LIVE Updates za Beijing Auto Show 2024 (25 April - 4 May)

China wanajitahidi sana kukimbiza na EV cars.
Checki mfano hii graph:
Picture 2.png
 
Mercedes Benz G Class ya Umeme.
6629ad82a31082fc2b6cc8c1.jpeg

If you can't beat them.. G Wagon ya umeme iyooo ikiwa na range ya kilometa 570 kwa full charge moja.

Hii ni series ya tatu ya Magari ya umeme kutoka Mercedes Benz baada ya EQ series (EQS, EQB, EQCE, EQA etc) na Mercedes-AMG GT 63 S E (ina E Performance/Hybrid).
 
Jaecoo J7 kutoka kwa Chery
Jaecoo ni sub brand ya Chery (kama Lexus na Toyota) ambayo specifically ni kwa magari nje ya China. Sasa wametoa Hybrid moja kali sana, J7.
Jaecoo-J7.jpg
1-71.jpg

Hii SUV, itakayo anzwa kuuzwa huu mwaka itakua approximately $50,000/= tu. Hii ina engine 1.6L Turbo na battery. Ina produce horsepower 194 na ukiwek EV peke yake ina range ya 100km.

image-124.png


Ndani kuna screen ya inch 10 Instrument Panel (screen ya dereva ya kuonesha speed, gear, na info nyingine) na kuna screen ya inch 15 pale katikati.

Pia gari ina level 2 ADAS yenye adaptive cruise control, automatic braking system, lane departure warning, blind spot detection.
 
BYD, XIAOMI au kampuni yoyote ya magari ije pia iwekeze Tanzania aisee. Dah Xiaomi mbaya sana kwenye EV yaani najua kabisa Elon Musk kila akilala lazima aote gari za Xiaomi zikiwa zina mkimbiza 😂
Huenda watengenezaji wa Chinese trucks & buses wakatangulia kufikiria kuwekeza Afrika Mashariki na kati maana kwa sasa wameliteka soko
 
Marekani wameshikwa pabaya na China

Ndani ya mwezi huu Marekani imewatuma wajumbe 2 waende China ziara tofauti

Janet Yellen (US Treasury Secretary)
Antony Blinken (US Secretary of State)

Wote katika ajenda zao mojawapo ya ajenda yao wanailalamikia China kuwa inachofanya sasa ni industrial overcapacity ikitia ndani kwenye utengenezaji wa EV

Wamesahau kuwa China imewekeza sana kwenye industrial robot na autonomous AI-based driving system
 
Volkswagen tena.
Wapenzi wa Volkswagen wametuletea Volkswagen ID.Concept ambayo ni Smart Car.

View attachment 2975180

Hii ni SUV flani, ambayo Volkswagen wamesema ina latest and most advanced Level 4 Automated driving.

PS: Automated Driving zina level kadhaa kuanzia level 1 hadi level 5. Hii Level 1 ni simple and lighter driving assistance mfano Cruise Control, Lane Keeping Assistant etc wakati Level 4 ni FSD (Full Self Driving) kwamba gari itafanya kila kitu kuanzia acceleration, braking, cornering, kusimama kwenye traffic lights, kupark, kusimama zebra, etc as long umeshaweka destination kwamb naenda Mbagala Rangi Tatu. Tuendelee na gari letu..

Hapa dereva ukiacha gari ijiendeshe, wewe na abiria wako wa mbele mnaweza geuka kabisa 180 degrees kupiga story na abiria wa nyuma. Sio kigeuza shingo, kugeuza seat kabisa.

View attachment 2975191


Ukiwa unaendesha hii chuma afu uka engage "Center Pilot" hapa AI inatake over inaanza kuendesha yenyewe chuma. Kwanza mkwara unaanza steering wheel ambayo inashape yetu pendwa ila mbaya Yoke style inazama na kubakisha dashboard plain, kama kwenye Sci-fi movies.

View attachment 2975183

Pia vioo vyote, cha mbele na vya pembeni, vina display information mbalimbali ambazo utaamua watu wa nje wazione au muzione nyie wa ndani tu.

Mfano, unaweza ukawa uko ndani unaendesha chuma afu unapita sehemu kuna mazingira mabaya, ukaamua kuweka display vioo vya pembeni vikawa vinaonesha wallpaper beach au kitu garden, ili passengers wafurahi.

Kioo cha mbele kina HUD augmented reality down to earth projection, nadhani hii tumeona kwenye Mercedes Benz EQS yaan HUD hii unakua unaona kabisa as if vitu vimewekwa kwa chini. Nashindwa kuelezea ila ngoja angalia hii picha kama itakusaidia.

View attachment 2975186

Na mwisho kuna hygiene mode, ambayo uta engage mfano umetoka safari afu ulikua na familia. Gari chafu kwa ndani. Basi mkishuka, uka enable gari itahakikisha ndani hakuna mtu afu itatoa UV light na antibacteria filters zitasafisha hewa ya ndani na kuna vacuum cleaner anaitwa Lupo ataanza kusafisha ndani kuondoa takataka ndogo ndogo.
View attachment 2975189

Ilikua moja ya presentation nzuri tungeweka link hapa ya video ila haina maana vitajaa vilink sana.
Sipati picha hili gari likitumika huku bongo na hawa bodaboda itakuaje!!!
 
Back
Top Bottom