KERO Wanafunzi Shule ya Nyabulugoya (Mwanza) hawapumzishwi, wanatumika kitega Uchumi cha Walimu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Kuna kero kubwa tunaipata Wazazi dhidi ya Shule ya Msingi Nyabulugoya iliyopo Nyegezi Jijini Mwanza, tunaomba tupazie sauti ili wenye nafasi zao wapate ujumbe huu.

Kila Jumamosi Wanafunzi wanaenda kufanyishwa mitihani kwa hela, imekuwa ni kitega uchumi cha Walimu.

Sasa hivi likizo ya wiki moja Watoto pia wanaambiwa waende tuition ya Shilingi 500 na ni lazima, tunakubali kuwa elimu ni ghali lakini Watoto pia wanahitaji kupumzika, sasa likizo ya one week tuition ya nini? Hii ni kero kwa kweli.

Itafika hatua akili za Watoto zitachoka kwa kuwa wanakosa muda wa kupumzika, muda wote ni kusoma na mitihai tu, hii sio sawa, Wizara ya Elimu ingalie hiki kinachoendelea, inawezekana sio hapa pekee.
 
Hapana hata mbeya wanafunzi hawapumzishwi hususan shule za msingi za hapa sinde wanafunzi hulipishwa muchango na iktokzea ck1 tu mtot km hakutoa bas anachapwa na na anatukanwa na kuambiwa kma tutakuja kwnu kuangalia kma kweli wew umeshindwa kulipa.hilo limenjgowa mm kwa mdogo wang alipigwa sana na akatukanwa mpaka mwalim akasema atakuja kukagua uome kwet kipoje ata tushindwe kimlipia ukizingatia ndan mna watot5 wote nj michango kila wiki hapo hukawalisha wakashiba
 
Serikali rudisheni ada mashuleni ili elimu iwe bora. Pia wazazi watambue wajibu wao.....acheni siasa rudisheni ada watu walishakuwa wapuuzi sana
 
Kuna kero kubwa tunaipata Wazazi dhidi ya Shule ya Msingi Nyabulugoya iliyopo Nyegezi Jijini Mwanza, tunaomba tupazie sauti ili wenye nafasi zao wapate ujumbe huu.

Kila Jumamosi Wanafunzi wanaenda kufanyishwa mitihani kwa hela, imekuwa ni kitega uchumi cha Walimu.

Sasa hivi likizo ya wiki moja Watoto pia wanaambiwa waende tuition ya Shilingi 500 na ni lazima, tunakubali kuwa elimu ni ghali lakini Watoto pia wanahitaji kupumzika, sasa likizo ya one week tuition ya nini? Hii ni kero kwa kweli.

Itafika hatua akili za Watoto zitachoka kwa kuwa wanakosa muda wa kupumzika, muda wote ni kusoma na mitihai tu, hii sio sawa, Wizara ya Elimu ingalie hiki kinachoendelea, inawezekana sio hapa pekee.
Mpeleke mwanao private mkuu!!
 
Back
Top Bottom