Dr. Chris Mauki vs Kataa Ndoa: Je, ndoa ni suala la Kisaikolojia? Ni lazima Uoe? Hayo na mengine mengi yamejibiwa hapa, sogea karibu kushiriki mjadala

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
631
960
Dr Mauki.jpg



JamiiForums imepata wasaa wa kuongea na Dr. Chris Mauki, Mtaalamu wa Saikolojia, Ndoa na Mahusiano, Malezi na Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam juu ya suala hili la Kataa Ndoa, mjadala ambao umekuwa mkali sana hasa kwa vijana wa zama hizi, twende kazi....

ndoa.jpg

SWALI: Ndoa ni nini? Je, ni suala la Kisaikolojia?

JIBU
: Ndoa ni muunganiko wa mwanume na mwanamke, ampao muunganiko huu unaweza ukawa umeunganishwa kiimani, kijamii, kimilia, kiserikali, lakini pia wote tunajua kwamba ipo sheria kwamba unapokaa na mtu wa jinsia ya tofauti kwenye nyumba yako zaidi ya siku 90 mkiwa na mahusiano ya kindoa basi inakuwa mmeona.

Pamoja na kuwa ndoa ni suala la kibaiolojia, kwasababu inahusisha vitu vya kibaiolojia ikijumuisha suala la ngono, pamoja na kwamba ndoa inahusisha pia suala la kisaikolojia ya kwamba ndani kuna mambo ya hisia, kuchukuliana kihisia, hisia za kuumia, hisia za furaha, na vitu kama hivyo, lakini pia ndoa ni jambo la kiimani. Wale wanaoamini kwenye Imani wanazungumza kwamba ndoa iliasisiwa na Mungu mwenyewe, alivyosema sio vyema mtu awe peke yake na hata ukiangalia Imani nyingi kabisa zinaonesha watu hao wa Imani zile kwamba Mungu alikuwa chanzo cha ndoa.

Sasa muundo wa ndoa unakuja kutofautiana na mwandamu anavyoendelea kijamii, nk.

ndoa3.jpg

Sio lazima, kwasababu kuna baadhi ya imani ambazo watu wa Imani hizo viongozi wao hawaoi, ingawa inaanza kwenda kwenye mjadala sasa kwamba labda waruhusiwe kuoa kwasababu tunaona kwamba kuna vitendo vinavyohusika wao kufanya ambavyo kama vinalazimisha kutaka kuwa na mahusiano lakini hawana mahusiano hayo kirasmi.

Inawezekana siyo lazima lakini ni muhimu, hoja iko wapi ya kwamba ni muhimu kuwa na ndoa. Hoja ni kwamba alivyoumbwa mwanaume ndani yake amewekewa uhitaji wa kihisia na uhitaji wa kibaiolojia ambaye hakuna wa kutumiza au wa kumtosheleza isipokuwa mwanamke, na ndani ya mwanamke alivyoumbwa kwa asili yake amewekewa mahitaji ya kihisia na mahitaji ya kibinadamu, yaani ya kibailojia ambayo hakuna wa kuyatosheleza isipokuwa mwanaume.

Baada ya hayo mahitaji ya kibaiolojia yakaja mahitaji mengine – Mahitaji ya Kijinsia, ambayo haya yanatokana na tamaduni na maisha ya watu tofauti tofauti ambayo wameyafanya, yakafanya sasa mwanaume amuhitaji mwanamke, na mwanamke amuhitahi mwanaume. Kuna jamii ambazo mwanaume hawezi kuishi peke yake mpaka apate mtu wa kumpikia, maana yake ni kwamba inabidi aoe, kuna jamii ambazo manamke hawezi kuishi peke yake mpaka apate mtu wa kumhudumia mahitaji yake maana yake itabidi apate mwanaume.

Kwahiyo ukifikiria utakuja kugundua kwamba hata kama siyo lazima, kwasababu kuna watu ambao hawajaoa na hawaolewa na hawafi lakini ni muhimu sana kuwa na mwenza. Sasa kwenye kutosheleza haya mahitaji ya kihisia na kibaiolojia mtu anaweza kuwa na mwanamke tu bila ndoa au anaweza kuwa na ndoa. Unapokuwa na mwanamke bila ndoa mahitaji hayo utayatimiza kabisa lakini kijamii bado watu wataona siyo halali wewe kuwa na huyo mtu, ni mpaka uwe na ndoa. Sasa ndoa ni chombo cha kuhalalisha yale mahusiano ya mwanamke na mwanaume ili jamii pamoja na Imani ifahamu kabisa kwamba unaishi na yule mtu.

Swali: Je, malezi (Trauma kwenye Makuzi na Malezi) yanaweza kuchagia mtu Kuchukia/Kupenda wazo la kuoa?

farakano11.jpg

Jibu: Ni kweli kwamba maumivu yoyote ya kihisia au nafsi katika makuzi yam toto wakike au wakiume (kitaalamu Trauma) inaweza ikachangia kuharibu mtazamo wa mtu kwenye kuingia katika mahusiano pamoja na ndoa?

Wako watu leo wameshindwa kuingia kwenye mahusiano na ndoa na hata walipojaribu meshindwa na kutoka. Wale walioingia nao kwenye ndoa hawakuwahi kujua ni nini lakini wanaona kabisa hakuwa sawa na alikuwa hapendeki na wengine jinsi unavyojaribu kumpenda sana na unashindwa kwasababu hapendeki ndio maana watu wana matatizo ya kisaikolojia yanayoitwa “Dismissive attachment Disorder”, yaani jinsi unavyompenda ndio jinsi anavyokuumiza kwasababu ndani yake aliumizwa akiwa mdogo. Picha yake ya mahusiano na ndoa ilikuwa mbovu katika hali ambayo imeharibu mtazamo wake wa mahusiano. Kwahiyo ni ngumu yeye kukubali mahusiano au kuingia kwenye mahusiano pampja na ndoa, n ahata katika nyakati atakazojikuta kaingia basi mafanikio yake au kukaa kwenye hayo mahusiano yake kutakuwa kudogo.

Trauma hizi zinaweza kusababishwa na vitu kama kubakwa katika umri mdogo tunasema kisaikolojia kwenye umri wa miaka 2 mpaka 12, kuishi katika familia (ndoa) ambayo ilikuwa katika magomvi sana kati ya baba na mama, kukosa mahusiano mazuri ya baba kwa hasa kwa mabinti (father-daughter relationship) kumsaidia kwenye kujiamini nk, lakini pia kuona ndoa au kukaa na ndoa iliyovunjika (wazazi waliotengana) katika umri mdogo pamoja na malezi ya mzazi mmoja (single parenting) yenye changamoto, sababu kuna malezi ya mzazi mmoja yanaweza yasiwe na changamoto lakini kwa kiasi kikubwa malezi ya mzazi mmoja yanaweza kuwa na changamoto yakamfanya mtoto wa kike au wa kiume akaumia hisia zake, akabalisha mtazamo wake kuhusu mahusiano na ndoa kwahiyo kesho na keshokutwa akawa na mtazamo hasi sana kuhusu ndoa na mwisho ikaathiri uwezo wako wa kuingiz, kukaa, kufanikiwa na kufurahia ndoa

Swali: Je, utandawazi unachangia vipi kwenye suala hili la vijana kukataa/kukubali ndoa?

globalization.png

Jibu: Kubadilika kwa maendeleo ya kijamii na maendeleo ya kiteknolojia (sayansi ya teknolojia) kunachangia kwa kiasi kikubwa sana. Utandawazi umechangia kwa kiasi kikubwa, utandawazi umewafungua na kuwaweka watoto wengi na vijana wengi kwenye urahisi wa kufikia na kupata hamu au haja ya tendo landoa au kufikia mshindo kwa mambo mengi. Teknolojia imeleta midoli, mashine, uwezekanao au urahisi wa kumpata mwanamke wa kulala naye kwa siku moja au kwa dakika chache kutoka kwa wanaoitwa Malaya (sex workers) wanaofanya kazi za kujiuza, ambapo kuna watu wa miaka 45, 50, nk hajaoa lakini ana uwezo wa kufanya ngono kila anapotaka kwasababu anawanunua kwa bei rahisi tu .

Kwahiyo maendeleo ya kijamii na maendeleo ya kisayansi na kiteknolojia hasa katika utandawazi kuna baadhi ya vitu vimekuja vimethiri kwa kiasi kikubwa mitazamo ya watu au watu kuona ndoa ni muhimu, lakini kingine kibaya zaidi ni kwamba utandawazi umerahisisha na kuweka bayana taarifa nyingi za watu wanaolaumu, kuua, na kukejeli, kuonesha waliyoumizwa kwenye ndoa. Kwahiyo jamii kubwa inaanza kupata picha kwamba ndoa siyo kitu tena cha furaha, bali ndoa ni kitu cha maumivu n ani kitu cha kukwepa na baadhi ya mitazamo hii hasi ndio zimehusika kuchangia sana kuku ana kuongezekakwa spidi kwa jamii la LGBTQAI+

SWALI: Peer pressure/Mtandaoni/Jamii inaweza kuwa sababu ya kufanya vijana Kuchukia/Kupenda ndoa?

peer.jpg

JIBU: Swali la msukumo wa makundi (peer pressure) linajibuwa na swali nililojibu hapo juu, kwamba watu wengi ambo ni wa rika la kufanana unapoona kwamba wengi wanatoka kwenye ndoa, unapoona kwamba wengi wanalaumu mambo ya ndoa au mahusiano, unapoona kwamba wengi wanakuonesha kwamba kuwa na mwanaume mmoja sio dili tafuta hela, au unapokuwa na mwanamke mmoja hufurahii (huinjoy) na wewe inakushawishi vilevile kutokana na nadharia mbalimbali kama za Albert Bandura - social learning theory zinaonesha kwamba watu wengi wanajifunza kwa kuiga, kwa kuona (modeling imitation) wanaona na kujifunza mwishowe wanakuwa hivyo hivyo.

Lakini pia unaonawaona watu wa rika lako kwa jinsi ambavyo alikuwa kwenye ndoa na kutoka, au alikuwa kwenye mahisano nab ado yupo lakini akaamua kubadilisha jinsia yake, kitendo hiki cha kuona watu wengi unaofanana nao, au wa umri wako au watu unaowajua wameenda kwenye mtazamo fulani kunashawishi kwa kiasi kikubwa na wewe kuchagua mtazamo ule au maisha yale kwasababu unaona kwamba hayo ndio maisha ya kuishi. Kwahiyo ni kweli kabisa kwamba awatu wa rika moja kwa namna ambayo wana mtazamo hasi katika ndoa inachangia sana watu wengi kuona ndoasiyo kitu cha kufurahisa tena kama ilivyokuwa zamani ambapo watu wengi walikuwa wanajivunia sanakuishi na kusubiri ndoa zao.

Je, nini maoni yako kwa haya machache aliyotueleza Dr. Mauki?

Itaendelea.....

Pia soma:

- Mjadala kwa wanaokataa Kuoa (Ndoa)
- Mjadala kwa wanaokubali kuoa (Ndoa)

======

Kwa muendelezo wa mahojiano haya soma:
Dr. Chris Mauki vs Kataa Ndoa 2: Feminists wanachangia kwa kiasi kikubwa watu kukataa ndoa. Kwa bahati mbaya sana asili haitakaa ibadilike!
 
. Kuhusu ndoa, hata mnengeandika vitabu billion 9000, lakini ndoa itabaki kuitwa kifungo Cha mateso.

. Waliofaidika na ndoa ni wazee wa zamani ila siyo Sasa. Na ndomaana kesi za kubambikiana watoto miaka ya hivi karibibuni zinazidi kushamiri.
 
Shukrani sana kwa mjadala huu umejaa madini mengi sana! Mbarikiwe sana!
Ingawa nina maswali mawili ambayo nadhani yametokana na majibu kutoka kwa Dr, Mauki.
Aliulizwa kuwa Je, utandawazi unachangia vipi kwenye suala hili la vijana kukataa/kukubali ndoa?
na amepata kujibu kwa upekee mzuri sana na kwa hoja pana! Ila katika hili swali langu ni hili:
Kutokana na ujio wa harakati za usawa na vuguvugu la mageuzi hususani ni harakati za usawa, Je mwanaume atapata faida ipi endapo akiingia kwenye ndoa, kuna utofauti upi ambao atapata kutoka kwa mwenzake baada ya kuwa wanandoa?
Swali la pili ni Mara kadhaa tumepata kukutana na wataalamu wa saikolojia wakizungumzia utofauti mkubwa baina ya ME na KE, kwa mtazamo wa saikolojia, wanawake wanaonekana ni watu walio emotional kuliko wanaume, Je kuna umuhimu wowote wa hisia katika ndoa, na je ni vyema kuwa na mwanamke ambae yupo sensitive sana katika hisia zake au mwanamke wa kawaida? na chaguo hili linaleta athari zipi katika muungano huu mtakatifu?!
Shukrani! Nipo!
 
the question of what you bring on the table for both men and women has brought fear of commitment hence people really don't want to get married but just wanna mingle around. This is why mostly people have multi lovers and the issue keeps on getting worse... not having a stable job or source of income can also be another case too, some men I know don't want to even be in a relationship with the idea of they can't really satisfy their partner's needs, so how a person like this get married and be there to contribute in providing for the new family?
 
What makes me not want to get married?

I don’t know about most men so I’m gonna speak for myself.

If you remove the desire to procreate and raise a family, why should a man get married? There really isn’t a huge motivation to get married if as a man, you do not desire children. The only other reasons I can think of are sex and companionship.

The challenge with modern relationships is that things have changed yet things still remain the same. Modern women want the best of both worlds. They want to be liberated women who have careers, have their own money and are in control of their lives with no interference from a man. No problem with that, that's all good. However the same women also have old fashioned expectations of men and what a man’s role should be especially when it comes to money. They still want the man to be the provider and responsible for the most if not all the financial responsibilities in the relationship. Quite a few modern women who are employed and earning good money still believe the “my money is my money, your money is our money” thinking. These are the same women who will get offended if you ask them to make you a meal or something like that. You will be labelled as an old fashioned male chauvinist who can’t handle a strong independent woman. For a man, it’s a no-win situation. Your supposed to be old fashioned when it comes to paying bills but new age when it comes to something like taking care of the house, cooking, cleaning etc.

A friend of mine who is in her 40s and unmarried recently posted a Facebook post saying something to the effect that a woman should never help a man pay rent. Doesn’t matter who’s earning more as far as she’s concerned, it’s a man’s responsibility to provide a roof over the family’s head. As a man I have no problem with that, what I do have is when the same woman calls me a chauvinist for asking for dinner. It’s like, there clear rules of what’s expected from a man but very ambiguous rules on what’s expected from a woman in a relationship.

Sex? Nope, only if she feels like it, its her body not yours.

Cooking for you? Nope, her mum used to do that for her dad and she’s not gonna do it for you because she’s liberated and you can damn well cook for yourself.

Cleaning the house? Get a maid you old fashioned chauvinist!

So if a man doesn’t desire kids or doesn’t want a family, getting married has few benefits if any benefits.
 
the question of what you bring on the table for both men and women has brought fear of commitment hence people really don't want to get married but just wanna mingle around. This is why mostly people have multi lovers and the issue keeps on getting worse... not having a stable job or source of income can also be another case too, some men I know don't want to even be in a relationship with the idea of they can't really satisfy their partner's needs, so how a person like this get married and be there to contribute in providing for the new family?
Kuna mwamba alikuwa anaitwa Kevin Samuels Mungu amrehemu1 Aliwahi kusema mwanamke akiwa anamtafuta mwanaume ataweka vigezo vingi sana kiasi kwamba unaweza kutengeneza kamusi ila ukimuuliza analeta nini kwenye mahusiano utaandika tu nyuma ya stamp!
 
Ndoa itaendelea vipi kutumika kuhalarisha mahusiano ya kimapenzi hili hali sheria iliyoianzisha hapa Tz haifai kwa sasa?

Sahivi kuna tofauti gani kati ya mtu me na ke katika ulimwengu huu wa usawa?

Kwanini hakuna huo usawa kwenye ndoa? Tena kila utajwapo hauna maana ya usawa bali upendeleo kwa mwanamke?

Hitimisho: ndoa zitaeleweka tukibadili sheria zetu za ndoa ziendane na maisha ya wakati wetu.
 
Back
Top Bottom