Uratibu mbaya wa makadirio ya kodi ndiyo sababu kubwa ya ukwepaji kodi

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,626
8,802
Mimi ni mtaalamu wa fedha na kwa mawazo yangu tatizo la kodi na TRA linaanza na uratatibu mbaya wa ukusanyaji wa kodi. Kuna kodi za aina mbili kubwa

1. Kodi za mauzo. Kwenye kodi hizi ambazo kwa ulewa wangu ni 18% mlipa kodi sio mfanyabiashara mfano mwenye duka. Mlipa kodi ni mnunuzi na mwenye biashara anatakiwa kuweka kodi pembeni na kuwapa TRA kisheria au kwa lugha ya kitaalamu hii kodi ni withholding tax. Sasa kuna watu wanafikiri mlipa kodi hii ni mwenye duka na imefika wakati mpaka wauzaji wanafikiri wenyewe ni walipa kodi hii kumbe sio hivyo mlipa kodi ni mnunuzi. Hivyo mfanyabiashara anauza kitu Tsh 1000 anatakiwa aweke kodi ya 18% na mnunuzi kulipa Tsh 1,180 na hiyo Tsh 180 hajalipa yeye ni mnunuzi na sio pesa yake.

2. Kodi ya mapato ni kodi za wafanyabiashara. Hizi ni kodi ambazo zinatoka kwenye faida ya biashara. Yaani baada ya mfanyabiashara kutoa matumizi yote na kubali na faidi kuna kodi anatakiwa kulipa ya mapato. Sina uhakika na % lakini inatokana na ukuwa na aina ya biashara. Kama una hasara hutakiwi kulipa kodi.

Tatizo Tanzania ni hizo kodi za namba 1. Mtu wa TRA badala ya kukagua vitabu vya risiti anaenda kwa mfanyabiashara na makadirio. Sasa makadirio ya nini wakati sheria inataka kila mtu atoe risiti. Na kama kuna risiti basi kiasi cha kodi kinajulikana kuna haja gani tena kuwatuma wafanyakazi na makadirio. Sasa mfano risiti zinaonyesha kodi ambazo wateja wamelipa za kwenda serikalini ni Tsh 10M hawa mafisadi wa TRA wanakuja na makadirio ambayo hatujui yametoka wapi ya kodi ya Tsh 20M halafu wanamwambia mwenye biashara kwamba tupe Tsh 2M halafu lipa kodi Tsh 5M Hivyo serikali inapungukiwa Tsh 3M. Lakini kibaya zaidi mwizi huyo huyo bado analipwa pesa na mshahara wake kwenye hiyo Tsh 7M. Sasa kama nchi tutaendeleo vipi kwa utaratibu huu?

1. Serikali badilisheni utaratibu toeni ujinga wa makadirio
2. Wekeni sheria kali kwa wala rushwa
3. Wekeni sheria kali kwa wafanyabiashara watoa rushwa mfano toeni hongera kama mfanyabiashara akiweza kumleta mla rushwa
4. Wekeni utamaduni na onyo kwa utamaduni wa rushwa
 
Kodi lazima ikadiriwe halafu wewe utaitetea kwa accounts zako kwa Sababu provisionally unakuwa ulijikadiria wewe mwenyewe

Tunza kumbukumbu zako vizuri
Kama nimeshalipa instalment 3, ile ya mwisho si inabidi accounts zangu zipitiwe kuona nilitengeneza faida kiasi gani? Makadirio yanaingiaje hapo!
 
Mkuu kuna Point fulani Unayo ila sasa Jinsi ulivoiweka Hata TRA hawataelewa.

Kwanza nianze na Utaratibu wa Makadirio,

Utaratibu wa makadirio una utaratibu wake na Kanuni zake.Kuna threshold za Kiwango cha Mapato na kiasi cha kodi unayopaswa kulipa.Sasa kwenye kuamua kiwango cha mapato TRA wanatumia vyanzo mbalimbali vya Taarifa zikiwamo Taarifa zinaotolewa na walipa kodi wenyewe,aina ya biashara,eneo la biashara na wakati mwingine hali ya kiuchumi.Sasa katika kufanya hivyo unaona kabisa kwamba Upo Utaratibu mzuri na Rahisi wa kuweza kusimamia Hiyo kodi ya Makadirio.

Sasa Tatizo ni nn?
Kwanza Tatizo ni Watanzania kutokuelewa kuhusu elimu ya kodi na sheria za kodi pamoja na haki zao kama walipa kodi na wajibu wao kama walipa kodi.

Suluhisho:
Suala kama hilo haliwezi kurekebishwa kwa sheria kali wali amri kali.Ni suala ambalo litachukua muda likihitaji wananchi kuendelea kujifunza na TRA nao kuendelea kujifunza na kuboresha Huduma zao.

Swala la Pili ni kuhusu hiyo kodi ya 18% ambayo inaitwa VAT,Kwanza tuelewe kwamba kodi ya VAT au kama inavyoitwa Sales TAX lengo lake kubwa ni kupanua wigo wa ulipaji wa kodi na kurahisisha ukusanyaji wa kodi.Kodi ya VAT inatozwa kwa assumtion kwamba yule mlaji wa Mwisho Ndio atakuwa mlipaji.Sasa Tafsiri ya Mlaji wa mwisho ni nani ndipo ambapo watu inabidi waelewe.Kwa mfano,Ukienda Sokoni ukanunua Mboga au uakaenda dukani kwa mangi ukanunua Bidhaa ambayo inatozwa VAT(Zinagatia kwamba sio kila bidhaa inatozwa VAT) basi ufahamu kwamba Wewe ambaye unaenda kutumia bidhaa hiyo Ndio Mlipaji.Hata kama utapewa Risit ambayo haina VAT bado wewe ni mlaji wa Mwisho.Yule Muuzaji wa Duka kwa sababu Yeye hajasajiliwa na VAT naye ni Mlaji wa Mwisho katika Mtazamo wa Kikodi mpaka atakapokuwa amesajiliwa kukusanya VAT.Kwa mtu ambaye amesajiliwa VAT yeye ataidai Mamlaka ya Mapato Ile Tofauti ya Kodi kati ya Makusanyo yake kutokana na Mauzo na Manunuzi ambapo iwapo Manunuzi yatazidi ila iwapo mauzo ndio yatazidi basi Ile Tofauti ya VAt atapaswa kulipa TRA.

Kwa wale ambao wanatuza kumbukumbu za Hesabu wao huwa wanao wajibu wa kuandaa HESABU za MWAKA kwa kupita Wahasibu na Wakaguzi pamoja na Wataalamu wa KODI ambao wamesajiliwa na TRA na NBAA ili waweze kupigiwa HESABU ya KODI Kikamilifu.

Baada ya kuchangia Mada hii kwa ujumla wake sasa nitoe Maoni ya Ujumla kuhusu Mfumo wetu wa KIKODI na namna ambavyo unaweza kurekebishwa:

  1. Swala la kwanza ni Viwango vyetu vya kodi,Kiwango cha Kodi ya Mapato kwa Tanzania ni 30% hiki ni kiwango kikubwa sana kwa aina ya uchumi tulio nao.Nasema nikiwango kikubwa kwa sababu kiwango hiki hakihamasishi ukuaji wa Biashara na kinaathiri sana gharam za uendeshaji hasa ukizingatia kwamba kuna gharama nyingi ambazo ni za kikodi ambazo kwa sasa zinaitwa TOZO ambazo zimeingizwa katika mfumo wetu wa Biashara.Ukitazama kwa ukaribu utaona kwamba Serikali ambayo haitoi vihamasishi vyovyote kwa wafanyabiashara inawatoza wafanyabiashara kodi ya 30% kisha kuna kuwa na gharama nyingine nyingi ambazo mfanyabiashara analipa kwa serikali hiyo hiyo.Ukija ukitazama unakuta Majukumu ya Compliance tu yanamgharimu mfanyabiashara zaidi ya 5% au zaidi ya mapato yake.Kitu serikali inaweza fanya ni Kupunguza Kiwango Cha Kodi ya Mapato kutoka 30% mpaka 15 au 20% na kisha kufanya VAT iwe Single DIGIT.Baada ya Hapo Biashara zote zilazimike kuwa na EFD regardless of SIZE na LOCATION na ihamasishe Digital Payment kwa kuondokana na TOZO za moja kwa moja katika Miamala ya Malipo kwa njia mtandao na zibaki standard charges.
  2. Swala la Pili ni Mifumo;Serikali iondokana kabisa na Suala la Mfanyakazi wa TRA kumfanyia Mjasiriamali Makadirio ya KODI.Kama kuna viwango elekezi viwekwe kwenye Mfumo na Kila Mtu awe na uwezo wa kutazama masuala yake ya kikodi na kuyasimamia Peke yake.TRA wafanye Monitoring ya Mifumo na iwapo kuna dalili z ukwepaji basi hapo ndipo waingilie kati.Unaporuhusu watu kukutana na kuanza kuneogotiate ndipo mazingira ya Rushwa yanapokuwepo.
All in all niwapongeze TRA kwa MFumo wao mpya ingawa bado una changamoto na unahitaji maboresho.Wajitahidi sana kuufanya huu mfumo uwe Intelligent System Yaani uwe na uwezo wa kujifunza kulingana na Data za walipa kodi wengine,location za walipa kodi wengine na taarifa nyingine za mlipa kodi.Teknoljia zipo na ninaamini kabisa kwamba wanaweza wakiwa na nia ya dhati.Yako Mengi sana ambayo ninayaona ila kwa leo tuanze na hayo na wengine nao wajdili
 
Kama nimeshalipa instalment 3, ile ya mwisho si inabidi accounts zangu zipitiwe kuona nilitengeneza faida kiasi gani? Makadirio yanaingiaje hapo!
Accounts zinatengenezwa annually

Ukishafunga mwaka wako wa kiuhasibu ndio unawasilisha returns zako TRA nadhani kuna grace period ya miezi 3 ukichelewa ndio utakutana na Estimated Final Assessment lakini ukiwahisha assessment Yako itatoka kulingana na accounts na Baada ya ukaguzi wa hizo Financial statements ndio itajulikana tax halali unayopaswa kulipa

1.Ukiwasilisha return utapata Final Assessment as per Accounts

2. Na Baada ya ukaguzi unaweza kupokea Additional Final Assessment after examination of Accounts

Ni kawaida Sana 😀
 
Kama nimeshalipa instalment 3, ile ya mwisho si inabidi accounts zangu zipitiwe kuona nilitengeneza faida kiasi gani? Makadirio yanaingiaje hapo!
Kwanza kila installment kabla hujalipa ni muhimu upitie hesabu zako uone kama kuna ziada ya kodi au kuna Pungufu ya Kodi Hii inakusaidia sana katika TAX planning.
 
Mkuu kuna Point fulani Unayo ila sasa Jinsi ulivoiweka Hata TRA hawataelewa.

Kwanza nianze na Utaratibu wa Makadirio,

Utaratibu wa makadirio una utaratibu wake na Kanuni zake.Kuna threshold za Kiwango cha Mapato na kiasi cha kodi unayopaswa kulipa.Sasa kwenye kuamua kiwango cha mapato TRA wanatumia vyanzo mbalimbali vya Taarifa zikiwamo Taarifa zinaotolewa na walipa kodi wenyewe,aina ya biashara,eneo la biashara na wakati mwingine hali ya kiuchumi.Sasa katika kufanya hivyo unaona kabisa kwamba Upo Utaratibu mzuri na Rahisi wa kuweza kusimamia Hiyo kodi ya Makadirio.

Sasa Tatizo ni nn?
Kwanza Tatizo ni Watanzania kutokuelewa kuhusu elimu ya kodi na sheria za kodi pamoja na haki zao kama walipa kodi na wajibu wao kama walipa kodi.

Suluhisho:
Suala kama hilo haliwezi kurekebishwa kwa sheria kali wali amri kali.Ni suala ambalo litachukua muda likihitaji wananchi kuendelea kujifunza na TRA nao kuendelea kujifunza na kuboresha Huduma zao.

Swala la Pili ni kuhusu hiyo kodi ya 18% ambayo inaitwa VAT,Kwanza tuelewe kwamba kodi ya VAT au kama inavyoitwa Sales TAX lengo lake kubwa ni kupanua wigo wa ulipaji wa kodi na kurahisisha ukusanyaji wa kodi.Kodi ya VAT inatozwa kwa assumtion kwamba yule mlaji wa Mwisho Ndio atakuwa mlipaji.Sasa Tafsiri ya Mlaji wa mwisho ni nani ndipo ambapo watu inabidi waelewe.Kwa mfano,Ukienda Sokoni ukanunua Mboga au uakaenda dukani kwa mangi ukanunua Bidhaa ambayo inatozwa VAT(Zinagatia kwamba sio kila bidhaa inatozwa VAT) basi ufahamu kwamba Wewe ambaye unaenda kutumia bidhaa hiyo Ndio Mlipaji.Hata kama utapewa Risit ambayo haina VAT bado wewe ni mlaji wa Mwisho.Yule Muuzaji wa Duka kwa sababu Yeye hajasajiliwa na VAT naye ni Mlaji wa Mwisho katika Mtazamo wa Kikodi mpaka atakapokuwa amesajiliwa kukusanya VAT.Kwa mtu ambaye amesajiliwa VAT yeye ataidai Mamlaka ya Mapato Ile Tofauti ya Kodi kati ya Makusanyo yake kutokana na Mauzo na Manunuzi ambapo iwapo Manunuzi yatazidi ila iwapo mauzo ndio yatazidi basi Ile Tofauti ya VAt atapaswa kulipa TRA.

Kwa wale ambao wanatuza kumbukumbu za Hesabu wao huwa wanao wajibu wa kuandaa HESABU za MWAKA kwa kupita Wahasibu na Wakaguzi pamoja na Wataalamu wa KODI ambao wamesajiliwa na TRA na NBAA ili waweze kupigiwa HESABU ya KODI Kikamilifu.

Baada ya kuchangia Mada hii kwa ujumla wake sasa nitoe Maoni ya Ujumla kuhusu Mfumo wetu wa KIKODI na namna ambavyo unaweza kurekebishwa:

  1. Swala la kwanza ni Viwango vyetu vya kodi,Kiwango cha Kodi ya Mapato kwa Tanzania ni 30% hiki ni kiwango kikubwa sana kwa aina ya uchumi tulio nao.Nasema nikiwango kikubwa kwa sababu kiwango hiki hakihamasishi ukuaji wa Biashara na kinaathiri sana gharam za uendeshaji hasa ukizingatia kwamba kuna gharama nyingi ambazo ni za kikodi ambazo kwa sasa zinaitwa TOZO ambazo zimeingizwa katika mfumo wetu wa Biashara.Ukitazama kwa ukaribu utaona kwamba Serikali ambayo haitoi vihamasishi vyovyote kwa wafanyabiashara inawatoza wafanyabiashara kodi ya 30% kisha kuna kuwa na gharama nyingine nyingi ambazo mfanyabiashara analipa kwa serikali hiyo hiyo.Ukija ukitazama unakuta Majukumu ya Compliance tu yanamgharimu mfanyabiashara zaidi ya 5% au zaidi ya mapato yake.Kitu serikali inaweza fanya ni Kupunguza Kiwango Cha Kodi ya Mapato kutoka 30% mpaka 15 au 20% na kisha kufanya VAT iwe Single DIGIT.Baada ya Hapo Biashara zote zilazimike kuwa na EFD regardless of SIZE na LOCATION na ihamasishe Digital Payment kwa kuondokana na TOZO za moja kwa moja katika Miamala ya Malipo kwa njia mtandao na zibaki standard charges.
  2. Swala la Pili ni Mifumo;Serikali iondokana kabisa na Suala la Mfanyakazi wa TRA kumfanyia Mjasiriamali Makadirio ya KODI.Kama kuna viwango elekezi viwekwe kwenye Mfumo na Kila Mtu awe na uwezo wa kutazama masuala yake ya kikodi na kuyasimamia Peke yake.TRA wafanye Monitoring ya Mifumo na iwapo kuna dalili z ukwepaji basi hapo ndipo waingilie kati.Unaporuhusu watu kukutana na kuanza kuneogotiate ndipo mazingira ya Rushwa yanapokuwepo.
All in all niwapongeze TRA kwa MFumo wao mpya ingawa bado una changamoto na unahitaji maboresho.Wajitahidi sana kuufanya huu mfumo uwe Intelligent System Yaani uwe na uwezo wa kujifunza kulingana na Data za walipa kodi wengine,location za walipa kodi wengine na taarifa nyingine za mlipa kodi.Teknoljia zipo na ninaamini kabisa kwamba wanaweza wakiwa na nia ya dhati.Yako Mengi sana ambayo ninayaona ila kwa leo tuanze na hayo na wengine nao wajdili
Umeupiga mwingi sana.
 
Mleta mada assume wewe ni mfanyabiashara umekutwa na kosa penalty yake ni 4.5 mill mimi afisa tra nikakwambia bwana kukusaidia nipe 500K kesi iishe au niishushe mpaka 1.5mill utakuwa tayari kuniripot nakula rushwa then uende ukailipe hiyo 4.5 mill?

Jibu utakalolipata ndiyo litakupa mwanga kwamba kwanini huwa haitokei mtu anayeitwa mfanyabiashara kum-snitch kijana wa kaizar kwa sababu wanaongea lugha moja
 
Viwango vya kodi ni vikubwa kama alivoshauri Masokotz , lakini Kwa wasafirishaji wa mizigo either kutoka ndani ya nchi kwenda nje au kutoka nje kuja ndani ya nchi iwe wazi, Kwa mfano container ya 20ft au 40ft ya vitenge ijulikane italipiwa bei ganiena labda container ya jinzi au shati au viatu italipiwa kiasi kadhaa, uwazi ukiwepo itaongeza morali ya ukusanyaji mapato
 
Ndugu Masokotz umeupiga mwingi sana. Ninadhani serikali na wananchi wapeane elimu ya kutosha kuhusu kodi ili watu wahamasike kulipa. Bado jamii inaona TRA kama adui yao kiasi kwamba kukwepa kodi ndo inaonekana ujanja badala ya kulipa. Kama alivyosema Ndugu Masokotz ninaunga mkono hoja kwamba kusiwepo na utitiri wa kodi ambazo zingine zinaitwa tozo. Pia kwa mtazamo wa kisiasa ni kuwa kwenye katiba mpya itamkwe kuwa Mbunge angalau awe na degree ili isaidie kutopitisha sheria za hovyo kwenye kodi. TRA ni watekelezaji tu wa sheria kwahiyo hata tukiwalaumu sana haina maana wakati watunga sheria wapo wanaota tu vitambi.
 
Kwa ufupi sana Serikali ndio no.1 moja kwa ukwepaji kodi na ndio inawafundisha wananchi wake wakwepe kodi, mfano: Serikali inatangaza tenda ya kununua vitabu kati ya watakao omba kuna mwenye VAT na asiye na VAT ili mwenye VAT apate faida ni lazima aongeze 18% kwenye total value na yule asiye na VAT hataongeza hiyo %18, siku ya ufunguzi huyu aliyeongeza %18 ataonekana ana bei kubwa ukilinganisha na yule asiye na VAT, mwisho yule asiye na VAT atatangazwa mshindi, je hapo serikali inaona ni sawa? Kwanini kila mfanyabiashara asilipe VAT?
 
Mleta mada assume wewe ni mfanyabiashara umekutwa na kosa penalty yake ni 4.5 mill mimi afisa tra nikakwambia bwana kukusaidia nipe 500K kesi iishe au niishushe mpaka 1.5mill utakuwa tayari kuniripot nakula rushwa?
Kwani Afisa wa TRA anapokukuta na KOSA ni kama TRAFIKI Barabarani?Afisa wa Kodi sio kama TRAFIKI Barabarani kwamba mnamalizana.Afisa wa TRA anapokuja katika Ofisi yako lazima azingatie Utaratibu wa Kisheria.Kama ni ukaguzi lazima uzingatie Sheria,Kama wewe ni mtuhumiwa wa Ukwepaji wa kodi lazima kuwe na Utaratibu wa Kisheria wa Kusimamia Sheria za Kodi.Mfanya Biashara ambaye anaona ni sawa Kumpa Afisa wa TRA rushwa ili asilipe au alipe Kodi ndogo basi hana elimu ya KODI na Hatakuwa ameokoa kitu chochote kile
 
Kingine watoe muda wa kipindi cha miezi mitatu Kwa biashara mpya, hii maana yake itaondoa ukiritimba wa migogoro ya kikodi Kwa wahusika wote, haiwezekani biashara inaanza leo na leo hiyohiyo ukadirie kodi hapana hapa unaandaa mazingira ya ukwepaji na ukumbuke biashara ina majira yaani high season na low season, hivo mamlaka iwakuze wafanyabishara wawe wakubwa huku wakiwapa elimu ili waone fahari kulipa kodi,
 
Kuna maeneo mengi ya kukusanya mapato ambayo mamlaka hazijayajua, juzi juzi Rais samia anatoa mfano wa kiongozi mkubwa kufanya magendo ya karafuu kupeleka mombasa, hiyo ni mfano mdogo tu magendo hufanywa na viongozi wakubwa Kwa mfano mtu anashiriana na watu wake mzigo wa vitenge ukifika bandarini haulipiwi kabisa au unatozwa kidogo huyu huyu akapambane na waliolipa kodi halali hapo ndio asie na mbeleko anaenda kutafuta wabia nchi za jirani anaagiza mizigo kama transit atakovoirudisha anajua yeye na kama atashusha njiani atajua pia hapo anakua anajitetea maana hana godfather,
 
Haya wafanyabiashara pia hukutana penalties sababu ya mifumo yetu ya ulipaji Kwa mfano mtu keshafika TRA awamu ya january hadi march kwenye makadirio alilipa umemkadiria Kwa kiwango atalipa kila miezi miwili au mitatu atalipa kias fulani basi ile control namba Kwa mwaka husika atumie hiyo hiyo kama itawezekana ili kuepuka safari za mara Kwa mara, au mfano kila ukifika muda wa kulipa atumiwe meseji ya control namba yeye popote alipo hata Kwa simu yake alipe ili kuepuka foleni kila wakati na sijui hua wanadhani mtu akifungua biashara lindi basi anaishi lindi tu hadi anakufa, kama wanaweza kutuma meseji za kuwatakia heri ya eid na pasaka na mwaka mpya Kwa nini control namba wasitume Kwa meseji?
 
Nimejibu kama Mlipa kodi bwashee

Wengi hawajui Kwamba kutoza kodi ni Art yaani Sanaa fulani lakini kulipa Kodi ni Sayansi kwa Sababu unaifeel kibiology katika mfumo wako wa hisia

Walipakodi huwa tunahitaji management fulani Hivi kimwili na Kiroho 😄😄
Sawa Ndugu Mlipa Kodi.Hvi Wabunge mnalipaga Kodi kweli?
 
Haya wafanyabiashara pia hukutana penalties sababu ya mifumo yetu ya ulipaji Kwa mfano mtu keshafika TRA awamu ya january hadi march kwenye makadirio alilipa umemkadiria Kwa kiwango atalipa kila miezi miwili au mitatu atalipa kias fulani basi ile control namba Kwa mwaka husika atumie hiyo hiyo kama itawezekana ili kuepuka safari za mara Kwa mara, au mfano kila ukifika muda wa kulipa atumiwe meseji ya control namba yeye popote alipo hata Kwa simu yake alipe ili kuepuka foleni kila wakati na sijui hua wanadhani mtu akifungua biashara lindi basi anaishi lindi tu hadi anakufa, kama wanaweza kutuma meseji za kuwatakia heri ya eid na pasaka na mwaka mpya Kwa nini control namba wasitume Kwa meseji?
TRA Tanzania Hili liko Ndani ya Uwezo wa TRA kwa sasa.
 
Mkuu kuna Point fulani Unayo ila sasa Jinsi ulivoiweka Hata TRA hawataelewa.

Kwanza nianze na Utaratibu wa Makadirio,

Utaratibu wa makadirio una utaratibu wake na Kanuni zake.Kuna threshold za Kiwango cha Mapato na kiasi cha kodi unayopaswa kulipa.Sasa kwenye kuamua kiwango cha mapato TRA wanatumia vyanzo mbalimbali vya Taarifa zikiwamo Taarifa zinaotolewa na walipa kodi wenyewe,aina ya biashara,eneo la biashara na wakati mwingine hali ya kiuchumi.Sasa katika kufanya hivyo unaona kabisa kwamba Upo Utaratibu mzuri na Rahisi wa kuweza kusimamia Hiyo kodi ya Makadirio.

Sasa Tatizo ni nn?
Kwanza Tatizo ni Watanzania kutokuelewa kuhusu elimu ya kodi na sheria za kodi pamoja na haki zao kama walipa kodi na wajibu wao kama walipa kodi.

Suluhisho:
Suala kama hilo haliwezi kurekebishwa kwa sheria kali wali amri kali.Ni suala ambalo litachukua muda likihitaji wananchi kuendelea kujifunza na TRA nao kuendelea kujifunza na kuboresha Huduma zao.

Swala la Pili ni kuhusu hiyo kodi ya 18% ambayo inaitwa VAT,Kwanza tuelewe kwamba kodi ya VAT au kama inavyoitwa Sales TAX lengo lake kubwa ni kupanua wigo wa ulipaji wa kodi na kurahisisha ukusanyaji wa kodi.Kodi ya VAT inatozwa kwa assumtion kwamba yule mlaji wa Mwisho Ndio atakuwa mlipaji.Sasa Tafsiri ya Mlaji wa mwisho ni nani ndipo ambapo watu inabidi waelewe.Kwa mfano,Ukienda Sokoni ukanunua Mboga au uakaenda dukani kwa mangi ukanunua Bidhaa ambayo inatozwa VAT(Zinagatia kwamba sio kila bidhaa inatozwa VAT) basi ufahamu kwamba Wewe ambaye unaenda kutumia bidhaa hiyo Ndio Mlipaji.Hata kama utapewa Risit ambayo haina VAT bado wewe ni mlaji wa Mwisho.Yule Muuzaji wa Duka kwa sababu Yeye hajasajiliwa na VAT naye ni Mlaji wa Mwisho katika Mtazamo wa Kikodi mpaka atakapokuwa amesajiliwa kukusanya VAT.Kwa mtu ambaye amesajiliwa VAT yeye ataidai Mamlaka ya Mapato Ile Tofauti ya Kodi kati ya Makusanyo yake kutokana na Mauzo na Manunuzi ambapo iwapo Manunuzi yatazidi ila iwapo mauzo ndio yatazidi basi Ile Tofauti ya VAt atapaswa kulipa TRA.

Kwa wale ambao wanatuza kumbukumbu za Hesabu wao huwa wanao wajibu wa kuandaa HESABU za MWAKA kwa kupita Wahasibu na Wakaguzi pamoja na Wataalamu wa KODI ambao wamesajiliwa na TRA na NBAA ili waweze kupigiwa HESABU ya KODI Kikamilifu.

Baada ya kuchangia Mada hii kwa ujumla wake sasa nitoe Maoni ya Ujumla kuhusu Mfumo wetu wa KIKODI na namna ambavyo unaweza kurekebishwa:

  1. Swala la kwanza ni Viwango vyetu vya kodi,Kiwango cha Kodi ya Mapato kwa Tanzania ni 30% hiki ni kiwango kikubwa sana kwa aina ya uchumi tulio nao.Nasema nikiwango kikubwa kwa sababu kiwango hiki hakihamasishi ukuaji wa Biashara na kinaathiri sana gharam za uendeshaji hasa ukizingatia kwamba kuna gharama nyingi ambazo ni za kikodi ambazo kwa sasa zinaitwa TOZO ambazo zimeingizwa katika mfumo wetu wa Biashara.Ukitazama kwa ukaribu utaona kwamba Serikali ambayo haitoi vihamasishi vyovyote kwa wafanyabiashara inawatoza wafanyabiashara kodi ya 30% kisha kuna kuwa na gharama nyingine nyingi ambazo mfanyabiashara analipa kwa serikali hiyo hiyo.Ukija ukitazama unakuta Majukumu ya Compliance tu yanamgharimu mfanyabiashara zaidi ya 5% au zaidi ya mapato yake.Kitu serikali inaweza fanya ni Kupunguza Kiwango Cha Kodi ya Mapato kutoka 30% mpaka 15 au 20% na kisha kufanya VAT iwe Single DIGIT.Baada ya Hapo Biashara zote zilazimike kuwa na EFD regardless of SIZE na LOCATION na ihamasishe Digital Payment kwa kuondokana na TOZO za moja kwa moja katika Miamala ya Malipo kwa njia mtandao na zibaki standard charges.
  2. Swala la Pili ni Mifumo;Serikali iondokana kabisa na Suala la Mfanyakazi wa TRA kumfanyia Mjasiriamali Makadirio ya KODI.Kama kuna viwango elekezi viwekwe kwenye Mfumo na Kila Mtu awe na uwezo wa kutazama masuala yake ya kikodi na kuyasimamia Peke yake.TRA wafanye Monitoring ya Mifumo na iwapo kuna dalili z ukwepaji basi hapo ndipo waingilie kati.Unaporuhusu watu kukutana na kuanza kuneogotiate ndipo mazingira ya Rushwa yanapokuwepo.
All in all niwapongeze TRA kwa MFumo wao mpya ingawa bado una changamoto na unahitaji maboresho.Wajitahidi sana kuufanya huu mfumo uwe Intelligent System Yaani uwe na uwezo wa kujifunza kulingana na Data za walipa kodi wengine,location za walipa kodi wengine na taarifa nyingine za mlipa kodi.Teknoljia zipo na ninaamini kabisa kwamba wanaweza wakiwa na nia ya dhati.Yako Mengi sana ambayo ninayaona ila kwa leo tuanze na hayo na wengine nao wajdili
Umeeleza vizuri sana, lakin ata wewe bado hujafahamu aina za kodi ya mapato na rate zake. You should understand that administration ya kodi sio rahisi kabisa kidunia. Hakuna nchi isiyokuwa na migogoro ya kodi duniani tunatofautiana tu ktk Mamlaka za kikodi na usimamizi wake. Mfanyabiashara or Income earner anafanya kila hila kuficha mapato yake na Mamlaka au serikali inafanya kila hila kufichua mapato yake katika namna za kisheria mifumo ya kodi. 30% rate hiyo ni income tax rate inayotozwa kwa makampuni kwenye faida na mfanyabiashara binafsi anatozwa 3.5% tu kwa mapato yake ya mwaka mzima. Bado huyo hyo mfanyabiashara anayo room ya kujikadiria kodi yake na kuwasilisha TRA(Provisional assessment) na akawasilisha final return. TRA wapo wazi sana tatizo ni compliance ya kodi tu Tanzania ni ndogo. Siasa nayo ina athari kubwa sana kwenye eneo la kodi
 
Back
Top Bottom