airGrid
JF-Expert Member
- Jul 9, 2015
- 628
- 396
Makonda ndo mtetezi no. 1 wa awamu ya tano, aulizwe anajua zilipo.Tunakumbuka miaka mitano iliyopita mfalme wa Morocco alitoa pesa ylza kujenga msikitini na pia uwanja wa mpira pale Dodoma. Zikaandaliwa ramani za uwanja huo na Rais Magufuli akapelekewa ramani. Serikali ikatuambia uwanja huo utakuwa mkubwa kuliko ule wa Mkapa pale Dar kwani utabeba watu elfu 85.
Miaka kadhaa imepita sasa na kuna ukimya mwingi wa serikali kuhusu jambo hili. Kabla ya kuanza ujenzi wa uwanja wa mpira Arusha tunataka kujua kwanza pesa za mfalme wa Morocco kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa Dodoma ziko wapi? Ni vema serikali ikaja na majibu yanayoeleweka kwenye hili jambo.
Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
Pia soma
- Ujenzi wa Uwanja wa Mpira Dodoma kwa msaada wa Mfalme wa Morocco umeishia wapi?