Arusha: Wakili mbaroni kwa kusambaza picha za Makonda. Polisi wamnyima dhamana, wadai wanasubiri maelekezo kutoka juu

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,037
9,926
Jeshi la Polisi limemkamata wakili Yonas Masiaya na kumnyima dhamana. Tukio hilo limetokea jana jioni, Aprili 30, 2024, huku likiwaacha wengi wakijiuliza maswali kuhusu utaratibu wa kisheria.

Wakili Masiaya anatuhumiwa kwa kosa la kusambaza picha ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha katika makundi ya WhatsApp. Hata hivyo, licha ya tuhuma hizo kuonekana kuwa dhaminika, Jeshi la Polisi limekataa kumpa wakili huyo dhamana, wakisema wanangojea maelekezo kutoka ngazi za juu.

Leo, Mei Mosi, 2024, wakili Ngeeyan Oloibormunyei Laizer pamoja na familia ya wakili Masiaya wamejitokeza katika kituo cha Polisi kufuatilia suala hilo. Hata hivyo, jitihada zao zimegonga mwamba baada ya Polisi kudai bado wanangojea maelekezo kutoka kwa viongozi wao.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umeelekeza mawakili wake mkoani Arusha kuchunguza kwa karibu suala hilo na tayari wameanza maandalizi ya kufungua kesi dhidi ya Jeshi la Polisi kwa kushindwa kumpa dhamana wakili Masiaya.

Wito umetolewa kwa Jeshi la Polisi:

  • Kumwachia wakili Masiaya kwa dhamana.
  • Kufanya upelelezi kwa kuzingatia Sheria na Amri Kuu za Jeshi la Polisi (PGO), bila kusubiri maelekezo kutoka juu ambayo ni nje ya utaratibu wa kisheria.
  • Kufanya upelelezi kabla ya kumkamata wakili Masiaya endapo kuna tuhuma dhidi yake.
  • Kudai mabadiliko ya sheria ya makosa ya kimtandao ili kulinda uhuru wa watanzania katika matumizi yao ya mitandao kwa kuzingatia Sheria za ulinzi wa taarifa na faragha.
 
Kama kawaida waandishi mtaishia kuandika matamko marefuuuuuuu na kutoa matamko alafu imeisha hiyooo.

Yaani Tanzania kada ya waalimu na waandishi habari ukichanganya na binam zao mapolisi sijui mlilogwaga na nani sijui
 
Kazi imeanza. Kama ilivyokuwa Dar kipindi kile akiwa uongozini imeanza upya Arusha. RIP Ben Saanane
 
Jeshi la Polisi limemkamata wakili Yonas Masiaya na kumnyima dhamana. Tukio hilo limetokea jana jioni, Aprili 30, 2024, huku likiwaacha wengi wakijiuliza maswali kuhusu utaratibu wa kisheria.

Wakili Masiaya anatuhumiwa kwa kosa la kusambaza picha ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha katika makundi ya WhatsApp. Hata hivyo, licha ya tuhuma hizo kuonekana kuwa dhaminika, Jeshi la Polisi limekataa kumpa wakili huyo dhamana, wakisema wanangojea maelekezo kutoka ngazi za juu.

Leo, Mei Mosi, 2024, wakili Ngeeyan Oloibormunyei Laizer pamoja na familia ya wakili Masiaya wamejitokeza katika kituo cha Polisi kufuatilia suala hilo. Hata hivyo, jitihada zao zimegonga mwamba baada ya Polisi kudai bado wanangojea maelekezo kutoka kwa viongozi wao.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umeelekeza mawakili wake mkoani Arusha kuchunguza kwa karibu suala hilo na tayari wameanza maandalizi ya kufungua kesi dhidi ya Jeshi la Polisi kwa kushindwa kumpa dhamana wakili Masiaya.

Wito umetolewa kwa Jeshi la Polisi:

  • Kumwachia wakili Masiaya kwa dhamana.
  • Kufanya upelelezi kwa kuzingatia Sheria na Amri Kuu za Jeshi la Polisi (PGO), bila kusubiri maelekezo kutoka juu ambayo ni nje ya utaratibu wa kisheria.
  • Kufanya upelelezi kabla ya kumkamata wakili Masiaya endapo kuna tuhuma dhidi yake.
  • Kudai mabadiliko ya sheria ya makosa ya kimtandao ili kulinda uhuru wa watanzania katika matumizi yao ya mitandao kwa kuzingatia Sheria za ulinzi wa taarifa na faragha.
Wanasubiri maelekezo kutoka juu wapi? Ni juu mbinguni au juu wapi huko wanakosubiri kupata hayo maelekezo? Hivi dhamana kwa Watuhumiwa inatolewa kwa kujibu wa Sheria au kwa mujibu wa matakwa au maelekezo kutoka kwa mtu fulani?

Hivi ndani ya Jeshi lote la Polisi hakuna hata Askari Polisi mmoja ambaye mwenye akili nzuri kidogo wa kuweza kulikwamua Jeshi hilo ili liondokane na majanga kama haya????
 
Kama kawaida waandishi mtaishia kuandika matamko marefuuuuuuu na kutoa matamko alafu imeisha hiyooo.

Yaani Tanzania kada ya waalimu na waandishi habari ukichanganya na binam zao mapolisi sijui mlilogwaga na nani sijui
Hizo kada mnazilaumu tu, kiujumla watanzania tumerogwa.

Kwañi DP imechukuliwa kada nyingine walifanya nini?


Kila mwaka wa uchaguzi kura zinaibiwa hizo kada zinafanya nini?
 
Wacha kwanza ajifunze adabu.

Ujwqji mwingi ndio umemponza, jifunzeni kuheshimu uhuru wa watu pia sio kudai haki tu.
 
Jeshi la Polisi limemkamata wakili Yonas Masiaya na kumnyima dhamana. Tukio hilo limetokea jana jioni, Aprili 30, 2024, huku likiwaacha wengi wakijiuliza maswali kuhusu utaratibu wa kisheria.

Wakili Masiaya anatuhumiwa kwa kosa la kusambaza picha ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha katika makundi ya WhatsApp. Hata hivyo, licha ya tuhuma hizo kuonekana kuwa dhaminika, Jeshi la Polisi limekataa kumpa wakili huyo dhamana, wakisema wanangojea maelekezo kutoka ngazi za juu.

Leo, Mei Mosi, 2024, wakili Ngeeyan Oloibormunyei Laizer pamoja na familia ya wakili Masiaya wamejitokeza katika kituo cha Polisi kufuatilia suala hilo. Hata hivyo, jitihada zao zimegonga mwamba baada ya Polisi kudai bado wanangojea maelekezo kutoka kwa viongozi wao.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umeelekeza mawakili wake mkoani Arusha kuchunguza kwa karibu suala hilo na tayari wameanza maandalizi ya kufungua kesi dhidi ya Jeshi la Polisi kwa kushindwa kumpa dhamana wakili Masiaya.

Wito umetolewa kwa Jeshi la Polisi:

  • Kumwachia wakili Masiaya kwa dhamana.
  • Kufanya upelelezi kwa kuzingatia Sheria na Amri Kuu za Jeshi la Polisi (PGO), bila kusubiri maelekezo kutoka juu ambayo ni nje ya utaratibu wa kisheria.
  • Kufanya upelelezi kabla ya kumkamata wakili Masiaya endapo kuna tuhuma dhidi yake.
  • Kudai mabadiliko ya sheria ya makosa ya kimtandao ili kulinda uhuru wa watanzania katika matumizi yao ya mitandao kwa kuzingatia Sheria za ulinzi wa taarifa na faragha.
picha za utupu au
 
Back
Top Bottom