JZHOELO
Senior Member
- Sep 20, 2011
- 196
- 352
Imekuwa ni shida sana kwa watanzania wengi kununua bidhaaa katika masoko haya ya mtandaoni kwani mengi huwa hayakupi fursa ya kutumiwa mzigo wako moja kwa moja Tanzania. Baadhi ya thread zilianzishwa na zimeelezea mengi sana kuhusiana na manunuzi haya ya mtandaoni, ila tulipata ufumbuzi mdogo.
Nimejaribu kupitia pitia forums nyingi nichanganue namna mbadala ya kupata mizigo bila ya kutumia gharama nyingi. hii ni kwa kutumia FOWARDING COMPANIES ambazo kazi yake ni;
1: Kukupatia anuani ya Marekani (au popote iliopo ila nashauri marekani au uingereza UK) au US Shipping Address
2: Kupokea mzigo kwenye soko ulilotumia (eidha amazon,ebay au lolote lile lisilo ship Tanzania)
3: Kukutumia mzigo wewe hapo ulipo kwa wakala kama DHL,FEDEX,UPS,USPS NK baada ya kujua kazi ya fowarding company unahitaji kuwa na vigezo vifuatavyo (kwa wageni wasiofahamu/hawajapitia previous threads:
1: CREDIT CARD (KADI YA BENKI) INAYOFANYA ONLINE PURCHASES;
Hii inapatikana almost bank zote hapa Tanzania (kasoro NMB sina uhakika), ni kadi yeyote ya visa au mastercard unachotakiwa ni kwenda kwenye tawi la benki yako na kuomba fomu ya kuruhusu kadi yako ifanye malipo ya mtandaoni(online purchases) na mara nyingi huchukua maximum 24hours kuactivate.
2: KUJIUNGA NA PAYPAL
Hiii ni kampuni inayolinda malipo yako kwa kutomuonesha muuzaji details (nyaraka) za kadi yako kama number na css ambayo vitampa muuzaji access ya kuchukua pesa zako. Ila kwa paypal utalindwa na kurudishiwa pesa pale panapotokea shida au huduma mbaya.
3: KUJIUNGA NA FOWARDING COMPANY
Hii hatua ni ya wewe kwenda kwenye website (tovuti) za hizi fowarding company na kujiunga (sighnup) nazo/nayo ili zianze kukupatia huduma... nitaelezea chini zaidi kuhusu ipi ni ipi na huduma zao zikoje na faida na hasara za kila moja ili ujichagulie wewe mwenyewe binafsi
4: KUTAMBUA SOKO BORA LENYE HUDUMA NZURI(ONLINE MARKET)
Hapa tunazungumzia website za masoko kama ebay,amazon, bestbuy, apple.com, dell.com, toshiba.com nk.. masoko haya ndipo utakapo nunua bidhaa yako.
PROCESS NZIMA KUANZIA UNANUNUA MPAKA MZIGO UNAKUFIKIA IKOJE?
Hii iko hivi....
1: Ingia katika soko lako ulilolichagua au unalopendelea, hapa nasuggest kutumia sana amazon(ndilo ninaloliamini) amazon ukiingia utakuta bidhaa nyingi ila kuwa makini kuchukua zile bidhaa zilizo na alama ya prime chini...alama hiyo inamaanisha kuwa huo mzigo unauzwa, utapakiwa, na kutumwa na amazon wenyewe, so no utapeli hapo, yani u get what u wanted.
2: Nunua na kuagiza kitu kwenda kwenye address ya fowarding company ulioichagua, hivyo mzigo ulioununua utaenda moja kwa moja kwenye company yako, wao wakishaupata watakutumia e-mail uthibitishe au uchague courier wa kukutumia mzigo wako, hapo ndio utachagua either dhl,ups,fedex nk.wao watakutumia na kuchukua kiasi chao cha pesa ya huduma na kukutumia mzigo pamoja na kukupatia tracking number ya kujua mzigo wako ulipo na utaupokea vyema.
FOWARDING COMPANIES ZENYEWE:
1: MYUS.COM link- MyUS.com - #1 International Shipping, Mail and Package Forwarding Service - MyUS.com. Hii ni company niliyoitumia na nina expirience nayo ya mizigo miwili, hawa ni waaminifu wana charge pesa kidogo na huwa hawachukui muda kukutumia mzigo wako. yaani unafika leo hata ukitaka utumwe leo unatumwa, na utafika upesi sana bila ya zengwe lolote.
Ubaya wao: wanatumia sana DHL ambayo kwa mizigo mikubwa ni gharama sana kwa mtanzania wa kawaida, kiasi cha dola kumi kujiunga na huduma zao
Uzuri wao: watakutumia mzigo hata kama utakuwa hauna pesa kwenye account yako, watakujulisha ni duka lipi lina discount ya kutumia huduma zao, watakukumbusha kulipa deni lao, utapewa muda wa miezi miwili kulipa pesa yao,
2: COMGATEWAY
Link: Shop the US Online and Ship Internationally | comGateway - Hawa pia ni fowarding company nzuri sana (thanks tu Mwl.RCT), nimepitia site yao na huona wana policy nzuri sana, cha kwanza ni sales tax-free U.S. online shopping yaani punguzo la kodi ya kufanya manunuzi marekani, hii inapelekea huduma zao kuwa nafuu zaidi,pia wana ushirika na shipping courie DHL na FEDEX hivyo kufanya huduma zao kuwa rahisi zaidi.pia wanakupa habari kuhusu discount za masoko mbalimbali kama myus..
3: BORDERLINX
Link: Buy in the USA, ship to Belgium with Borderlinx - Hawa pia ni wazuri sana na hawana tofauti sana na stackry ... Wanawiana ingawa ni competitors wakubwa hivyo inakupa urahisi wa kuwatumia..Hawa pia hawana registration fee na wanakupa option tofauti tofauti za kutumiwa mzigo wako.
4: SHIPITO
Link: USA Address & Mail Forwarding Shipito.com | English - Hii pia ni kampuni kongwe ya fowarding na wao gharama zao ni nafuu sana ingawa wanapokea malalamiko mengi sana kutoka kwa wateja wao ukiangalia kwenye forums nyingi.ila kiujumla ni wazuri kwasababu malalamiko ni madogo kulinganisha na ufanisi na pia wanajua na ni wazoefu sana na kazi yao
5: STACKRY
Link: Stackry - US shopping, global shipping - Hii nayo haina tofauti na myus isipokuwa hawa wao hawana kiasi cha kulipia kujiunga nao na wao pia wanakupa option nyingi za kutumia mizigo yako na mabo yao pia ni mazuri kulinganisha na comment wanazopokea kutoka kwa wateja wao. waungwana ni hayo tu niliyo nayo, kazi kwenu ni kufanya utafiti na pia kuangalia na kuchunguza mabo kabla ya kuchukua uamuzi.
STACKRY na BORDERLINX walikuwa recommended sana na wanasifiwa mno angalia hii link -http://tech-vise.com/10-parcel-forwarding-services-for-international-shoppers/ pitia hizo websites na ujionee mwenyewe chagua moja na utazame kama wanakufaa.
HUU NI MTAZAMO WANGU BINAFSI WAKUU , Please evaluate kindly.
Nilikuwa nataka kuonyesha steps ila naona thread haitoshi maana nimeagiza mzigo na nimechukua hatua zote ili mpate kuona ila I think there are limits..
Help Mwl.RCT
Nimejaribu kupitia pitia forums nyingi nichanganue namna mbadala ya kupata mizigo bila ya kutumia gharama nyingi. hii ni kwa kutumia FOWARDING COMPANIES ambazo kazi yake ni;
1: Kukupatia anuani ya Marekani (au popote iliopo ila nashauri marekani au uingereza UK) au US Shipping Address
2: Kupokea mzigo kwenye soko ulilotumia (eidha amazon,ebay au lolote lile lisilo ship Tanzania)
3: Kukutumia mzigo wewe hapo ulipo kwa wakala kama DHL,FEDEX,UPS,USPS NK baada ya kujua kazi ya fowarding company unahitaji kuwa na vigezo vifuatavyo (kwa wageni wasiofahamu/hawajapitia previous threads:
1: CREDIT CARD (KADI YA BENKI) INAYOFANYA ONLINE PURCHASES;
Hii inapatikana almost bank zote hapa Tanzania (kasoro NMB sina uhakika), ni kadi yeyote ya visa au mastercard unachotakiwa ni kwenda kwenye tawi la benki yako na kuomba fomu ya kuruhusu kadi yako ifanye malipo ya mtandaoni(online purchases) na mara nyingi huchukua maximum 24hours kuactivate.
2: KUJIUNGA NA PAYPAL
Hiii ni kampuni inayolinda malipo yako kwa kutomuonesha muuzaji details (nyaraka) za kadi yako kama number na css ambayo vitampa muuzaji access ya kuchukua pesa zako. Ila kwa paypal utalindwa na kurudishiwa pesa pale panapotokea shida au huduma mbaya.
3: KUJIUNGA NA FOWARDING COMPANY
Hii hatua ni ya wewe kwenda kwenye website (tovuti) za hizi fowarding company na kujiunga (sighnup) nazo/nayo ili zianze kukupatia huduma... nitaelezea chini zaidi kuhusu ipi ni ipi na huduma zao zikoje na faida na hasara za kila moja ili ujichagulie wewe mwenyewe binafsi
4: KUTAMBUA SOKO BORA LENYE HUDUMA NZURI(ONLINE MARKET)
Hapa tunazungumzia website za masoko kama ebay,amazon, bestbuy, apple.com, dell.com, toshiba.com nk.. masoko haya ndipo utakapo nunua bidhaa yako.
PROCESS NZIMA KUANZIA UNANUNUA MPAKA MZIGO UNAKUFIKIA IKOJE?
Hii iko hivi....
1: Ingia katika soko lako ulilolichagua au unalopendelea, hapa nasuggest kutumia sana amazon(ndilo ninaloliamini) amazon ukiingia utakuta bidhaa nyingi ila kuwa makini kuchukua zile bidhaa zilizo na alama ya prime chini...alama hiyo inamaanisha kuwa huo mzigo unauzwa, utapakiwa, na kutumwa na amazon wenyewe, so no utapeli hapo, yani u get what u wanted.
2: Nunua na kuagiza kitu kwenda kwenye address ya fowarding company ulioichagua, hivyo mzigo ulioununua utaenda moja kwa moja kwenye company yako, wao wakishaupata watakutumia e-mail uthibitishe au uchague courier wa kukutumia mzigo wako, hapo ndio utachagua either dhl,ups,fedex nk.wao watakutumia na kuchukua kiasi chao cha pesa ya huduma na kukutumia mzigo pamoja na kukupatia tracking number ya kujua mzigo wako ulipo na utaupokea vyema.
FOWARDING COMPANIES ZENYEWE:
1: MYUS.COM link- MyUS.com - #1 International Shipping, Mail and Package Forwarding Service - MyUS.com. Hii ni company niliyoitumia na nina expirience nayo ya mizigo miwili, hawa ni waaminifu wana charge pesa kidogo na huwa hawachukui muda kukutumia mzigo wako. yaani unafika leo hata ukitaka utumwe leo unatumwa, na utafika upesi sana bila ya zengwe lolote.
Ubaya wao: wanatumia sana DHL ambayo kwa mizigo mikubwa ni gharama sana kwa mtanzania wa kawaida, kiasi cha dola kumi kujiunga na huduma zao
Uzuri wao: watakutumia mzigo hata kama utakuwa hauna pesa kwenye account yako, watakujulisha ni duka lipi lina discount ya kutumia huduma zao, watakukumbusha kulipa deni lao, utapewa muda wa miezi miwili kulipa pesa yao,
2: COMGATEWAY
Link: Shop the US Online and Ship Internationally | comGateway - Hawa pia ni fowarding company nzuri sana (thanks tu Mwl.RCT), nimepitia site yao na huona wana policy nzuri sana, cha kwanza ni sales tax-free U.S. online shopping yaani punguzo la kodi ya kufanya manunuzi marekani, hii inapelekea huduma zao kuwa nafuu zaidi,pia wana ushirika na shipping courie DHL na FEDEX hivyo kufanya huduma zao kuwa rahisi zaidi.pia wanakupa habari kuhusu discount za masoko mbalimbali kama myus..
3: BORDERLINX
Link: Buy in the USA, ship to Belgium with Borderlinx - Hawa pia ni wazuri sana na hawana tofauti sana na stackry ... Wanawiana ingawa ni competitors wakubwa hivyo inakupa urahisi wa kuwatumia..Hawa pia hawana registration fee na wanakupa option tofauti tofauti za kutumiwa mzigo wako.
4: SHIPITO
Link: USA Address & Mail Forwarding Shipito.com | English - Hii pia ni kampuni kongwe ya fowarding na wao gharama zao ni nafuu sana ingawa wanapokea malalamiko mengi sana kutoka kwa wateja wao ukiangalia kwenye forums nyingi.ila kiujumla ni wazuri kwasababu malalamiko ni madogo kulinganisha na ufanisi na pia wanajua na ni wazoefu sana na kazi yao
5: STACKRY
Link: Stackry - US shopping, global shipping - Hii nayo haina tofauti na myus isipokuwa hawa wao hawana kiasi cha kulipia kujiunga nao na wao pia wanakupa option nyingi za kutumia mizigo yako na mabo yao pia ni mazuri kulinganisha na comment wanazopokea kutoka kwa wateja wao. waungwana ni hayo tu niliyo nayo, kazi kwenu ni kufanya utafiti na pia kuangalia na kuchunguza mabo kabla ya kuchukua uamuzi.
STACKRY na BORDERLINX walikuwa recommended sana na wanasifiwa mno angalia hii link -http://tech-vise.com/10-parcel-forwarding-services-for-international-shoppers/ pitia hizo websites na ujionee mwenyewe chagua moja na utazame kama wanakufaa.
HUU NI MTAZAMO WANGU BINAFSI WAKUU , Please evaluate kindly.
Nilikuwa nataka kuonyesha steps ila naona thread haitoshi maana nimeagiza mzigo na nimechukua hatua zote ili mpate kuona ila I think there are limits..
Help Mwl.RCT
Habari Watanzania, Heri ya miaka 58 ya uhuru!
Bila kupoteza muda ngoja tuongee namna ya kununua vitu kutoka nchini China hasa kupitia platform ya Alibaba (Made in China).
Kwanza kabisa Alibaba sio platform peke yake ya kuweza kununua vitu nchini China kuna platforms kama Global sources, Made-in-China, Banggood na kadhalika.
Najaribu kufikiria unafahamu kuingia kwenye mtandao wa alibaba na unaweza kutafuta bidhaa. Sasa nataka kukuonesha namna ya kuwa mbele ya wauzaji wa kichina kwenye platform ya alibaba na vitu vya kufanya kuepuka kupoteza muda na kuumia kichwa mbeleni.
1. Bidhaa (Product)
Hakikisha muuzaji wa kichina (supplier) anafahamu nini kabisa unataka kununua hapa inamaanisha (products specifications). Hakikisha unaeleza vizuri kwa ufanisi na kiundani unataka nini hasa kwenye bidhaa yako. Ushauri Chukua dakika 10-15 kuandaa maelezo ya bidhaa, vitu kama
- Size (Ukubwa)
- Material (Materio)
- Grade (kiwango cha ubora)
- Application (In use)
- Packaging (uhifadhi wake)
- Quantity (Uwingi)
- Shipping Terms (namna ya usafiri)
- Target Price (Bei uliyopanga) HII NI MUHIMU SANA
2. Fanya Kuhakiki (Evaluation)
Mara zote unapoongea na muuzaji wa kichina ( supplier ) jaribu kuhakikisha vitu vingi tu nje na mbali ya bei ambayo watu wengi wao wanaangalia sana hii na kukosea kuto kuangalia vitu vingine. Jaribu kufirikia kwa namna hii
- Je wanajibu message zako kiusahihi na kwa wakati ) Are they responsive?
- Je wanauliza maswali yanayoendana na nini unataka katika bidhaa yako au wanakupa tu maelezo ya bidhaa zao?
- Je wanapicha za bidhaa unazozitaka wewe?
- Je mnaweza fanya mawasiliano kwa kuwapigia calls, whatsapp call au skype?
- Je wao ni watengenezaji au wao ni kampuni ya kuuza na kununu ( Manufactures Vs Trading company) Hii tutaiongelea siku zijazo
- Je wanatoa maelezo kiuwazi au kuna vitu wanaficha kuuliza?
- Nchi zipi sana wanauza hiyo products zao? Hii ni kubwa sana kwasababu hii inaweza kuonesha ni UBORA gani ambao hawa wanatengeneza.
3. Mazungumzo zaidi ya Biashara (Negotiations)
Wachina wanamsemo unasema “一分钱一分货” “Yi fen qian Yi fen huo” maana yake "unapata unacholipia"
Hii inamaanisha sio kila wakati ufanye manunuzi ya bei ya chini chini sana, mara nyingi bei za chini na ubora wa bidhaa huendana sana.
Wakati unapokua unaongea na wauzaji wengi kwa wakati mmoja unapotaka biadhaa jaribu kuweka mahusiano ya muda murefu unapoengea nao na useme " unataka biashara ya muda mrefu sio biashara ya siku moja tu" kwahiyo ni vizuri kutengeneza urafiki nao ( Hii ni mtazamo wa biashara wa kichina)
Pointi ya kubeba, hata kama una haraka vipi at least ongea na wauzaji zaidi ya 3 kujua vizuri bei ya bidhaa unayoitaka.
Pia Jaribu kuulizia Bei za bidhaa zako zikiwa na uwingi tofauti, kwasababu katika ulimwengu wa wachina uwingi ndiyo kila kitu . Unaweza uliza bei ya piece 5,000 na Bei 50,000 ukakuta gap lililopo ni kubwa sana. Katika mazunguzo zaidi, usisahau kuongelea bidhaa kuwa nyingi.
4. Hakikisha Kimtandao (Online Research & Due Diligence)
Sio kila king'aacho ni almasi, Yes ni kweli sio kila muuzaji wa kichina ni wa kweli, hakikisha unapitia maelezo yake vizuri kuogopa kuibiwa na kudanganywa mtandaoni. Yes watu wanaibiwa kila siku na kila saa kwa wauzaji wapo kwenye mitandao ya kina alibaba. Kwa teknolojia ya photoshop na kuedit vitu, hata vijana wa chuo wanaweza weka profile zao kwenye alibaba na kuuza.
5. Uliza Sample (Sample)
Baada ya kuona huyu supplier ni mzuri na unaweza kumuamini kwa kiwango kikubwa, na bei nakila kitu kimekamilika, wakati mzuri wa kuomba Sample.
Hapa hatuongelei imani tu kwa kuamini kwa macho, omba SAMPLE utumiwe uone. Sample inaweza tumia siku 5-12 kufika kwa DHL, Fedex na wengine lakini ni vyema zaidi ya kuanza kutengeneza vitu vyenye uwingi mkubwa na vikawa tofauti na unachokihitaji.
6. Pokea Sample (Evaluate Sample)
Ihakikishe sample yako kama ipo sawa na kile unachokihitaji, kama unataka kubadirisha na kufanya design yako pia ni muda sahihi wa kufanya hivyo.
7. Purchase Order (P.O)
Unaponunu kitu chochote kwenye mtandao wa alibaba au platform ya China au hata kwa mikataba ya uso wa uso hakikisha unakua na Purchase order ambayo itakulinda kwa siku za usoni. HAKIKISHA Purchase order inakua na maelezo yote unayotaka kuanzia
8. Payments
Unapofanya malipo ya aina yoyote kwanza kabisa hakuna 100% inalipwa bila kupata kitu chochote upfront.
Hakuna standard inayosema lazima ulipe 30% advance payment na baadaye ulipe 70% hii ni imekua kama kawaida lakini kuna wauzaji ( supplier) wanataka 50% advance na 50% kabla hawajatuma kwa meli.
Unaweza kuongeza zaidi na mnaweza kubadirisha mawazo namna mnavyotaka iwe.
Usikubali kutuma kwa njia ya Western Union, mara nyingi 98% ni utapeli. Kwa order ya aina yoyote hakikisha unafanya Bank Transfer.
DIRTY TRICK: HAKIKISHA MPOKEAJI WA PESA NA JINA LA USAJILI WA KAMPUNI AU KIWANDA VINAFANANA. KAMA HAIFANANI HII NI BENDERA NYEKUNDU KABISA KUNA MCHEZO UNAWEZA FANYIKA WA UTAPELI ( KUA MAKINI)
9. Usafirishaji (Shipment)
Inashangaza kwamba watu wananuna kontena na kontena, lakini hawakagui mzigo kabla haujasafirishwa kutoka China kuja Tanzania. Nimesikia case sio moja ni zaidi ya tano watu wanaagiza A wanapokea Z ( wanapokea tofauti na wanachoagiza). Hakikisha unafanya ukaguzi kabla mizigo yako haijaondoka kuanza safari kuja Tanzania.
Kuna makampuni ya ukaguzi ambayo yanafanya hii, lakini mengine yanakua na deal na viwanda kuwaandikia report kua mzigo ni sawa japokua ni mzigo mbovu. (Kuwa makini)
Baada ya kufanya ukaguzi ndiyo unaweza kuruhusu mzigo kuondoka na kuja sehemu husika.
Kiufupi hii ni namna unaweza kufanya unaponunua bidhaa kutoka China.
Kama unataka wasiliana nami unaweza nitafuta kwa number +255627637767
Karibu Pia ofisini kwangu Mikocheni, Hekima Garden kwa maelezo zaidi.
Asante.