Je, utawala wa IST unafika Kikomo?

IST bei imepanda sokoni lakini sababu kubwa ni kwamba hamna mnunuaji wa IST anaingia showroom saivi.

Wengi wanazinunua mtaani ambako IST zimenyooka, uzuri watumiaji IST wa namba D wengi huyatunza magari yao ni nadra sana kuikuta IST haifai imechoka hii inapelekea wanaotaka yamiliki IST wayapate kwa bei rahisi mtaani.

ukiwa na 10m-13m unapata IST imenyoooka kwa uzuri wa macho hata ya showroom haikuti.

Wakat showroom bila 17m kwenda mbele hulambi IST
Bei imekaza sana IST so watu wanaona bora hyo hela wajibane kdg wachukue la juu juu
 
Wabongo kwa ujuaji komesha yani ya kitaa iizidi ya showroom kwa ukali,,upo serious kweli
Kanunue yako ya show room leta picha (nnje na ndani) halafu nikuletee picha ya kitaani uone kwa vitendo kitu kinachoongelewa.

Watu gari wana zipimp,wanazitia miziki,wanazitia seat cover za maana halafu mambo yanawakalia kooni wanaweka gari sokoni

sasa wewe kalete lako la showroom uonyeshwe Ist ya mtaani iliyonyooka kupita hiyo ya showroom.
 
Wabongo kwa ujuaji komesha yani ya kitaa iizidi ya showroom kwa ukali,,upo serious kweli
maana unafikiri wenzio wanaendesha magari kama walivyoyanunua showroom.

Mtu ana nunua gari Showroom mfukoni ana 5m ya ku upgrade gari, akisha li upgrade mzigo unarudshwa sokoni kwa bei mteremkooo... Kalete lako la showroom uonyeshwe IST zilizokaa mithili ya BMW ndio utajua kuja watu wanapenda magari yao.
 
Hakuna kitu kama hicho, kitu kipya ni kipya tu hamna ubishi hapo sana sana utanujua kopo lililojazwa maspika maana naona kilichokuvuruga ni maspika Yale wanayoweka
tofaut ni ndogo sana, Tofaut ya showroom na Hii ya mtaani ni engine tu.

hiii utaikuta inasoma km 100,000 hiii ya showroom itakua na km 70,000 ni mileage tu hapo ndio tofaut.
 
Hakuna kitu kama hicho, kitu kipya ni kipya tu hamna ubishi hapo sana sana utanujua kopo lililojazwa maspika maana naona kilichokuvuruga ni maspika Yale wanayoweka
Yani mimi unipe la showroom lina mileage chache uniuzie 19m halafu huyu mileage zimepshana na ya showroom kama 20,000 tu ananiuzia kwa 13m niache nichukue la showroom? ntakua sina akili.
 
IST ipewe maua yake kwenye usajili wa No. D. Kwa utafiti usio rasmi asilimia 30 ya No.D ni magari ya IST. Lakini tangu usajili wa "E" uanze ni IST chache sana zimesajiliwa. Kwa utafiti usio rasmi Nissan Dualis inakimbiza sana kwenye usajili wa "E".

Kwa Nini watu wameacha kuchangamkia IST kama hapo awali?


Fikiri haya yafuatayo:

1. Mimi nina gari namba D ni ya 2015.
2. Maana yake namba D zina miaka 8.
3. NAMBA E Zimeanza lini?

Kwa mantiki hii, utafiti wako hauna uhalali, maana namba E lazima ziwe chache.

Kama IST hazinunuliwi tena kwa kiwango kikubwa, nini ni Mbadala wake?
 
IST ipewe maua yake kwenye usajili wa No. D. Kwa utafiti usio rasmi asilimia 30 ya No.D ni magari ya IST. Lakini tangu usajili wa "E" uanze ni IST chache sana zimesajiliwa. Kwa utafiti usio rasmi Nissan Dualis inakimbiza sana kwenye usajili wa "E".

Kwa Nini watu wameacha kuchangamkia IST kama hapo awali?
Zamani pijo,bito n.k
Chaser
Mark 2
 
Back
Top Bottom