Pongezi za Miaka 60 ya Muungano: Twende Kwenye Muungano Kamili wa Ukweli wa Nchi Moja, Serikali Moja na Rais Mmoja? Kero Zote za Muungano Zitayeyuka!

Wanabodi,

Loe nchi yetu tumeadhimisha miaka 60 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, na kuwa nchi moja ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Muungano wetu ni muungano adimu na muungano adhimu, kwasababu hapa duniani hakuna muungano mwingine wowote kama huu muungano wetu. Ni muungano wa nchi mbili kuungana na kuunda nchi moja ya JMT, yenye nchi mbili ndani yake, Tanzania na Zanzibar, wenye marais wawili, rais wa JMT na Rais wa Zanzibar, wenye Katiba mbili, katiba ya JMT na Katiba ya Zanzibar, wenye mabunge mawili, Bunge la JMT na Baraza la Wawakilishi, lenye mahakama mbili, mahakama kuu ya Tanzania na Mahakama kuu ya Zanzibar. Kwa maoni yangu, muungano wa aina hii kudumu kwa miaka 60, itoshe, sasa twende kwenye muungano kamili wa nchi moja, serikali moja na rais mmoja!.

Kuungana kwa TANU na ASP
Vyama vya TANU na ASP vilipoungana ile 1977, sii wengi humu walikuwa wamezaliwa!, wengi humu wamezaliwa, wameikuta CCM, hawakuikuta TANU na ASP, hivyo hawajui kwanini TANU na ASP viliungana, na viliungana ili iweje?.

Mimi ni mtu wa 60s, hivyo ile 1977, TANU na ASP zilipoungana nilikuwa darasa la tatu, kijijini Itonjanda, nikikaa kwa bibi mzaa Baba, Bibi Wakawombwe, (RIP) baada ya Baba Mzee Mayalla(RIP) kuhusika na yale mambo fulani ya Mwanza ya 1976!.

Sababu ya TANU na ASP kuungana, ni kuelekea kwenye serikali moja!. Baba wa taifa, Mwalimu Nyerere alisema huu muungano wa vyama vya TANU na ASP na kuzaliwa chama kipya, Chama cha Mapinduzi, CCM, ni mwanzo wa safari ya kuondoka kwenye serikali mbili, kuelekea kwenye serikali moja!. Jee ndoto hii ya Mwalimu Nyerere, kwa Tanzania kuwa nchi moja ya JMT yenye serikali moja na rais mmoja, itakuja kutimia?.

Watanzania wanahitaji sana kuelimishwa kuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu, tena ni Rais Samia, ndie kiongozi wa kwanza wa juu aliyetoa ruhusa watu waachwe huru kujadili muungano. Baada ya muungano, nchi zote mbili zilitoweka, hakuna nchi ya Tanganyika wala hakuna nchi ya Zanzibar, bali nchi ya Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Zanzibar.

Elimu ya Uraia Kuhusu Muungano wetu adimu na adhimu!.
Duniani kuna miungano ya aina mbili Kuu,

1. Miungano ya union, nchi mbili au zaidi zinaungana kuunda nchi moja. Zile nchi zote zinakufa na inazaliwa nchi moja mpya.

2. Miungano ya federation, ni nchi mbili au zaidi zinaungana na kuunda nchi moja, ila zile nchi zote zinakuwa na serikali ya muungano, Federal Government na State Government, kila nchi ina utawala wake wa ndani.

Muungano wetu ni very unique, ndio maana unaitwa muungano adimu na adhimu, kwasababu ni muungano pekee duniani ambao upande mmoja ni muungano wa union kwa nchi mbili kuungana kuunda nchi moja ya JMT, na upande wa pili ni muungano wa federation wenye serikali mbili, marais wawili, mabunge mawili na mahakama mbili.

Muungano wetu kimataifa ni muungano wa union, Tanzania kimataifa ni nchi moja ya JMT, yenye serikali moja ya JMT, chini ya rais mmoja wa JMT, ambaye ni mkuu wan chi, mkuu wa serikali na amiri jeshi mkuu.

Lakini Kitaifa, nchi ya Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye sehemu mbili, Tanzania Bara na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar, yenye katiba mbili, katiba ya JMT, na katiba ya Zanzibar, yenye serikali mbili, serikali ya JMT na serikali ya Zanzibar, SMZ, yenye marais wawili, rais wa JMT na rais wa Zanzibar

Mkanganyiko wa Katiba.

Kama nilivyosema kimataifa Tanzania ni nchi moja ya JMT, hakuna mkanganyiko wowote wa kimataifa kuhusu Tanzania.

Lakini Kitaifa kuna mkanganyiko wa katiba kati ya katiba ya JMT na katiba ya Zanzibar.
Kwa mujibu wa katiba ya JMT, ya mwaka 1977, Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye sehemu mbili, Tanzania Bara na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar. Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, inaiita Zanzibar ni nchi, ni moja ya nchi mbili zinazounda JMT!. Kitendo cha katiba ya Zanzibar kuuita Zanzibar ni nchi, kinawakanganya Watanzania kudhani kuwa nchi ya Tanganyika ndio pekee iliyokufa ila nchi ya Zanzibar ipo haikufa.

Naomba niwahakikishie Tanzania ni nchi moja ya JMT, ile nchi inayotajwa na katiba ya Zanzibar kuwa ni nchi ya Zanzibar, sii kweli kuwa Zanzibar ni nchi, bali ni jina tuu, hayo mabadiliko ya katiba ya Zanzibar kujiita nchi, kimuungano ni mabadiko batili, ila, kwa vile mabadiliko hayo ni kwaajili ya Zanzibar tuu, na hayatambuliwi na katiba ya JMT, serikali ya JMT, imeamua kuyapuuza!, lakini kufuatia hizi kelele, tutapuuza mpaka lini?. Si ni bora twende kwenye serikali moja, haya yote yaishe?.

Hitimisho
Kwa vile Rais Samia, anakwenda kutupatia katiba mpya, nashauri hili la mkanganyika wa katiba kati ya katiba ya JMT na Katiba ya Zanzibar, pia litarekebishwa, na kwa maoni yangu, dawa pekee ya uhakika na ya kudumu ambayo ni mwarobaini wa kuzimaliza kero zote za muungano, ni kwenda kwenye serikali moja. Nimalizie na hili swali, je, Tanzania sasa tumefika wakati wa kutimiza ndoto ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, ya uzalendo wa kweli wa JMT, wa kwenda kwenye nchi moja, yenye serikali moja na rais mmoja?

Hongera kwa miaka 60 ya Muungano wetu adimu na adhimu,
Sasa twende kwenye nchi moja, serikali moja na rais mmoja!.

Mungu Ibariki Tanzania.

Paskali
Wazo zuri sana kama litakubaliaka.
 
Naunga mkono hoja. Kwa wakati huu yakitokea kama yale ya 'kuchafuka hali ya hewa Zanzibar', hoja za OIC au kashikashi kama zile za wale G55 na lile azimio la bunge la madai ya serikali tatu sijui nani atasimama kuliokoa taifa.

Ili tuwe salama ni muhimu tuwe na serikali moja tu.
Salama ya kitu gani kwani Zanzibar iko salama kwa kuvamiwa na Tanganyika? Si mnatuuwa kila uchaguzi kulazimisha kuweka vibaraka vyenu?
 
binafsi sina shaka kabisaa,
ndoto ya Baba wa Mwl.J.K.Nyerere yaweza kutimia vizuri sana na kikamilifu, endapo tu viongozi wenye wenye utashi dhabiti wa kisiasa, watathubutu, watatuelekeza, watatusimamia, watatupitisha na kutuongoza kufikia huko kwa maridiano na amani, huku sote tukiwa na ufahamu, uelewa na nia moja dhabiti ya kua nchi moja Tanzania 🐒
Hilo sahau km ilishindikana wakati ulopta saiv ningum sn fanya uchunguzi pande zote mbili utapata uhalisia
 
Zanzibar ni mali ya tanganyikaaa

Full stop

Ova
Tanganyika ndio mali ya Zanzibar, Mama mnae Hadi 2030 mtake mistake, na tutabadisha katiba awatawale mpaka achoke mwenyewe na hamna la kumfanya.
 
Tanganyika ndio mali ya Zanzibar, Mama mnae Hadi 2030 mtake mistake, na tutabadisha katiba awatawale mpaka achoke mwenyewe na hamna la kumfanya.
Hiyo ya kutawala hainihusu,atawale hata maisha
Ila zanzibar ni mali ya tanganyika

Ova
 
Wakati katiba ya zanzibar inaitambua zanzibar kama nchi serikali ya jamhuri ya muungano ilikua wapi hadi ilo likawezekana?.Mapendekezo yako ni kiini macho tu.wazanzibar walishajitafuta wakajipata na kamwe hawawezi kukubali kurudi nyuma.Ukitazama vizuri utagundua hakuna nchi iliyokufa bali watanganyika tulikubali kua makondoo tukalala uku wenzetu wakiamka.na kamwe hawawezi kukubali walale kwakukubali kupoteza serikali yao.Njia pekee yakupunguza hizo kero ni serikali tatu wala sio moja.Tofauti na hivyo ni porojo za kisiasa uku miaka ikienda.
 
Wanabodi,

Loe nchi yetu tumeadhimisha miaka 60 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, na kuwa nchi moja ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Muungano wetu ni muungano adimu na muungano adhimu, kwasababu hapa duniani hakuna muungano mwingine wowote kama huu muungano wetu. Ni muungano wa nchi mbili kuungana na kuunda nchi moja ya JMT, yenye nchi mbili ndani yake, Tanzania na Zanzibar, wenye marais wawili, rais wa JMT na Rais wa Zanzibar, wenye Katiba mbili, katiba ya JMT na Katiba ya Zanzibar, wenye mabunge mawili, Bunge la JMT na Baraza la Wawakilishi, lenye mahakama mbili, mahakama kuu ya Tanzania na Mahakama kuu ya Zanzibar. Kwa maoni yangu, muungano wa aina hii kudumu kwa miaka 60, itoshe, sasa twende kwenye muungano kamili wa nchi moja, serikali moja na rais mmoja!.

Kuungana kwa TANU na ASP
Vyama vya TANU na ASP vilipoungana ile 1977, sii wengi humu walikuwa wamezaliwa!, wengi humu wamezaliwa, wameikuta CCM, hawakuikuta TANU na ASP, hivyo hawajui kwanini TANU na ASP viliungana, na viliungana ili iweje?.

Mimi ni mtu wa 60s, hivyo ile 1977, TANU na ASP zilipoungana nilikuwa darasa la tatu, kijijini Itonjanda, nikikaa kwa bibi mzaa Baba, Bibi Wakawombwe, (RIP) baada ya Baba Mzee Mayalla(RIP) kuhusika na yale mambo fulani ya Mwanza ya 1976!.

Sababu ya TANU na ASP kuungana, ni kuelekea kwenye serikali moja!. Baba wa taifa, Mwalimu Nyerere alisema huu muungano wa vyama vya TANU na ASP na kuzaliwa chama kipya, Chama cha Mapinduzi, CCM, ni mwanzo wa safari ya kuondoka kwenye serikali mbili, kuelekea kwenye serikali moja!. Jee ndoto hii ya Mwalimu Nyerere, kwa Tanzania kuwa nchi moja ya JMT yenye serikali moja na rais mmoja, itakuja kutimia?.

Watanzania wanahitaji sana kuelimishwa kuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu, tena ni Rais Samia, ndie kiongozi wa kwanza wa juu aliyetoa ruhusa watu waachwe huru kujadili muungano. Baada ya muungano, nchi zote mbili zilitoweka, hakuna nchi ya Tanganyika wala hakuna nchi ya Zanzibar, bali nchi ya Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Zanzibar.

Elimu ya Uraia Kuhusu Muungano wetu adimu na adhimu!.
Duniani kuna miungano ya aina mbili Kuu,

1. Miungano ya union, nchi mbili au zaidi zinaungana kuunda nchi moja. Zile nchi zote zinakufa na inazaliwa nchi moja mpya.

2. Miungano ya federation, ni nchi mbili au zaidi zinaungana na kuunda nchi moja, ila zile nchi zote zinakuwa na serikali ya muungano, Federal Government na State Government, kila nchi ina utawala wake wa ndani.

Muungano wetu ni very unique, ndio maana unaitwa muungano adimu na adhimu, kwasababu ni muungano pekee duniani ambao upande mmoja ni muungano wa union kwa nchi mbili kuungana kuunda nchi moja ya JMT, na upande wa pili ni muungano wa federation wenye serikali mbili, marais wawili, mabunge mawili na mahakama mbili.

Muungano wetu kimataifa ni muungano wa union, Tanzania kimataifa ni nchi moja ya JMT, yenye serikali moja ya JMT, chini ya rais mmoja wa JMT, ambaye ni mkuu wan chi, mkuu wa serikali na amiri jeshi mkuu.

Lakini Kitaifa, nchi ya Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye sehemu mbili, Tanzania Bara na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar, yenye katiba mbili, katiba ya JMT, na katiba ya Zanzibar, yenye serikali mbili, serikali ya JMT na serikali ya Zanzibar, SMZ, yenye marais wawili, rais wa JMT na rais wa Zanzibar

Mkanganyiko wa Katiba.

Kama nilivyosema kimataifa Tanzania ni nchi moja ya JMT, hakuna mkanganyiko wowote wa kimataifa kuhusu Tanzania.

Lakini Kitaifa kuna mkanganyiko wa katiba kati ya katiba ya JMT na katiba ya Zanzibar.
Kwa mujibu wa katiba ya JMT, ya mwaka 1977, Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye sehemu mbili, Tanzania Bara na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar. Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, inaiita Zanzibar ni nchi, ni moja ya nchi mbili zinazounda JMT!. Kitendo cha katiba ya Zanzibar kuuita Zanzibar ni nchi, kinawakanganya Watanzania kudhani kuwa nchi ya Tanganyika ndio pekee iliyokufa ila nchi ya Zanzibar ipo haikufa.

Naomba niwahakikishie Tanzania ni nchi moja ya JMT, ile nchi inayotajwa na katiba ya Zanzibar kuwa ni nchi ya Zanzibar, sii kweli kuwa Zanzibar ni nchi, bali ni jina tuu, hayo mabadiliko ya katiba ya Zanzibar kujiita nchi, kimuungano ni mabadiko batili, ila, kwa vile mabadiliko hayo ni kwaajili ya Zanzibar tuu, na hayatambuliwi na katiba ya JMT, serikali ya JMT, imeamua kuyapuuza!, lakini kufuatia hizi kelele, tutapuuza mpaka lini?. Si ni bora twende kwenye serikali moja, haya yote yaishe?.

Hitimisho
Kwa vile Rais Samia, anakwenda kutupatia katiba mpya, nashauri hili la mkanganyika wa katiba kati ya katiba ya JMT na Katiba ya Zanzibar, pia litarekebishwa, na kwa maoni yangu, dawa pekee ya uhakika na ya kudumu ambayo ni mwarobaini wa kuzimaliza kero zote za muungano, ni kwenda kwenye serikali moja. Nimalizie na hili swali, je, Tanzania sasa tumefika wakati wa kutimiza ndoto ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, ya uzalendo wa kweli wa JMT, wa kwenda kwenye nchi moja, yenye serikali moja na rais mmoja?

Hongera kwa miaka 60 ya Muungano wetu adimu na adhimu,
Sasa twende kwenye nchi moja, serikali moja na rais mmoja!.

Mungu Ibariki Tanzania.

Paskali
Rejea za mwandishi kuhusu muungano na serikali moja.
Serikali moja haiwezi kuwa dawa kwa sababu Zanzibar itakataa. Mwalimu alisema Karume alitaka serikali moja lakini yeye alikataa kwa hofu ya kuonekana Tanganyika imeimeza Zanzibar. Kwa vile Muungano hauwezi kuwa wa kulazimisha, hiyo ya serikali moja ni DOA.

Muungano wa serikali tatu nao ni kiini macho na hauwezekani kwa sababu Zanzibar wanataka full sovereignity ambayo ni pamoja na kiti UN na kwenye mashirika mengine ya kitaifa, balozi zake ( ukiwa na kiti UN ni lazima uwe na ubalozi wako), country code yao n.k. Hawasemi sasa lakini bila shaka huko mbeleni watataka kuwa na sarafu yao. Kingine ni kuwa wanataka huo Muungano uwe wa Mkataba kuwa kila baada ya kipindi fulani unaangaliwa upya kama unastahili kuendelea kuwepo. Tanganyika nayo ikiwa na vyote hivyo hapatakuwa na Muungano maana Jamhuri ya Muungano haiwezi nayo kuwa na kiti UN, country code yake na sarafu yake. Haiwezekani kuwa na Muungano wa nchi mbili ambao serikali ya Muungano inakuwa haina meno. Itafika wakati Rais wa Tanganyika au wa Zanzibar wataweza kukataa kuchangia bajeti ya serikali ya Muungano. Aidha, serikali ya Muungano haitaweza kuingia kwenye mikataba ya kimataifa hakuna mtu anajua hatma yake baada ya muda fulani. Kuliko kupoteza muda na aina hii ya Muungano ni heri Muungano uliokuwepo uvunjwe na kila mmoja achukue fito zake. Mfumo huu unaweza kufanikiwa pale tuu ambapo serikali za Zanzibar na Tanganyika zitakuwa kama serikali za majimbo ( mifano hai ni Marekani, India, Canada, UK n.k.) na serikali ya muungano ndio itakuwa na full sovereignity ( itasimamia mahusiano yote na nchi nyingine, ulinzi wa mipaka yake, uchumi, miongozo ya kisera katika masuala ya elimu, miundombinu n.k).

Muungano wa serikali mbili ndio pekee unaweza kuwa na uhai kwa sharti kwamba Zanzibar isahau dai lao la kuwa sovereign country na ikubali kuwa ni junior partner. Hali iliyopo ya kuipa serikali usawa na serikali ya JMT sio sustainable maana kila siku watanganyika wataona wananyonywa na wazanzibari wataona wanatawaliwa na watanganyika.

Kwa matazamo wangu ni kuwa hamna muundo ambao ni sustainable bila ya pande zote mbili kutambua kuwa katika Muungano kila moja itabidi ipoteze sovereignity yake. Kama hilo haliwezekani ni bora mapema tuu tukubaliane kutengana ili kila nchi iende kivyake. Tahadhari ni kuwa tusijidanganye kuwa baada ya kutengana uhusiano wetu utabaki kama ulivyo. Tukumbuke vidonda vilivyoachwa baada ya kuvunjika kwa EAC vilichukua muda mrefu kupona. Kuvunjika kwa JMT itakuwa hivyo hivyo.

Amandla...
 
Wanabodi,

Loe nchi yetu tumeadhimisha miaka 60 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, na kuwa nchi moja ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Muungano wetu ni muungano adimu na muungano adhimu, kwasababu hapa duniani hakuna muungano mwingine wowote kama huu muungano wetu. Ni muungano wa nchi mbili kuungana na kuunda nchi moja ya JMT, yenye nchi mbili ndani yake, Tanzania na Zanzibar, wenye marais wawili, rais wa JMT na Rais wa Zanzibar, wenye Katiba mbili, katiba ya JMT na Katiba ya Zanzibar, wenye mabunge mawili, Bunge la JMT na Baraza la Wawakilishi, lenye mahakama mbili, mahakama kuu ya Tanzania na Mahakama kuu ya Zanzibar. Kwa maoni yangu, muungano wa aina hii kudumu kwa miaka 60, itoshe, sasa twende kwenye muungano kamili wa nchi moja, serikali moja na rais mmoja!.

Kuungana kwa TANU na ASP
Vyama vya TANU na ASP vilipoungana ile 1977, sii wengi humu walikuwa wamezaliwa!, wengi humu wamezaliwa, wameikuta CCM, hawakuikuta TANU na ASP, hivyo hawajui kwanini TANU na ASP viliungana, na viliungana ili iweje?.

Mimi ni mtu wa 60s, hivyo ile 1977, TANU na ASP zilipoungana nilikuwa darasa la tatu, kijijini Itonjanda, nikikaa kwa bibi mzaa Baba, Bibi Wakawombwe, (RIP) baada ya Baba Mzee Mayalla(RIP) kuhusika na yale mambo fulani ya Mwanza ya 1976!.

Sababu ya TANU na ASP kuungana, ni kuelekea kwenye serikali moja!. Baba wa taifa, Mwalimu Nyerere alisema huu muungano wa vyama vya TANU na ASP na kuzaliwa chama kipya, Chama cha Mapinduzi, CCM, ni mwanzo wa safari ya kuondoka kwenye serikali mbili, kuelekea kwenye serikali moja!. Jee ndoto hii ya Mwalimu Nyerere, kwa Tanzania kuwa nchi moja ya JMT yenye serikali moja na rais mmoja, itakuja kutimia?.

Watanzania wanahitaji sana kuelimishwa kuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu, tena ni Rais Samia, ndie kiongozi wa kwanza wa juu aliyetoa ruhusa watu waachwe huru kujadili muungano. Baada ya muungano, nchi zote mbili zilitoweka, hakuna nchi ya Tanganyika wala hakuna nchi ya Zanzibar, bali nchi ya Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Zanzibar.

Elimu ya Uraia Kuhusu Muungano wetu adimu na adhimu!.
Duniani kuna miungano ya aina mbili Kuu,

1. Miungano ya union, nchi mbili au zaidi zinaungana kuunda nchi moja. Zile nchi zote zinakufa na inazaliwa nchi moja mpya.

2. Miungano ya federation, ni nchi mbili au zaidi zinaungana na kuunda nchi moja, ila zile nchi zote zinakuwa na serikali ya muungano, Federal Government na State Government, kila nchi ina utawala wake wa ndani.

Muungano wetu ni very unique, ndio maana unaitwa muungano adimu na adhimu, kwasababu ni muungano pekee duniani ambao upande mmoja ni muungano wa union kwa nchi mbili kuungana kuunda nchi moja ya JMT, na upande wa pili ni muungano wa federation wenye serikali mbili, marais wawili, mabunge mawili na mahakama mbili.

Muungano wetu kimataifa ni muungano wa union, Tanzania kimataifa ni nchi moja ya JMT, yenye serikali moja ya JMT, chini ya rais mmoja wa JMT, ambaye ni mkuu wan chi, mkuu wa serikali na amiri jeshi mkuu.

Lakini Kitaifa, nchi ya Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye sehemu mbili, Tanzania Bara na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar, yenye katiba mbili, katiba ya JMT, na katiba ya Zanzibar, yenye serikali mbili, serikali ya JMT na serikali ya Zanzibar, SMZ, yenye marais wawili, rais wa JMT na rais wa Zanzibar

Mkanganyiko wa Katiba.

Kama nilivyosema kimataifa Tanzania ni nchi moja ya JMT, hakuna mkanganyiko wowote wa kimataifa kuhusu Tanzania.

Lakini Kitaifa kuna mkanganyiko wa katiba kati ya katiba ya JMT na katiba ya Zanzibar.
Kwa mujibu wa katiba ya JMT, ya mwaka 1977, Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye sehemu mbili, Tanzania Bara na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar. Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, inaiita Zanzibar ni nchi, ni moja ya nchi mbili zinazounda JMT!. Kitendo cha katiba ya Zanzibar kuuita Zanzibar ni nchi, kinawakanganya Watanzania kudhani kuwa nchi ya Tanganyika ndio pekee iliyokufa ila nchi ya Zanzibar ipo haikufa.

Naomba niwahakikishie Tanzania ni nchi moja ya JMT, ile nchi inayotajwa na katiba ya Zanzibar kuwa ni nchi ya Zanzibar, sii kweli kuwa Zanzibar ni nchi, bali ni jina tuu, hayo mabadiliko ya katiba ya Zanzibar kujiita nchi, kimuungano ni mabadiko batili, ila, kwa vile mabadiliko hayo ni kwaajili ya Zanzibar tuu, na hayatambuliwi na katiba ya JMT, serikali ya JMT, imeamua kuyapuuza!, lakini kufuatia hizi kelele, tutapuuza mpaka lini?. Si ni bora twende kwenye serikali moja, haya yote yaishe?.

Hitimisho
Kwa vile Rais Samia, anakwenda kutupatia katiba mpya, nashauri hili la mkanganyika wa katiba kati ya katiba ya JMT na Katiba ya Zanzibar, pia litarekebishwa, na kwa maoni yangu, dawa pekee ya uhakika na ya kudumu ambayo ni mwarobaini wa kuzimaliza kero zote za muungano, ni kwenda kwenye serikali moja. Nimalizie na hili swali, je, Tanzania sasa tumefika wakati wa kutimiza ndoto ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, ya uzalendo wa kweli wa JMT, wa kwenda kwenye nchi moja, yenye serikali moja na rais mmoja?

Hongera kwa miaka 60 ya Muungano wetu adimu na adhimu,
Sasa twende kwenye nchi moja, serikali moja na rais mmoja!.

Mungu Ibariki Tanzania.

Paskali
Rejea za mwandishi kuhusu muungano na serikali moja.
Nimependa umefanya ufafanuzi rahisi kila mmoja kuelewa!
 
Serikali moja haiwezi kuwa dawa kwa sababu Zanzibar itakataa. Mwalimu alisema Karume alitaka serikali moja lakini yeye alikataa kwa hofu ya kuonekana Tanganyika imeimeza Zanzibar. Kwa vile Muungano hauwezi kuwa wa kulazimisha, hiyo ya serikali moja ni DOA.

Muungano wa serikali tatu nao ni kiini macho na hauwezekani kwa sababu Zanzibar wanataka full sovereignity ambayo ni pamoja na kiti UN na kwenye mashirika mengine ya kitaifa, balozi zake ( ukiwa na kiti UN ni lazima uwe na ubalozi wako), country code yao n.k. Hawasemi sasa lakini bila shaka huko mbeleni watataka kuwa na sarafu yao. Kingine ni kuwa wanataka huo Muungano uwe wa Mkataba kuwa kila baada ya kipindi fulani unaangaliwa upya kama unastahili kuendelea kuwepo. Tanganyika nayo ikiwa na vyote hivyo hapatakuwa na Muungano maana Jamhuri ya Muungano haiwezi nayo kuwa na kiti UN, country code yake na sarafu yake. Haiwezekani kuwa na Muungano wa nchi mbili ambao serikali ya Muungano inakuwa haina meno. Itafika wakati Rais wa Tanganyika au wa Zanzibar wataweza kukataa kuchangia bajeti ya serikali ya Muungano. Aidha, serikali ya Muungano haitaweza kuingia kwenye mikataba ya kimataifa hakuna mtu anajua hatma yake baada ya muda fulani. Kuliko kupoteza muda na aina hii ya Muungano ni heri Muungano uliokuwepo uvunjwe na kila mmoja achukue fito zake. Mfumo huu unaweza kufanikiwa pale tuu ambapo serikali za Zanzibar na Tanganyika zitakuwa kama serikali za majimbo ( mifano hai ni Marekani, India, Canada, UK n.k.) na serikali ya muungano ndio itakuwa na full sovereignity ( itasimamia mahusiano yote na nchi nyingine, ulinzi wa mipaka yake, uchumi, miongozo ya kisera katika masuala ya elimu, miundombinu n.k).

Muungano wa serikali mbili ndio pekee unaweza kuwa na uhai kwa sharti kwamba Zanzibar isahau dai lao la kuwa sovereign country na ikubali kuwa ni junior partner. Hali iliyopo ya kuipa serikali usawa na serikali ya JMT sio sustainable maana kila siku watanganyika wataona wananyonywa na wazanzibari wataona wanatawaliwa na watanganyika.

Kwa matazamo wangu ni kuwa hamna muundo ambao ni sustainable bila ya pande zote mbili kutambua kuwa katika Muungano kila moja itabidi ipoteze sovereignity yake. Kama hilo haliwezekani ni bora mapema tuu tukubaliane kutengana ili kila nchi iende kivyake. Tahadhari ni kuwa tusijidanganye kuwa baada ya kutengana uhusiano wetu utabaki kama ulivyo. Tukumbuke vidonda vilivyoachwa baada ya kuvunjika kwa EAC vilichukua muda mrefu kupona. Kuvunjika kwa JMT itakuwa hivyo hivyo.

Amandla...
Mkuu Fundi Mchundo, asante sana kwa objectivity yako kwenye hili.
P
 
Serikali moja haiwezi kuwa dawa kwa sababu Zanzibar itakataa. Mwalimu alisema Karume alitaka serikali moja lakini yeye alikataa kwa hofu ya kuonekana Tanganyika imeimeza Zanzibar. Kwa vile Muungano hauwezi kuwa wa kulazimisha, hiyo ya serikali moja ni DOA.

Muungano wa serikali tatu nao ni kiini macho na hauwezekani kwa sababu Zanzibar wanataka full sovereignity ambayo ni pamoja na kiti UN na kwenye mashirika mengine ya kitaifa, balozi zake ( ukiwa na kiti UN ni lazima uwe na ubalozi wako), country code yao n.k. Hawasemi sasa lakini bila shaka huko mbeleni watataka kuwa na sarafu yao. Kingine ni kuwa wanataka huo Muungano uwe wa Mkataba kuwa kila baada ya kipindi fulani unaangaliwa upya kama unastahili kuendelea kuwepo. Tanganyika nayo ikiwa na vyote hivyo hapatakuwa na Muungano maana Jamhuri ya Muungano haiwezi nayo kuwa na kiti UN, country code yake na sarafu yake. Haiwezekani kuwa na Muungano wa nchi mbili ambao serikali ya Muungano inakuwa haina meno. Itafika wakati Rais wa Tanganyika au wa Zanzibar wataweza kukataa kuchangia bajeti ya serikali ya Muungano. Aidha, serikali ya Muungano haitaweza kuingia kwenye mikataba ya kimataifa hakuna mtu anajua hatma yake baada ya muda fulani. Kuliko kupoteza muda na aina hii ya Muungano ni heri Muungano uliokuwepo uvunjwe na kila mmoja achukue fito zake. Mfumo huu unaweza kufanikiwa pale tuu ambapo serikali za Zanzibar na Tanganyika zitakuwa kama serikali za majimbo ( mifano hai ni Marekani, India, Canada, UK n.k.) na serikali ya muungano ndio itakuwa na full sovereignity ( itasimamia mahusiano yote na nchi nyingine, ulinzi wa mipaka yake, uchumi, miongozo ya kisera katika masuala ya elimu, miundombinu n.k).

Muungano wa serikali mbili ndio pekee unaweza kuwa na uhai kwa sharti kwamba Zanzibar isahau dai lao la kuwa sovereign country na ikubali kuwa ni junior partner. Hali iliyopo ya kuipa serikali usawa na serikali ya JMT sio sustainable maana kila siku watanganyika wataona wananyonywa na wazanzibari wataona wanatawaliwa na watanganyika.

Kwa matazamo wangu ni kuwa hamna muundo ambao ni sustainable bila ya pande zote mbili kutambua kuwa katika Muungano kila moja itabidi ipoteze sovereignity yake. Kama hilo haliwezekani ni bora mapema tuu tukubaliane kutengana ili kila nchi iende kivyake. Tahadhari ni kuwa tusijidanganye kuwa baada ya kutengana uhusiano wetu utabaki kama ulivyo. Tukumbuke vidonda vilivyoachwa baada ya kuvunjika kwa EAC vilichukua muda mrefu kupona. Kuvunjika kwa JMT itakuwa hivyo hivyo.

Amandla...
mkuu bora wewe umeeleweka.
 
Wanabodi,

Loe nchi yetu tumeadhimisha miaka 60 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, na kuwa nchi moja ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Muungano wetu ni muungano adimu na muungano adhimu, kwasababu hapa duniani hakuna muungano mwingine wowote kama huu muungano wetu. Ni muungano wa nchi mbili kuungana na kuunda nchi moja ya JMT, yenye nchi mbili ndani yake, Tanzania na Zanzibar, wenye marais wawili, rais wa JMT na Rais wa Zanzibar, wenye Katiba mbili, katiba ya JMT na Katiba ya Zanzibar, wenye mabunge mawili, Bunge la JMT na Baraza la Wawakilishi, lenye mahakama mbili, mahakama kuu ya Tanzania na Mahakama kuu ya Zanzibar. Kwa maoni yangu, muungano wa aina hii kudumu kwa miaka 60, itoshe, sasa twende kwenye muungano kamili wa nchi moja, serikali moja na rais mmoja!.

Kuungana kwa TANU na ASP
Vyama vya TANU na ASP vilipoungana ile 1977, sii wengi humu walikuwa wamezaliwa!, wengi humu wamezaliwa, wameikuta CCM, hawakuikuta TANU na ASP, hivyo hawajui kwanini TANU na ASP viliungana, na viliungana ili iweje?.

Mimi ni mtu wa 60s, hivyo ile 1977, TANU na ASP zilipoungana nilikuwa darasa la tatu, kijijini Itonjanda, nikikaa kwa bibi mzaa Baba, Bibi Wakawombwe, (RIP) baada ya Baba Mzee Mayalla(RIP) kuhusika na yale mambo fulani ya Mwanza ya 1976!.

Sababu ya TANU na ASP kuungana, ni kuelekea kwenye serikali moja!. Baba wa taifa, Mwalimu Nyerere alisema huu muungano wa vyama vya TANU na ASP na kuzaliwa chama kipya, Chama cha Mapinduzi, CCM, ni mwanzo wa safari ya kuondoka kwenye serikali mbili, kuelekea kwenye serikali moja!. Jee ndoto hii ya Mwalimu Nyerere, kwa Tanzania kuwa nchi moja ya JMT yenye serikali moja na rais mmoja, itakuja kutimia?.

Watanzania wanahitaji sana kuelimishwa kuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu, tena ni Rais Samia, ndie kiongozi wa kwanza wa juu aliyetoa ruhusa watu waachwe huru kujadili muungano. Baada ya muungano, nchi zote mbili zilitoweka, hakuna nchi ya Tanganyika wala hakuna nchi ya Zanzibar, bali nchi ya Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Zanzibar.

Elimu ya Uraia Kuhusu Muungano wetu adimu na adhimu!.
Duniani kuna miungano ya aina mbili Kuu,

1. Miungano ya union, nchi mbili au zaidi zinaungana kuunda nchi moja. Zile nchi zote zinakufa na inazaliwa nchi moja mpya.

2. Miungano ya federation, ni nchi mbili au zaidi zinaungana na kuunda nchi moja, ila zile nchi zote zinakuwa na serikali ya muungano, Federal Government na State Government, kila nchi ina utawala wake wa ndani.

Muungano wetu ni very unique, ndio maana unaitwa muungano adimu na adhimu, kwasababu ni muungano pekee duniani ambao upande mmoja ni muungano wa union kwa nchi mbili kuungana kuunda nchi moja ya JMT, na upande wa pili ni muungano wa federation wenye serikali mbili, marais wawili, mabunge mawili na mahakama mbili.

Muungano wetu kimataifa ni muungano wa union, Tanzania kimataifa ni nchi moja ya JMT, yenye serikali moja ya JMT, chini ya rais mmoja wa JMT, ambaye ni mkuu wan chi, mkuu wa serikali na amiri jeshi mkuu.

Lakini Kitaifa, nchi ya Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye sehemu mbili, Tanzania Bara na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar, yenye katiba mbili, katiba ya JMT, na katiba ya Zanzibar, yenye serikali mbili, serikali ya JMT na serikali ya Zanzibar, SMZ, yenye marais wawili, rais wa JMT na rais wa Zanzibar

Mkanganyiko wa Katiba.

Kama nilivyosema kimataifa Tanzania ni nchi moja ya JMT, hakuna mkanganyiko wowote wa kimataifa kuhusu Tanzania.

Lakini Kitaifa kuna mkanganyiko wa katiba kati ya katiba ya JMT na katiba ya Zanzibar.
Kwa mujibu wa katiba ya JMT, ya mwaka 1977, Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye sehemu mbili, Tanzania Bara na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar. Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, inaiita Zanzibar ni nchi, ni moja ya nchi mbili zinazounda JMT!. Kitendo cha katiba ya Zanzibar kuuita Zanzibar ni nchi, kinawakanganya Watanzania kudhani kuwa nchi ya Tanganyika ndio pekee iliyokufa ila nchi ya Zanzibar ipo haikufa.

Naomba niwahakikishie Tanzania ni nchi moja ya JMT, ile nchi inayotajwa na katiba ya Zanzibar kuwa ni nchi ya Zanzibar, sii kweli kuwa Zanzibar ni nchi, bali ni jina tuu, hayo mabadiliko ya katiba ya Zanzibar kujiita nchi, kimuungano ni mabadiko batili, ila, kwa vile mabadiliko hayo ni kwaajili ya Zanzibar tuu, na hayatambuliwi na katiba ya JMT, serikali ya JMT, imeamua kuyapuuza!, lakini kufuatia hizi kelele, tutapuuza mpaka lini?. Si ni bora twende kwenye serikali moja, haya yote yaishe?.

Hitimisho
Kwa vile Rais Samia, anakwenda kutupatia katiba mpya, nashauri hili la mkanganyika wa katiba kati ya katiba ya JMT na Katiba ya Zanzibar, pia litarekebishwa, na kwa maoni yangu, dawa pekee ya uhakika na ya kudumu ambayo ni mwarobaini wa kuzimaliza kero zote za muungano, ni kwenda kwenye serikali moja. Nimalizie na hili swali, je, Tanzania sasa tumefika wakati wa kutimiza ndoto ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, ya uzalendo wa kweli wa JMT, wa kwenda kwenye nchi moja, yenye serikali moja na rais mmoja?

Hongera kwa miaka 60 ya Muungano wetu adimu na adhimu,
Sasa twende kwenye nchi moja, serikali moja na rais mmoja!.

Mungu Ibariki Tanzania.

Paskali
Rejea za mwandishi kuhusu muungano na serikali moja.
Mpaka pale wazanzibar watakapo amua kuukana utaifa wao maana sisi watanganyika tumeshachoka kutanga na nyika..
 
Back
Top Bottom