisi wote ni Watanzania lakini ajabu Mtanganyika akienda Zanzibar endapo atahitaji kuendesha gari basi atatakiwa kuomba kibali maalum kinachotolewa na mamlaka za huko, vinginevyo utakuwa unavunja sheria.
Hili suala halijakaa sawa kabisa, sawa na lile la kulipia kodi electronics kutoka Zanzibar, au Mzanzibar kumiliki ardhi Bara wakati Mtanganyika anawekewa vikwazo mfululu kumiliki ardhi Zanzibar.
Huu Muungano ni wa kishenzi sana.
Wakati napitia pitia mitandaoni kutafuta style mpya kwa ajili ya shangazi yenu ndio nikakutana na hili bandiko kuwa aina ya kujamiiana huku mwanamke akiwa amemkalia mwanaume juu ('woman on top' or 'cowgirl' or 'reverse cowgirl'), hatari kwa afya ya mwanaume kwani hupelekea maumivu makali kwani hupekelea fracture ya uume kwa asilimia kubwa wakati wa kushiriki tendo la ndoa.
Inashauriwa mwanaume ndio akae juu ili kupunguza uwezekano wa kupata madhara.
Ikatokea mwanaume amemwaga manii kwenye taulo ambalo muda mchache baadae mwanamke akalitumia kukaushia uke wake.
Kuna uwezekano akapata ujauzito kupitia taulo hilo?
Inadaiwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi, amekitaka Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kusitisha mkutano wake uliopangwa kufanyika kesho Julai 23,huko Buriaga, Temeke jijini Dar es Salaam.
Barua inayodaiwa kuandikwa na Sisty Nyahoza, Naibu Msajili wa vyama.
Salaam ndugu zangu,
Leo katika pita zangu mitandaoni nimeona baadhi ya kurasa zinazoweka masula ya burudani na habari za Wasanii zikieleza kuwa kuna sauti ya Keefe D imevunja ikikiri kuhusika na kifo cha 2 Pac.
Upi ukweli kuhusu sauti na sakati hilo?
Nimeona mjadala kuhusu mihula anayoruhusiwa kugombea makamu aliyeshika madaraka ya Urais kutokana na kuchukua kiti katikati ya muhula baada ya Rais aliyekuwepo madarakani kushindwa kuendelea aidha kwa kufariki akiwa madarakani, kujiudhuru au sababu za kiafya.
Mjadala umechagizwa na kauli ya Sophia Mjema aliyesema Rais Samia ni hadi 2035, huku wanaharakati wakipinga vikali kuwa hana sifa ya kugombea mihula miwili tena.
Je, ukweli ni upi?
Aprili 27, 2023, akaunti ya Mtandao wa Twitter inayotumia jina la MainLandAfrica iliweka chapisho linalodai kuwa Bilionea wa Marekani Dan Friedkin amekodisha takriban Ekari 6,000,000 za ardhi nchini Tanzania.
Chapisho hilo lilienda mbali zaidi kwa kudai kuwa Friedkin ni mmiliki wa Ekari zingine 25,000 za ardhi zinazounda pori la Akiba la Mwiba.
Wanaojua kuhusu huyu jamaa watupe details anafanya biashara gani na ardhi kubwa kiasi hicho?
Kiongozi mkuu wa Chama cha EFF amemtaka Raila Odinga kuacha maandamano na kukubali kuwa alishindwa. Amesema pia aache kuvuruga amani nchini Kenya kwani Rais Ruto alipita kwa haki.
Julius Malema akihutubia kwenye maadhimisho ya miaka 10 ya EFF
Chips ni chakula kinachotengenezwa kutoka kwenye viazi. Chakula hiki kimekuwa kinahusishwa na matatizo mengi ya kiafya ikiwemo magonjwa ya moyo.
Wataalam, tusaidieni ni kipi hasa kinachofanya chips iwe mbaya kiasi cha kuhusishwa na mambo mabaya.
Mende ni maarufu kwa ukakamavu wao, na mara nyingi hutajwa kuwa ndio walionusurika zaidi katika vita vya nyuklia. Wengine hata wanadai kwamba wanaweza kuishi bila vichwa vyao.
Suala la mende kuendelea kushi hata baada ya kukatwa kichwa lipoje?
Inadaiwa huyu jamaa bhana enzi za utumwa, alitumika na masta wake kama mbegu ya kuzalisha watumwa wenye nguvu. Inadaiwa kutokana na kuwa na nguvu, umbo maridadi na urefu wa futi 7 hivyo masta wake alimpa upendeleo wa kipekee wa kumpunguzia majukumu mengi huku kazi yake kubwa ilikiwa ni kulala na kuwapa mimba wanawake mbalimbali ili waweze kumzalia masta wao watoto wenye nguvu ambao wangetumika katika shughuli za kitumwa.
Roque Jose Florêncio aliacha idadi kubwa sana ya watoto.
Ingawa ni kama utani na inachekesha ila huwezi amini kuwa ng'ombe akijamba/kutoa ushuzi basi kile kitokacho huambatana na gesi ya methane ambayo huzalisha joto na moto/mwanga.
Wanaharakati mbalimbali wa mazingira wamekuwa wakidiscourage ufugaji/uzalishaji wa ng'ombe kwa wingi na kusema wazi kuwa ushuzi wa ng'ombe huleta mabadiliko ya hali ya hewa, kwa sababu ng'ombe hutoa methane, gesi chafu inayohusishwa na ongezeko la joto duniani.
Ng'ombe akiwa anajamba, ukiwasha njiti ya kiberiti moto unawaka kutokana na gesi ya methane.
Ningependa kujua ukweli wa hili jambo.
Tanzania yasaini mikataba minne na Falme za Kiarabu ndani ya mwaka mmoja.
1. Kuendeleza uwanja wa ndege wa KIA
2. Ushirikiano na Posta Tanzania
3. Kuendeleza misitu yote nchini na TFS
4. DP World na TPA
Hii dunia ina vitu vya ajabu sana na vya kushangaza. Kuna historia baadhi unaweza unaweza kushangazwa nazo mojawapo ikiwa hii niliyopata kusimuliwa.
Msitu wa Nyumbanitu una historia nyingi za kushangaza. Msitu huu upo katika Wilaya ya Wanging'ombe mkoa wa Njombe. Msitu huu nimepata kusimuliwa kuwa endapo mwanamke atakuwa kwenye siku zake basi hatoruhusiwa kuingia katika msitu huo, Ikiwa atakaidi basi akiingia kwenye huo msitu ndio utakuwa mwisho wake wa kuonekana maana atapotea mazima.
Nadhani hili jambo mnaona linavyostaajibisha. Najiuliza huu msitu una nguvu na miujiza gani mpaka uweze kuwatendea hivyo dada zetu.
Miaka kadhaa nyuma niliwahi kusikia mwanamke mmoja nchini Uganda kajifungua watoto wawili (mapacha) wenye baba tofauti, hali hii ilinishangaza sana.
Hali kama hii iliripotiwa pia Septemba 9, 2022 kwenye jarida la CNBC ambapo mwanamama mmoja kutoka Minerois, Brazil alithibitika kuwa na ujauzito wa mapacha ambao baada ya kupimwa DNA zao ilibainika kuwa walikuwa wa baba tofauti.
Kisayansi, ni kweli kuwa jambo hili linaweza kutokea? Kama jibu ni ndio, linatokeaje?
Kijana wa miaka 29 aliushangaza ulimwengu kwa kitendo cha kikatili kisichokuwa na chembe ya utu. Inadaiwa baada ya kumpindua na kumuua Rais aliyekuwa madarakani William Tolbert, Samuel Doe alihakikisha anamaliza mizizi ya mtangulizi wake kwa kuua viongozi wote waandamizi.
Inadaiwa Aprili 22, 1980 viongozi 13 walifikishwa ufukweni mwa bahari ya Atlantic nchini humo, wanaume hao 13 walikuwa nusu uchi ambapo walifyatuliwa risasi na vikosi vya Rais Samuel Doe.
Kati ya waliouawa ni pamoja na Frank E. Tolbert ambaye alikuwa Kaka yake na rais Tolbert, na Rais wa Bunge la seneti.
Picha: hali ilivyokuwa siku ya mauaji
Muosha huoshwa, Rais Samuel Doe naye alikuja kupinduliwa na kuuawa kikatili sana na waasi.
Magonjwa ya Zinaa ikiwemo kaswende yanachangia mtu kupata ugonjwa wa Afya ya akili ikiwemo Kupoteza Kumbukumbu, Msongo wa Mawazo na Mania.
UKIMWI pia unatajwa kuchangia kwa kiasi kikubwa matatizo ya Afya ya Akili kwa Wagonjwa.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.