A
Anonymous
Guest
Nina kero kadhaa kuhusu Shule ya Msingi Kiswahilini inayopatikana Wilaya ya Sikonge, Kata Igigwa, Kijiji cha Tumbili, Kitongoji cha Kiswahilini yenye Wanafunzi 300 ina changamoto kadhaa
1. Mbali na kuwa na Wanafunzi 300, shule hiyo ya Mkoani Tabora ina matundu ya vyoo mawili tu tena yenye uchakavu, hata hivyo kuna matundu mengine 10 ambayo yamejengwa lakini hayajakamilika kwa muda wa miezi sita sasa.
Hivyo, Wanafunzi wote wanatumia matundu mawili jambo ambalo ni hatari kiafya.
2. Changamoto ya pili ni Walimu wa shule hiyo hawana vyoo vyao, hali mbayo inawafanya wawe wanaenda mtaani kupata huduma, wengine wanaenda vichakani, hiyo hali inaumiza sana.
3. Walimu wa hii Shule wanatembea umbali wa Kilometa 1.5 kwenda shule na wakati huohuo ikifika Saa Sita na Nusa Mchana wanarudi nyumbani kula na kurudi Saa Saba na Nusu ili kukamilisha muda uliobaki hadi saa kumi na nusu.
Tumeshafikisha malalamiko yetu kwa mamlaka husika lakini hakuna msaada wala majibu yoyote yanayotolewa ukizingatia shule ni mpya lakini bado imejengwa bila kuwepo kwa nyumba za Walimu na kuwafanya wawe wanaingia tu huku na huko.
Jambo lingine ni kuwa Shule hii yenye Darasa la Awali hadi la Tano ina jumla ya vyumba vya madarasa 3 tu, ambavyo vimejengwa kwa nguvu za Wananchi, kuna upungufu wa madarasa.
1. Mbali na kuwa na Wanafunzi 300, shule hiyo ya Mkoani Tabora ina matundu ya vyoo mawili tu tena yenye uchakavu, hata hivyo kuna matundu mengine 10 ambayo yamejengwa lakini hayajakamilika kwa muda wa miezi sita sasa.
Hivyo, Wanafunzi wote wanatumia matundu mawili jambo ambalo ni hatari kiafya.
2. Changamoto ya pili ni Walimu wa shule hiyo hawana vyoo vyao, hali mbayo inawafanya wawe wanaenda mtaani kupata huduma, wengine wanaenda vichakani, hiyo hali inaumiza sana.
3. Walimu wa hii Shule wanatembea umbali wa Kilometa 1.5 kwenda shule na wakati huohuo ikifika Saa Sita na Nusa Mchana wanarudi nyumbani kula na kurudi Saa Saba na Nusu ili kukamilisha muda uliobaki hadi saa kumi na nusu.
Tumeshafikisha malalamiko yetu kwa mamlaka husika lakini hakuna msaada wala majibu yoyote yanayotolewa ukizingatia shule ni mpya lakini bado imejengwa bila kuwepo kwa nyumba za Walimu na kuwafanya wawe wanaingia tu huku na huko.
Jambo lingine ni kuwa Shule hii yenye Darasa la Awali hadi la Tano ina jumla ya vyumba vya madarasa 3 tu, ambavyo vimejengwa kwa nguvu za Wananchi, kuna upungufu wa madarasa.