Bush Dokta
JF-Expert Member
- Apr 11, 2023
- 12,748
- 21,394
Duuh huyo Adamu ni nani? Alifanya nini na hizo picha walizipata wapi?Wanaume wawili, Furaha Jacob pamoja na Mustapha Kuhenga (28) wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakituhumiwa kuchapisha na kusambaza picha za ngono mtandaoni.
Jacob ambaye ni mkemia na Kuhenga mtaalamu wa TEHAMA, wanakabiliwa na mashtaka matatu ikiwa ni pamoja na kumtisha na kumsababishia msongo wa mawazo, Adam Mihayo.
Akisoma mashtaka hayo, Wakili wa Serikali, Cathbert Mbilingi amesema shtaka la kwanza la shambulio la mtandao linamhusu Jacob pekee ambapo Februari 11, 2024 anadaiwa kutuma video WhatsApp yenye maudhui ya ngono kupitia simu yake kwa lengo la kumtishia Mihayo.
Kwa upande wa Kuhenga anadaiwa kati ya Desemba Mosi na Desemba 31, 2023 alituma video yenye maudhui ya ngono kwa kutumia simu yake kupitia mtandao wa WhatsApp na kumsababishia msongo wa mawazo Mihayo.
Shtaka la mwisho linawahusu watuhumiwa wote wawili ambapo wanadaiwa kuchapisha picha zenye maudhui ya ngono kwenye akaunti ya mtandao wa kijamii wa WhatsApp za Mihayo Desemba Mosi 2023 na Machi 2024.
Pia soma
- Furaha Dominic akamatwa akisambaza picha za Utupu
Swahili Times