mchawi wa kusini
JF-Expert Member
- Apr 18, 2018
- 809
- 818
Habari JF Ili mjue nani mwamba Kati ya Iran na Israel fuatana na mimi twende pamoja.
IRAN NA ISRAEL,NANI MWAMBA?
Tarehe 13/04/2024,Islamic Revolutionary Guards Corps (IRGC) ambayo ni tawi la kijeshi la nchi ya Iran,ikishirikiana na kikundi kutoka nchi ya Iraq(Iraqi Popular Mobilization Forces),kikundi cha Hezbollah ya Lebanon,na kikundi cha Houthis ya Yemeni walianza mashambulizi dhidi ya nchi ya Israel.Walitumia dron na ndege zisizo na rubani na aina mbalimbali za silaha.Hayo mashambulizi yalipewa jina la 'Operation True Promise'(OTP)!Zaidi ya mashambulizi 300 yamefanywa na makundi hayo!
Kwenye mashambulizi hayo makali,nchi ya Israel ilidai kwamba imeweza kuzuia mashambulizi hayo kwa asilimia 99 kwa njia ya kunasa au kudungua makombora hewani,tena nje ya nchi hiyo.Jeshi la Israel(IDF)imetumia teknoljia yake ya kunasa makombora ya 'Arrow 3 System', 'David's Sling','Iron Dome','Patriot System' na 'Iron Beam',huku ikisaidiwa na washirika wake ambao ni nchi za Marekani, Uingereza, Ufaransa na Yordani(Jordan).Ufaransa umeenda mbali zaidi kwa kutuma meli yake kubwa ya kijeshi kutoa huduma za ujasusi wa anga(air surveillance).Nchi ya Jordan imesema inalinda wananchi wake kwa kudungua ndege na makombora mengi kutoka Iran...Wao wameipa ushirika wao jina la 'Operation Iron Shield',eti kwakuwa wao hawapigani,wanazuia tu🥹!
Sasa nani mwenye nguvu zaidi za kijeshi kati ya Iran na Israel?Jibu unaweza ukawa nalo.
Iran ni kubwa zaidi kuliko Israel kijiografia na ina idadi ya watu karibu milioni 90, karibu mara 10 zaidi ya Israeli - lakini hii haimaanishi kuwa ina nguvu kubwa zaidi ya kijeshi.....Elewa huu ukweli.
Iran imewekeza fedha nyingi kwenye makombora na ndege zisizo na rubani. Ina hifadhi kubwa ya silaha hizo lakini pia imekuwa ikitoa kiasi kikubwa kwa washirika wake - Wahouthi nchini Yemen na Hezbollah nchini Lebanon,na nchi nyinginezo.
Inachokosa ni mifumo ya kisasa ya ulinzi wa anga na ndege za kivita. Urusi inaaminika kushirikiana na Iran kuboresha hizo, kwa kurudisha msaada wa kijeshi ambao Tehran imetoa Moscow katika vita vyake na Ukraine - hasa katika mfumo wa ndege zisizo na rubani za Shahed ambazo Warusi sasa wanaripotiwa kutengeneza wenyewe.
Sasa shida kubwa kwa Iran ni kwamba hawezi kumpiga Israel bila kupita kwenye anga ya nchi zingine....hata ingawa nchi nyingi ni washirika wake.
Kwa upande wake, Israeli ina moja ya vikosi vya anga vya juu na vya kisasa zaidi ulimwenguni. Kulingana na ulinganishi wa kijeshi wa IISS, Israel ina takriban vikosi 14 vya ndege - ikiwa ni pamoja na F15, F16 na ndege za hivi punde za F-35.
Israel pia ina tajriba ya kufanya mashambulizi ndani kabisa ya maeneo ya mahasimu wake.
Pia itambulike,Israel ina uwezo mkubwa sana wa kuyanasa au kudungua makombora kutoka nje ya nchi,yakiwa angani.Kitu ambacho Iran haina!
Sasa unaweza kujaji mwenyewe...
IRAN NA ISRAEL,NANI MWAMBA?
Tarehe 13/04/2024,Islamic Revolutionary Guards Corps (IRGC) ambayo ni tawi la kijeshi la nchi ya Iran,ikishirikiana na kikundi kutoka nchi ya Iraq(Iraqi Popular Mobilization Forces),kikundi cha Hezbollah ya Lebanon,na kikundi cha Houthis ya Yemeni walianza mashambulizi dhidi ya nchi ya Israel.Walitumia dron na ndege zisizo na rubani na aina mbalimbali za silaha.Hayo mashambulizi yalipewa jina la 'Operation True Promise'(OTP)!Zaidi ya mashambulizi 300 yamefanywa na makundi hayo!
Kwenye mashambulizi hayo makali,nchi ya Israel ilidai kwamba imeweza kuzuia mashambulizi hayo kwa asilimia 99 kwa njia ya kunasa au kudungua makombora hewani,tena nje ya nchi hiyo.Jeshi la Israel(IDF)imetumia teknoljia yake ya kunasa makombora ya 'Arrow 3 System', 'David's Sling','Iron Dome','Patriot System' na 'Iron Beam',huku ikisaidiwa na washirika wake ambao ni nchi za Marekani, Uingereza, Ufaransa na Yordani(Jordan).Ufaransa umeenda mbali zaidi kwa kutuma meli yake kubwa ya kijeshi kutoa huduma za ujasusi wa anga(air surveillance).Nchi ya Jordan imesema inalinda wananchi wake kwa kudungua ndege na makombora mengi kutoka Iran...Wao wameipa ushirika wao jina la 'Operation Iron Shield',eti kwakuwa wao hawapigani,wanazuia tu🥹!
Sasa nani mwenye nguvu zaidi za kijeshi kati ya Iran na Israel?Jibu unaweza ukawa nalo.
Iran ni kubwa zaidi kuliko Israel kijiografia na ina idadi ya watu karibu milioni 90, karibu mara 10 zaidi ya Israeli - lakini hii haimaanishi kuwa ina nguvu kubwa zaidi ya kijeshi.....Elewa huu ukweli.
Iran imewekeza fedha nyingi kwenye makombora na ndege zisizo na rubani. Ina hifadhi kubwa ya silaha hizo lakini pia imekuwa ikitoa kiasi kikubwa kwa washirika wake - Wahouthi nchini Yemen na Hezbollah nchini Lebanon,na nchi nyinginezo.
Inachokosa ni mifumo ya kisasa ya ulinzi wa anga na ndege za kivita. Urusi inaaminika kushirikiana na Iran kuboresha hizo, kwa kurudisha msaada wa kijeshi ambao Tehran imetoa Moscow katika vita vyake na Ukraine - hasa katika mfumo wa ndege zisizo na rubani za Shahed ambazo Warusi sasa wanaripotiwa kutengeneza wenyewe.
Sasa shida kubwa kwa Iran ni kwamba hawezi kumpiga Israel bila kupita kwenye anga ya nchi zingine....hata ingawa nchi nyingi ni washirika wake.
Kwa upande wake, Israeli ina moja ya vikosi vya anga vya juu na vya kisasa zaidi ulimwenguni. Kulingana na ulinganishi wa kijeshi wa IISS, Israel ina takriban vikosi 14 vya ndege - ikiwa ni pamoja na F15, F16 na ndege za hivi punde za F-35.
Israel pia ina tajriba ya kufanya mashambulizi ndani kabisa ya maeneo ya mahasimu wake.
Pia itambulike,Israel ina uwezo mkubwa sana wa kuyanasa au kudungua makombora kutoka nje ya nchi,yakiwa angani.Kitu ambacho Iran haina!
Sasa unaweza kujaji mwenyewe...