Iran yaishambulia Israel, sarafu yake yaporomoka kwa kiwango cha ajabu

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,770
41,630
Usiku wa Jumamosi, tarehe13 April 2024, Iran iliishambulia Israel kwa makombora mbalimbali na drones 300, huku mitambo ya Israel, Marekani, Uingereza na Jordan, ikidaka zaidi ya 99% ya makombora yote, na karibia yote yakitunguliwa kabla ya kuingia anga la Israel. Machache yaliyofanikiwa kutua Israel yalileta uharibifu mdogo ikiwemo kumjeruhi binti wa umri wa miaka 14 ambaye alijeruhiwa na vipande vya drones iliyotunguliwa akiwa angani.

Shambulio hilo linafuatia shambulia la Israel kwenye ubalozi mdogo wa Iran nchini Iran lililoua makamanda wawili wa ngazi ya juu kabisa wa jeshi la Iran, pamoja na maafisa wengine 11. Israel ilidai kuwa jengo hilo halikuwa ubalozi mdogo bali linatumiwa na makundi ya wapiganaji wanaoishambulia Israel wanaosaidiwa na Iran.

Kufuatia shambulio la jana, mataifa mengi yamelaani shambulio hilo na kuomba utulivu, huku mataifa karibia yote tajiri Duniani, yakisema kuwa yanasimama na Israel, yakiilaani Iran kuwa ndiyo chanzo cha migogoro Mashariki ya kati likiwemo shambulio la tarehe 7 October 2023 dhidi ya Israel lililozaa maafa makubwa yanayoendelea dhidi ya Wapalestina. Mataifa yenye uchumi mkubwa Duniani yamekutana jana juu ya hatua za kuchukua dhidi ya Iran, huku Israel ikiendelea na vikao kuamua hatua za kuchukua dhidi ya Iran. Waziri Mkuu wa Israel amesema kuwa Jeshi la Israel ni imara, wananchi wa Israel ni imara, na wanaishi kwa falsafa moja kuwa anayetishia usalama wao watamwangamiza.

Mara baada ya shambulio hilo, sarafu ya Iran imeporomoka ghafla kwa speed ya ajabu, ambapo sasa dollar moja inabadilishwa kwa rial 660,000, huku wananchi wengi wakihangaika kubafilisha pesa zao ili wazitunze katika sarafu za kigeni.

$1 = 660,000 Rial!!!

Tunasema shilingi yetu ni dhaifu, sijui hii ya Rial ya Iran, itaitwaje!!

Iran's Rial Dips to All-time Low Against US Dollar

The Iranian Rial continued its downward spiral on Saturday amidst escalating tensions with Israel and concerns of a potential war.

The US dollar surpassed the 660,000-rial mark for the first time on the open market.

With an annual inflation rate reaching about 50 percent, Iranians have been scrambling to convert their savings into hard currencies or gold.

The Rial's decline intensified following the recent Israeli attack on Iran's consulate in Syria and subsequent tensions between the two nations.

The Iranian government has yet to offer a public explanation for the sharp decline of the Rial.
 
Hii vipi ni feki...
Ajabu ni kwamba...pesa ya Tanzania ina thamani kuliko ya irani ila Iran Siyo masikini, hatembezi bakuli kama Mwigulu na Samia.
 

Attachments

  • Screenshot_20240415-121720_Samsung Internet.jpg
    Screenshot_20240415-121720_Samsung Internet.jpg
    277.3 KB · Views: 3
Mkuu acha kusikiliza CNN, wanakulisha matango pori.
Iran imetumia mbinu za hali ya juu sana ambayo haikutegemewa.
Iran imerusha drones za bei rahisi, zilizotunguliwa na makombora ghali sana ya Iron Dome.
Makombora ya Iron Dome yalipoelekea kuisha ndio zikarushwa supersonic missiles zilizoenda kuteketeza viwanja viwili vya ndege vya Israel.
Vita ni akili.
 
Hiyo ishuke mpaka isiwe na thamani kabisa wala sio kitisho iran anaishi kwa vikwazo ndani ya miaka 70 hiyo ndio dola kuu ya kiislamu isiyo shoboka na mtu na wanaonyesha kwa vitendo kuchukizwa na dhuluma dhidi ya wengine!

Vita siku zote vina madhara makubwa sana hasa kwa maisha ya wananchi.

Serikali ya Iran kwa miaka mingi imewafanya wananchi waishi kwa mateso na umaskini makubwa licha ya kuwa na utajiri mkubwa wa mafuta. Sehemu kubwa ya pato la Taifa inaishia kwenye masuala ya vita na silaha.
 
Acha ujinga wewe...
Vikwazo vipo kitambo sana...na hivyo vikwazo ndiyo vimefanya Irani iwe strong hii leo....

Asikudanganye mtu. Iran ni dhaifu sana kiuchumi, na ina negative economic growth wakati ina utajiri mkubwa wa mafuta.

As a result of Trump's reimposition of sanctions in 2018, Iran's economic growth fell by 13.6 percentage points, from a positive annual growth rate of 9.5% during 2016-2017, when the JCPOA had eased U.S. sanctions, to negative 4.1% per year.

Besides the 28% already in poverty, a further 40% of Iran's population was at risk of falling into poverty in the next two years, the World Bank said.

As of early 2022, 30 percent of Iran's households were living below the poverty line, and there are other reports revealing even more alarming figures.3 Apr 2023.
 
Hiyo ishuke mpaka isiwe na thamani kabisa wala sio kitisho iran anaishi kwa vikwazo ndani ya miaka 70 hiyo ndio dola kuu ya kiislamu isiyo shoboka na mtu na wanaonyesha kwa vitendo kuchukizwa na dhuluma dhidi ya wengine!
Aiseeee ana vikwazo vya nuda mrefu sana. Tatizo nini mpaka wamuwekee vikwazo sasa ni miaka 70?
 
Mkuu acha kusikiliza CNN, wanakulisha matango pori.
Iran imetumia mbinu za hali ya juu sana ambayo haikutegemewa.
Iran imerusha drones za bei rahisi, zilizotunguliwa na makombora ghali sana ya Iron Dome.
Makombora ya Iron Dome yalipoelekea kuisha ndio zikarushwa supersonic missiles zilizoenda kuteketeza viwanja viwili vya ndege vya Israel.
Vita ni akili.
Kwa hiyo wewe ndio upo detailed kuliko CNN? Waajemi wa kisiwandui mna shida sana.
 
Mkuu acha kusikiliza CNN, wanakulisha matango pori.
Iran imetumia mbinu za hali ya juu sana ambayo haikutegemewa.
Iran imerusha drones za bei rahisi, zilizotunguliwa na makombora ghali sana ya Iron Dome.
Makombora ya Iron Dome yalipoelekea kuisha ndio zikarushwa supersonic missiles zilizoenda kuteketeza viwanja viwili vya ndege vya Israel.
Vita ni akili.

Usidanganyike. Vyombo vyote vya habari Duniani, mpaka vya nchi za Kiarabu vimetangaza tukio hilo kwa kina. Mataifa ya Magharibi yamedhihirisha kuwa makombora na drones za Iran, siyo tishio kwao. Ni kombora aina moja tu ambalo ni supersonic, ndilo ambalo Iran haijatumia. Imetumia aina 3 tofauti za drones.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom