Namna ya shambulizi la Israel huko Isfahan-Iran inathibitisha Israel wamedhamiria na wanawaalika Iran kwa vita kamili.

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,990
46,767
Tukio la Jana la Israel kushambulia kwa ndege nchini Iran kujibu shambulizi la drones la Iran lililotangulia ni la kiwango cha juu kuashiria vita kamili . Hili Shambulizi lilipangwa kwa mkakati kama vile jeshi lililoko vitani serious na sio kama michezo ya kidali poo anayojaribu kufanya Iran. Hili ni shambulizi la mkakati mpana ukilitizama kwa sababu

Moja, Kuna chenga ya kijeshi waliofanyiwa Iran, ''military deception''(MILDEC) na serikali ya Israel. Chenga ya kijeshi ni kitendo cha kumuaminisha kiuongo adui kwamba utafanya au hautafanya jambo fulani ili kumchanganya afanye namna itakavyokuwa na faida kwako, ni kama kumpoteza maboya. Baada ya shambulio la Iran serikali ya Israel ilikaa vikao vingi na taarifa za mwisho za vikao hivyo zilizotoka ziliashiria Israel hawatafanya shambulizi lolote ndani ya Iran hivi karibuni lakini muda mfupi tu wameshambulia. Hii ni tofauti na vile Iran ilivyofanya shambulizi la kupanga la droni na kulitekeleza kwa siku nzima ikiwapa Israel na washirika wake muda mrefu wa kutosha kujipanga kukabiliana nalo.

Mbili, wamepiga karibia katikati kabisa ya Iran na zaidi wamepiga eneo muhuimu na la kimkakatil la Iran kijeshi na kiulinzi. Isfahan ni eneo ambalo kuna miradi ya nuclear, kambi kubwa ya jeshi na viwanda vya uzalishaji silaha zikiwemo droni. Hili ni onyo kwa Iran kwamba wamedhamiria vita na wanaweza kufika na kupiga popote katika nchi hiyo yenye ukubwa wa eneo mara mbili ya Tanzania.

Tatu, Israel wamepiga nchi tatu kwa wakati mmoja kwa mkupuo. Katika siku moja wameshambulia Syria, Iraq na Iran kuwaonyesha wa-Iran kwamba wako tayari kwa lolote.
Sasa tutegemee majibu kutoka kwa Iran.

Nne, Israel imeonyesha kwamba inaweza kufanya maamuzi yake peke yake kama nchi huru bila kujali washirika wake wa Marekani na Ulaya linapokuja suala la ulinzi, vita na pride ya nchi yao. Pamoja na msimamo wa Marekani na Uingereza wa kwamba hawataiunga Israel katika mashambulizi ya Iran kwa sasa, Israel imeendelea mbele na kufanya mashambulizi yenyewe kama ilivyopanga na kuona inafaa bila kujali msimamo wa washirika wake.
 
Kila mtu wakiwemo viongozi wa Israel yenyewe wameona aibu kulizungumzia hili shambulio kutokana na kushindwa kufikia malengo.

Shambulio lililozuiliwa kiulani na Iran yenyewe bila madhara yoyote, unaweza kufananishaje na lile lililoshindwa kuzuiwa na nchi zaidi ya 8 na likapiga target iliyokusudiwa!

Shambulio la Iran liliishtua na kushangaza dunia jinsi lilivyofanikiwa kupenya ngome za ulinzi za mataifa kama US, UK, France, Germany, Saudi Arabia, Jordan, Iraq, Syria na Israel yenyewe. Hili la Israel watu wengi duniani hawajui kama limetokea maana halikuleta madhara. Lakini pia limeivua nguo Israel kwa shambulio lake kuzuiwa na nchi moja tu (Iran) bila msaada wa US wala UK.
 

Attachments

  • Screenshot 2024-04-19 at 12.03.15.png
    Screenshot 2024-04-19 at 12.03.15.png
    632.3 KB · Views: 6
Naona unajitekenya na kujamba mwenyewe. Kila mtu wakiwemo viongozi wa Israel yenyewe wameona aibu kulizungumzia hili shambulio kutokana na kushindwa kufikia malengo.

Shambulio lililozuiliwa kiulani na Iran yenyewe bila madhara yoyote, unaweza kumfananishaje na lile lililoshindwa kuzuiwa na nchi zaidi ya 8 na likapiga target iliyokusudiwa!
Acheni kujifariji hakuna shambulizi lolote lililo fanyika ndani ya Iran zaidi ya vidrone vilivyo tunguliwa mjini Isfahan.
Tuwasikilize Iran au tuwasikilize ninyi? Maana hata Iran wenyewe wanatofautiana katika utoaji wa taarifa huku wakiwa wame block mawasiliano ya maeneo yaliyoshambuliwa.
 
Nakuunga mkono mtoa mada hapo juu humu wengi ni wafia dini wamejawa na misimamo mikali na Mori nyingi ni watu wa kwenda kama nyumbu sasa Kuna mmoj hapo juu yey anataka Israel ijibu kama ilivyo shambuliwa drone 150 missiles 150 au Israel yeye ajibu kwa 1000 sasa 😂😂 yani kam watoto Yan tena wa shule ya msingi... Israel wanatumia akil San wao wametoa response ila ni kam message tu sio kumatch Iran attacks ni kama vile wanajua kifatacho ni nn na wamejiandaa jaman jaman hupugani vita kwa mzuka ya kidin na vitisho kwamba ukigusa nakulipiza mara 100 ni uzamani huo it's strategy naamin Israel ametuma message na Yuko tayal kwa hatua ifatayo ngoja uone Iran ilivyo na akili za kondoo itajibu mzima mzima
 
Tukio la Jana la Israel kushambulia kwa ndege nchini Iran kujibu shambulizi la drones la Iran lililotangulia ni la kiwango cha juu kuashiria vita kamili . Hili Shambulizi lilipangwa kwa mkakati kama vile jeshi lililoko vitani serious na sio kama michezo ya kidali poo anayojaribu kufanya Iran. Hili ni shambulizi la mkakati mpana ukilitizama kwa sababu

Moja, Kuna chenga ya kijeshi waliofanyiwa Iran, ''military deception''(MILDEC) na serikali ya Israel. Chenga ya kijeshi ni kitendo cha kumuaminisha kiuongo adui kwamba utafanya au hautafanya jambo fulani ili kumchanganya afanye namna itakavyokuwa na faida kwako, ni kama kumpoteza maboya. Baada ya shambulio la Iran serikali ya Israel ilikaa vikao vingi na taarifa za mwisho za vikao hivyo zilizotoka ziliashiria Israel hawatafanya shambulizi lolote ndani ya Iran hivi karibuni lakini muda mfupi tu wameshambulia. Hii ni tofauti na vile Iran ilivyofanya shambulizi la kupanga la droni na kulitekeleza kwa siku nzima ikiwapa Israel na washirika wake muda mrefu wa kutosha kujipanga kukabiliana nalo.

Mbili, wamepiga karibia katikati kabisa ya Iran na zaidi wamepiga eneo muhuimu na la kimkakatil la Iran kijeshi na kiulinzi. Isfahan ni eneo ambalo kuna miradi ya nuclear, kambi kubwa ya jeshi na viwanda vya uzalishaji silaha zikiwemo droni. Hili ni onyo kwa Iran kwamba wamedhamiria vita na wanaweza kufika na kupiga popote katika nchi hiyo yenye ukubwa wa eneo mara mbili ya Tanzania.

Tatu, Israel wamepiga nchi tatu kwa wakati mmoja kwa mkupuo. Katika siku moja wameshambulia Syria, Iraq na Iran kuwaonyesha wa-Iran kwamba wako tayari kwa lolote.
Sasa tutegemee majibu kutoka kwa Iran.
Ulivyoandika utazan ww ndii neta yau umesifia sanaa, kwa ufupi hujaleta habari Bali maelezo yote yliotoa ya kusifia tu
 
Kama vidume pigeni tuone, Iran kapiga kambi mbili na kuua wamajeshi kadhaa wamefariki..Tarifa ya wali mliadai mmezui makombora 99% sasa mnasema 84%.

Dhumuni lenu👉 Wale wanaowaita taifa la Mungu wasikate tamaa ila deep inside hamna huo uwezo , syria na Gaza kote wamekubali ila Iran mnapitisha drones za kufukuza nzinge sio mashamba ya mahindi hao.
 
Naona unajitekenya na kujamba mwenyewe. Kila mtu wakiwemo viongozi wa Israel yenyewe wameona aibu kulizungumzia hili shambulio kutokana na kushindwa kufikia malengo.

Shambulio lililozuiliwa kiulani na Iran yenyewe bila madhara yoyote, unaweza kumfananishaje na lile lililoshindwa kuzuiwa na nchi zaidi ya 8 na likapiga target iliyokusudiwa!

Shambulio la Iran liliishtua na kushangaa dunia jinsi lilivyofanikiwa kupenya ngome za ulinzi za mataifa kama US, UK, France, Germany, Saudi Arabia, Jordan, Iraq, Syria na Israel yenyewe. Hili la Israel watu wengi duniani hawajui kama limetokea maana halikuleta madhara. Lakini pia limeivua nguo Israel kwa shambulio lake kuzuiwa na nchi moja tu (Iran) bila msaada wa US wala UK.
Mkuu wengi humu hawajielewi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom