Wasaalam.
Nawashukuru watanzania wote kwa ufuatiliaji wa wasilisho la bajeti ya wizara ya jamii 2024/25.
Namshukuru Mungu kwamba, mjadala mkubwa wakati wa uwasilishaji, ni ishara ya elimu kuifikia jamii kwa kina kuhusu kupambana na kutokomeza ukatili wa kijinsia na kudhibiti mmomonyoko wa...
Wasalaam,
Ile siku ni Leo tarehe 15 Mei, 2024. Kila mkoa unaadhimisha na wilaya zake na kata zake na vijiji vyake.
Vyombo vya habari vinapaza sauti. Ukiona kimya uliko, basi kuna mtu hajatimiza tu wajibu wake wa kupaza sauti au wa kusikiliza sauti iliyopazwa.
Sisi tuko Dodoma, Viwanja vya...
Wasalaam,
Sehemu kubwa ya jamii haijui sheria mbalimbali hivyo, hushindwa kuchukua hatua dhidi ya wanaovunja sheria hizo na kuharibu ustawi wa jamii ya makundi yote.
Kusambaza maudhui mbalimbali kupitia habari mitandaoni inahitaji kufahamu sheria husika.
Hawa MbengoTv siyo peke yao wanaokosea...
Salaam nyingi za upendo kwenu.
Wazazi na Walezi, tunapoelekea kwenye siku ya familia duniani tarehe 15 Mei, 2024, tafadhali tuanze ukurasa mpya wa kuwa karibu zaidi na watoto wetu. Zawadi iliyo bora zaidi kwa mtoto wako kwenye nyakati za Dunia ya leo, ni kuwa karibu naye, tena karibu zaidi...
Wasaalam mpendwa katika JMT 🇹🇿.
Huenda mimi na wewe hatukuwepo wakati Muungano wa 🇹🇿 ulipozaliwa, ila leo tumepata Neema ya kuwepo unapotimiza miaka 60. Tumeingia kwenye historia hii kubwa.
Nami nimefika mapema Sana Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kujumuika kuadhimisha, kusikiliza na kuelimika...
Wasaalam Wana Jukwaa wote.
Tunaelekea Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Familia hapo Mei 15, 2024 ambapo, nchi yetu tutaungana na zingine duniani kuadhimisha.
Familia ni chanzo cha jamii yetu hivyo, ni kiungo muhimu sana kwa maendeleo na ustawi wa jamii. Malezi bora kwa watoto ndani ya...
Wasaalam Wana Jukwaa wote.
Kwa aliyebarikiwa neema ya Kulea watoto kwa malezi ya kambo au kumuasili kisheria awe wake;
UTARATIBU;
Baada ya kuwasilisha maombi Halmashauri;
1. Afisa Ustawi wa Jamii atakutembelea na kufanya tathmini.
2. Taarifa itawasilishwa kwa Kamishna wa Ustawi wa Jamii...
Salaam nyingi za za upendo kwenu wote.
Aprili 12, kila mwaka ni Siku ya Mtoto wa Mtaani Duniani.
Kaulimbiu Mwaka huu ni ‘TUWAJIBIKE’.
Uwajibikaji uanze ngazi ya familia kwa wazazi/ walezi kutimiza jukumu la kulea. Sheria ya Mtoto Sura ya 13 kifungu cha 6 – 13, kila Mlezi/ Mzazi anawajibika...
Familia ya Advocate Gwajima, tunawashukuru Watanzania Wote kwa upendo na faraja kipindi chote cha kuuguza hadi msiba wa mama mzazi wa Advocate Gwajima (mume wangu) aliyejulikana kama SOPHIA GWAJIMA (mama mkwe wangu) na aliyezaliwa mwaka 1945 na kufariki tarehe 27 Machi, 2024 katika Hospitali ya...
Imetolewa taarifa hapa Jf hoja mchanganyiko na anayejitambulisha kama Anonymous kuwa: mtajwa hapo juu sikumsikiliza alipokuja mara ya pili kwamba amekwama kwenye mfumo wa huduma dawati la jinsia.
Kwanza napongeza watoa taarifa za kijamii pale penye changamoto za kijamii ambazo, zimekwama hatua...
Hivi ndivyo ilivyokuwa kwenye maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 8 Machi, 2024 Dodoma, Chamwino ambako pia TUMEZINDUA SERA MPYA ya Taifa ya Jinsia na Maendeleo ya Wanawake ya Mwaka 2023 mbadala wa ile ya mwaka 2000.
Sera hii ya Mwaka 2023 imezingatia maeneo mapya kadhaa (tutaendelea...
Mhe. Rais, naungana na Wataalamu na Makundi yote ya Kijamii chini ya Wizara hii ya Jamii kukutakia Heri ya Siku ya Kuzaliwa. Tunakutakia Afya njema na Mafanikio tele katika utumishi wako kwa Taifa la Tanzania.
Mwenyezi Mungu awe pamoja nawe daima.🙏🏾
Ndugu wana Jukwaa la JF; Wasaalam.
Tafadhali pokeeni taarifa kuhusu Siku ya Mwanamke anayeishi Kijijini 15 OKT, 2023. Kila mkoa utafanya kwa utaratibu wake ngazi zote za mamlaka yake. Sisi Wizara ya Jamii tutaungana na Mkoa wa Arusha, Kijiji cha Levelousi, Arumeru.
HISTORIA; Azimio la Umoja wa...
Ndugu Wanajukwaa, nawasalimu kwa Jina la JMT.
Kwa heshima tafadhali pokeeni ujumbe huu wa Wizara yenu ya Jamii, Ili twende Pamoja kwa Maendeleo na Ustawi wa Jamii.
Kesho 9 hadi 11 Okt 2023 tunaanza Mkutano wa Kimataifa wa kutokomeza Ukeketaji.
1. Mkutano huu utaenda sambamba na Maadhimisho ya...
Link hii hapa, karibuni[emoji847]
https://youtube.com/live/MhZaCP3E9GA?si=FvE9aTPWw7MPBWaj
==========
DKT. DOROTHY GWAJIMA, WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM
Jukwaa hili kitaifa ni la tatu, ambapo la kwanza lilikuwa ni mwaka 2021 na Mgeni Rasmi alikuwa Rais wa...
TAARIFA KWA UMMA (Rejea Kiambatisho).
Wasaalam Wana Jukwaa.
Nimeambatisha taarifa kwa umma kuhusu siku ya Wazee kitaifa mkoani Geita, tarehe 6 Oktoba, 2023. Viwanja isomeke KALANGALALA na siyo Kahangalala, my apologies, naomba radhi🙏🏽🤝
Fuatana nasi tafadhali kwenye tamko hili na kwenye siku...
Wapendwa Wana JF Salaam.
Awali ya yote, NAWAPONGEZA SANA wote ambao wanaunga mkono kwa Kila mbinu katika mapambano dhidi ya UKATILI Wa KIJINSIA na kwa WATOTO. AHSANTENI SANA 🙏🏽🤝
Hata hivyo, TAFADHALI hii tusikilize hii Video hapa iliyoambatishwa, tuulize maswali na tutoe maoni. Waziri wenu wa...
Ndugu Wananchi, nawasalimu kwa Jina la JMT[emoji1241]
Nimekuwa nikipokea taarifa kutoka kwa baadhi ya wanajamii kuwa zipo changamoto na usumbufu ambao ni mtihani sana kupata huduma za mtoto wa kumlea malezi ya Kambo au Kuasili kiasi kwamba, eti baadhi wenye sifa na vibali wanakata tamaa huku...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.