Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,455
- 11,435
Kutokana na taarifa za ukubwa wa jeshi la Israel na umiliki wa silaha za kisasa,haikutarajiwa kwamba kungetokea nchi yoyote ile ikajiamini kuirushia makombora kulenga maeneo yake muhimu hasa ikizingatiwa kuwa iliwahi kuyashinda mataifa kadhaa ya kiarabu mwaka 1967 katika vita maarufu vya siku 7.
Iran kwa ujasiri mkubwa imefanya hivyo na siku zimepita na historia imeandikwa kuwa Israel imepigwa na imeemewa kurudisha mapigo.
Kuna mataifa kadhaa yameisaidia Israel kujilinda na madhara ya mashambulio hayo ambayo kama si msaada huo basi kungetokea madhara kiwango kikubwa.Mataifa hayo ni Marekani,Uiengereza,Ufaransa na Ujerumani kwa upande mmoja.
Upande wa pili ni mataifa matatu ya kiarabu ambayo ni Jordan,UAE na Saudi Arabia ambayo kwanza yaliruhusu anga zao kuruka ndege za F35 za Israel kuyawahi makombora ya Iran kabla hayajaingia anga la Israel.Vile vile nchi hizo ziliwasha mitambo yao ya kudungulia vitu virukavyo juu ya anga zao ambapo droni nyingi za Iran ziliweza kudunguliwa kabla hazijafika Israel zilikokusudiwa.
Baada ya shambulio hilo la Iran iwapo Israel itakusudia kurudisha kipigo itabidi ipate ruhusa rasmi ya nchi za kiarabu jiran nayo ili kurusha ndege au makombora ya aina nyengine.Ruhusa hiyo itakuwa ni tofauti na ule ushirikiano legelege wa umoja dhidi ya Iran uliotumiwa na mataifa hayo ya kiarabu kuzuia mashambulizi dhidi ya Israel.Mataifa hayo hayatoweza kufanya hivyo tena kwani tayari yamejulikana na Iran imeshatoa vitisho dhidi yao.
Uzito mwengine mkubwa ni kuwa marafiki na washirika wa Israel kutoka Marekani na Ulaya tayari wameionya Israel isirudishe majibu kiholela kwani kufanya hivyo kutachochea Hizbullah kutumia silaha zake kali zaidi ambazo haijazitumia na italeta ulemavu kwa eneo lote la kaskazini ya Israel na hata kufika maeneo yote.Kurudisha majibu kutachochea mahasimu wengine wa Israel kama Houth na Syria nao kuanzisha mashambulizi rasmi kuisaidia Iran.
Mwisho wa yote jeshi la Israel ambalo tayari limesambaa na kutumia nguvu kubwa Gaza litaingia udhaifu wa kuendeleza mapigano peke yake na ya muda mrefu na Iran.
Zaidi unaweza ukaongeza maarifa hapo chini.
Iran kwa ujasiri mkubwa imefanya hivyo na siku zimepita na historia imeandikwa kuwa Israel imepigwa na imeemewa kurudisha mapigo.
Kuna mataifa kadhaa yameisaidia Israel kujilinda na madhara ya mashambulio hayo ambayo kama si msaada huo basi kungetokea madhara kiwango kikubwa.Mataifa hayo ni Marekani,Uiengereza,Ufaransa na Ujerumani kwa upande mmoja.
Upande wa pili ni mataifa matatu ya kiarabu ambayo ni Jordan,UAE na Saudi Arabia ambayo kwanza yaliruhusu anga zao kuruka ndege za F35 za Israel kuyawahi makombora ya Iran kabla hayajaingia anga la Israel.Vile vile nchi hizo ziliwasha mitambo yao ya kudungulia vitu virukavyo juu ya anga zao ambapo droni nyingi za Iran ziliweza kudunguliwa kabla hazijafika Israel zilikokusudiwa.
Baada ya shambulio hilo la Iran iwapo Israel itakusudia kurudisha kipigo itabidi ipate ruhusa rasmi ya nchi za kiarabu jiran nayo ili kurusha ndege au makombora ya aina nyengine.Ruhusa hiyo itakuwa ni tofauti na ule ushirikiano legelege wa umoja dhidi ya Iran uliotumiwa na mataifa hayo ya kiarabu kuzuia mashambulizi dhidi ya Israel.Mataifa hayo hayatoweza kufanya hivyo tena kwani tayari yamejulikana na Iran imeshatoa vitisho dhidi yao.
Uzito mwengine mkubwa ni kuwa marafiki na washirika wa Israel kutoka Marekani na Ulaya tayari wameionya Israel isirudishe majibu kiholela kwani kufanya hivyo kutachochea Hizbullah kutumia silaha zake kali zaidi ambazo haijazitumia na italeta ulemavu kwa eneo lote la kaskazini ya Israel na hata kufika maeneo yote.Kurudisha majibu kutachochea mahasimu wengine wa Israel kama Houth na Syria nao kuanzisha mashambulizi rasmi kuisaidia Iran.
Mwisho wa yote jeshi la Israel ambalo tayari limesambaa na kutumia nguvu kubwa Gaza litaingia udhaifu wa kuendeleza mapigano peke yake na ya muda mrefu na Iran.
Zaidi unaweza ukaongeza maarifa hapo chini.