SweetMillah
New Member
- Aug 7, 2022
- 4
- 11
Ulemavu ni Hali ya upungufu wa kazi katika kiungo kimoja wapo katika mwili wa mwanadam au mnyama kiungo hicho chaweza kuwa mkono, mguu macho nk kupelekea uhitaji wa vifaa maalumu ili kujishirikisha katika shughuli za kijamii na kiuchumi.
Binafsi nimezaliwa nikiwa na uwezo wa kusikia na nilipokuwa shule ya msingi nilikuwa nikifanya vyema nikafanikiwa kujiunga kidato Cha kwanza,maendeleo yangu yalikuwa mazuri tu Hadi kidato Cha pili ambapo ghafla nilianza kujihisi sisikii vizuri nilipoitwa sikusikia vizuri mda mwingine nilitukanwa au kupigwa na walimu kwasabab nilishindwa kujieleza kuwa sisikii vizuri , pengine kwasabab ya woga na aibu watanchukuliaje nikisema sisikii vizuri ilihali nilikuwa mzima?
Kwakua ilikua shule ya kutwa nyumbani Nako walianza kinigundua walipoita mara mbili mara tatu pasina wasikia, mda mwingine walinituma hiki Mimi naleta kingine. Mara nyingi nilikuwa naumia pale waliposema hivi wewe husikii? Niliogopa kuwajibu mda mwingi nilibaki kimya nikijitafajari, nilianza kuyasahau masomo nikaanza kuacha kwenda shule kwasabab nilijiona tifauti na wenzangu nilitamani kupelekwa shule za viziwi tuu lakini baba yangu alilikataa hilo. Hatimaye nilipelekwa hospital za kata na za ma specialist mfano Bugando, Hindu, Regency, Ekenywa nk lakini majibu yalisikitisha mara nyingi walikuta masikio ni mazima na hayana tatizo isipokuwa mishipa ya fahamu ndiyo shida
Nilipewa dawa aina ya Neurton ya kumeza Hadi tatizo litapokoma na kifaa maalumu kwa ajili ya kusikia lakini havikuweza saidia. Hatimaye nilirudi shule nikiwa na furaha lakini kifaa hakikunisaidia chochote bado nilishindwa kutafsiri maneno sikuona umuhimu niliacha kukivaa hatimaye nilijisomea mwenyewe, nilijifundisha pia kupitia kusoma huku nikisaidiwa na walimu kwa ukaribu hadi kidato cha nne, kilichoniumiza ni wanafunzi kutofahamu lugha za alama,
• Binafsi nilikuwa sizijui na ningezijuaje ilihali shule nilizotoka hakuna mafunzo hayo?
• Wanafunzi walionizunguka hawakuwa na ujuzi wa lugha za alama hivyo ilinikwamishia mawasiliano shuleni na nilianza kuwa mkimya Hali iliyoniumiza mda mwingi sana.
• Shule maalumu kwa viziwi zilikuwa mbali na maeneo nilipo kutokana na mfuko wa mzazi ikawa ni vigumu.
Niliendelea na masomo sikukata tamaa nilijitahidi Sana hata kuwazidi wenzangu kwani nilikuwa miongoni mwa tatu Bora na hatimaye tano Bora nilijitahidi kusoma na kumuonba Mungu nisishuke hapo na kweli sikushuka hapo. Japo maneno yalikuwa mengi shuleni wengine walithubutu kusema siwezi zidiwa na mtu asiyesikia lakini haikuniumiza kwasababu niliijenga akili yang kuwa inaaweza na mara nyingi sikuwalaumu " Bali nili ilaumu serikali kwa kutotoa Elimu juu ya walemavu kwa wanafunzi wasio na ulemavu ili na wao waelewe kuwa mlemavu anaweza Kama mtu ambaye asiye na ulemavu na kwa kutowafunza upendo mashuleni juu ya walemavu ilinipelekea kutamani uwepo wa somo la ulemavu Kama ilivyo Katika kupambana na rushwa"
Nilifaulu kidato cha nne kwa div 2.18 (HGL) sikuyafurahia matokeo kwasababu nilitaka sayansi ili nije kuwa Daktari wa masikio siku moja japo haikuwa hivyo nilikubali matokeo na nilimshukuru Mungu. Hatimaye nilijiunga kidato cha tano changamoto zilikuwa ni zilezile lakini nilipambana nazo, kutokana na uzoefu wangu nilipokuwa wazazi kunitia moyo nilipokuwa high school sikuwa na wazaz bali mimi kama mimi. Kejeli kwa wanafunzi (bullying) zilikuwa nyingi muda mwingine nilirudi nyumbani kwa kisingizio cha kuumwa japo nipate wa kunitia moyo ili nikaiendeleze safari yangu ya elimu.
Nilipokuwa shuleni sukutaka kukaa tu muda wenzangu waliokuwa wakipiga story kwakuwa muda mwingine sikuweza kujumuika nao hiyo ilitokana na kuona sisikii naenda kufanya nini muda mwingine hata nilipowasikia kwa shida na kuchangia mada hakuna aliyenijali. Hivyo nilichukua daftari na kutumia muda huo kuandika hadithi wengi walivutiwa na mwandiko wangu walianza kuisoma hadithi iliyomhusu (Binti yatima aliyekatishwa masomo kisa mapenzi na hatma yake). Muda mwingine waligombania daftari kwani mara nyingi wahusika nilitumia majina yao wenyewe walizidi kutamani na walianza kujifunza sikuona anayeninyanyapaa tena muda mwingine walijikusanya nikaanza kuwafundisha lugha za alama na taratibu walianza kuelewa ikanirahisishia mawasiliano nao.
Nilijiona mwenye nguvu na mtu mpya hii ilinijengea ujasiri na hatimaye nilianza kuwa mchangamfu na si mkimya Tena. Walimu walifurahishwa na Mimi na walisoma hadithi nilizoandika walinambia nilikuwa wapi siku zote walitaka kuniunga na FEMA lakini muda ulikuwa wa mwisho kumaliza kidato Cha SITA na hatimaye nilimaliza hivi leo niko chuo mwaka wa pili
Ninapokua field napata vikwazo na kukosa hamasa kwani wafanyakazi wengi hawana ufahamu wa lugha ya alama kwa viziwi na vipofu hivyo hunikwamishia mawasiliano na motisha ya kujifunza.
Naishauri serikali kutoa Elimu ya lugha za alama kwa shule zote za wenye ulemavu na wasio na ulemavu hii itarahisha mawasiliano, kwani hata mlemavu aendapo dukani atakuwa na uhakika wa maelewano kwani ni elimu hutolewa yangu daraja la chini Kama ilivyo kusoma na kuandika.
Binafsi nimezaliwa nikiwa na uwezo wa kusikia na nilipokuwa shule ya msingi nilikuwa nikifanya vyema nikafanikiwa kujiunga kidato Cha kwanza,maendeleo yangu yalikuwa mazuri tu Hadi kidato Cha pili ambapo ghafla nilianza kujihisi sisikii vizuri nilipoitwa sikusikia vizuri mda mwingine nilitukanwa au kupigwa na walimu kwasabab nilishindwa kujieleza kuwa sisikii vizuri , pengine kwasabab ya woga na aibu watanchukuliaje nikisema sisikii vizuri ilihali nilikuwa mzima?
Kwakua ilikua shule ya kutwa nyumbani Nako walianza kinigundua walipoita mara mbili mara tatu pasina wasikia, mda mwingine walinituma hiki Mimi naleta kingine. Mara nyingi nilikuwa naumia pale waliposema hivi wewe husikii? Niliogopa kuwajibu mda mwingi nilibaki kimya nikijitafajari, nilianza kuyasahau masomo nikaanza kuacha kwenda shule kwasabab nilijiona tifauti na wenzangu nilitamani kupelekwa shule za viziwi tuu lakini baba yangu alilikataa hilo. Hatimaye nilipelekwa hospital za kata na za ma specialist mfano Bugando, Hindu, Regency, Ekenywa nk lakini majibu yalisikitisha mara nyingi walikuta masikio ni mazima na hayana tatizo isipokuwa mishipa ya fahamu ndiyo shida
Nilipewa dawa aina ya Neurton ya kumeza Hadi tatizo litapokoma na kifaa maalumu kwa ajili ya kusikia lakini havikuweza saidia. Hatimaye nilirudi shule nikiwa na furaha lakini kifaa hakikunisaidia chochote bado nilishindwa kutafsiri maneno sikuona umuhimu niliacha kukivaa hatimaye nilijisomea mwenyewe, nilijifundisha pia kupitia kusoma huku nikisaidiwa na walimu kwa ukaribu hadi kidato cha nne, kilichoniumiza ni wanafunzi kutofahamu lugha za alama,
• Binafsi nilikuwa sizijui na ningezijuaje ilihali shule nilizotoka hakuna mafunzo hayo?
• Wanafunzi walionizunguka hawakuwa na ujuzi wa lugha za alama hivyo ilinikwamishia mawasiliano shuleni na nilianza kuwa mkimya Hali iliyoniumiza mda mwingi sana.
• Shule maalumu kwa viziwi zilikuwa mbali na maeneo nilipo kutokana na mfuko wa mzazi ikawa ni vigumu.
Niliendelea na masomo sikukata tamaa nilijitahidi Sana hata kuwazidi wenzangu kwani nilikuwa miongoni mwa tatu Bora na hatimaye tano Bora nilijitahidi kusoma na kumuonba Mungu nisishuke hapo na kweli sikushuka hapo. Japo maneno yalikuwa mengi shuleni wengine walithubutu kusema siwezi zidiwa na mtu asiyesikia lakini haikuniumiza kwasababu niliijenga akili yang kuwa inaaweza na mara nyingi sikuwalaumu " Bali nili ilaumu serikali kwa kutotoa Elimu juu ya walemavu kwa wanafunzi wasio na ulemavu ili na wao waelewe kuwa mlemavu anaweza Kama mtu ambaye asiye na ulemavu na kwa kutowafunza upendo mashuleni juu ya walemavu ilinipelekea kutamani uwepo wa somo la ulemavu Kama ilivyo Katika kupambana na rushwa"
Nilifaulu kidato cha nne kwa div 2.18 (HGL) sikuyafurahia matokeo kwasababu nilitaka sayansi ili nije kuwa Daktari wa masikio siku moja japo haikuwa hivyo nilikubali matokeo na nilimshukuru Mungu. Hatimaye nilijiunga kidato cha tano changamoto zilikuwa ni zilezile lakini nilipambana nazo, kutokana na uzoefu wangu nilipokuwa wazazi kunitia moyo nilipokuwa high school sikuwa na wazaz bali mimi kama mimi. Kejeli kwa wanafunzi (bullying) zilikuwa nyingi muda mwingine nilirudi nyumbani kwa kisingizio cha kuumwa japo nipate wa kunitia moyo ili nikaiendeleze safari yangu ya elimu.
Nilipokuwa shuleni sukutaka kukaa tu muda wenzangu waliokuwa wakipiga story kwakuwa muda mwingine sikuweza kujumuika nao hiyo ilitokana na kuona sisikii naenda kufanya nini muda mwingine hata nilipowasikia kwa shida na kuchangia mada hakuna aliyenijali. Hivyo nilichukua daftari na kutumia muda huo kuandika hadithi wengi walivutiwa na mwandiko wangu walianza kuisoma hadithi iliyomhusu (Binti yatima aliyekatishwa masomo kisa mapenzi na hatma yake). Muda mwingine waligombania daftari kwani mara nyingi wahusika nilitumia majina yao wenyewe walizidi kutamani na walianza kujifunza sikuona anayeninyanyapaa tena muda mwingine walijikusanya nikaanza kuwafundisha lugha za alama na taratibu walianza kuelewa ikanirahisishia mawasiliano nao.
Nilijiona mwenye nguvu na mtu mpya hii ilinijengea ujasiri na hatimaye nilianza kuwa mchangamfu na si mkimya Tena. Walimu walifurahishwa na Mimi na walisoma hadithi nilizoandika walinambia nilikuwa wapi siku zote walitaka kuniunga na FEMA lakini muda ulikuwa wa mwisho kumaliza kidato Cha SITA na hatimaye nilimaliza hivi leo niko chuo mwaka wa pili
Ninapokua field napata vikwazo na kukosa hamasa kwani wafanyakazi wengi hawana ufahamu wa lugha ya alama kwa viziwi na vipofu hivyo hunikwamishia mawasiliano na motisha ya kujifunza.
Naishauri serikali kutoa Elimu ya lugha za alama kwa shule zote za wenye ulemavu na wasio na ulemavu hii itarahisha mawasiliano, kwani hata mlemavu aendapo dukani atakuwa na uhakika wa maelewano kwani ni elimu hutolewa yangu daraja la chini Kama ilivyo kusoma na kuandika.