billionea alpha
JF-Expert Member
- Apr 10, 2014
- 1,444
- 1,647
Piga chini, hiyo ng'ombe. Usithubutu kumrudia....Jumamosi ya leo kwangu ni njema sana! Namshukuru Mungu wa mbinguni, pole sana kwa ndugu zetu mnaopitia magumu, Mungu atawasaidia aminini.
Wakuu ni muda wa miaka kadhaa nilikuwa na binti mmoja nikaingia nae kwenye mahusiano yasiyo kuwa rasmi, baadae niliamua kwenda kwao kujitambulisha sababu tayari alikuwa mjamzito, nilipokelewa hadi hatua za kutoa posa na kupangiwa mahari, tuliendelea kukaa kwa furaha sababu nilikuwa nampenda na yeye alionyesha upendo na wakati huo nilikuwa na kibarua sehemu fulani.
Ilifikia muda nikapata shida kazini nikapoteza kazi, hapo ndipo nilianza kuona picha za rangi zote, dharau, kejeri, kunyimwa papuchi, sometimes hapiki chakula najipikia, kwao wakaniandama sana, kiufupi sikupata ahueni yeyote nilipohitaji kuwashirikisha kuhusu tabia zake, wote walinikataa kiaina.
Alifikia hatua ya kujifungua nikiwa nae bado nilihudumia kadri ya uwezo huku nikiugulia moyoni kwa machungu, sikuwa na ajira japo nina elimu ya juu na yeye alikuwa anafanya kazi hadi sasa.
Kiufupi kama mwanaume mpambanaji niliamua kutoka hiyo sehemu na kwenda kutafuta niliamuacha aendelee na maisha yake.
Hivi karibuni nilirudi huo mkoa na anafahamu napoishi na mambo yangu yameanza kunyooka maana niliamua kujiajiri, naona sasa anajisogeza sana hapo ni baada ya kuwa nimeanza kuongeza kiwango cha matumizi kwa mtoto na amepata taarifa kwa watu na mengine kajionea mwenyewe kwamba kwa sasa niko na ahueni hata zaidi ya alivyonikuta mwanzo.
Kimbembe kimeanza anataka nikatoe mahari kwao nimchukue tuishi tena pamoja lakini mimi moyo wangu hautaki kabisa na kwa sasa niko na imekuwa ni simu na sms nyingi sana kutoka kwake na akionana na watu wanaonifahamu anaanza kunimwagia sifa.
Kiukweli wakati naondoka kwenye maisha yake hatukuachana vizuri ilikuwa ni fukuto kweli kweli, yaani mambo yalikuwa mengi siwezi kuyaeleza yote mengine yaliniliza kwa uchungu wa kukosa pesa na kudhalilishwa sana na huyu mwanamke.
Kila nikienda kumsalimia mtoto nashikwa uchungu why niko mbali na mtoto wangu isitoshe ndiye wa kwanza, na mtoto keshaanza shule na ananipenda sana ni kawaida kunililia nikiwa namuaga!
Nikikumbuka matendo ya huyu binti aliyonifanyia ndani ya mwaka 1 wa madhiha na uvumilivu wa hali ya juu hadi kufikia kumchoka akilini mwangu, nikiwaza kumrudia roho inagoma maana nafikiria siku nikiyumba tena yatarudi yaleyale.
Familia yake ameshawambia haya yote nao naona wameanza kumwambia aniombe nikatoe mahari ili tuishi tulee mtoto.
Wakuu pointi ya msingi nakuwa matatani kufanya maamuzi hasa nikikumbuka matendo aliyonifanyia na nikimuona mtoto wangu ndo kabisaaa akili inahama, naombeni ushauri wenu.
By Chumvi YMawe