Siku ya Familia 15 Mei Yaja

Dkt. Gwajima D

JF-Expert Member
Nov 28, 2015
550
3,619
IMG-20240419-WA0003.jpg
Wasaalam Wana Jukwaa wote.

Tunaelekea Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Familia hapo Mei 15, 2024 ambapo, nchi yetu tutaungana na zingine duniani kuadhimisha.

Familia ni chanzo cha jamii yetu hivyo, ni kiungo muhimu sana kwa maendeleo na ustawi wa jamii. Malezi bora kwa watoto ndani ya familia ni chanzo cha jamii iliyo njema na yenye Baraka.

Lengo la maadhimisho ni kutathmini nafasi ya familia katika ustawi na maendeleo yao na mchango wao kwa taifa.

Mwaka 2024 maadhimisho yatafanyika kimikoa kwa kugusa ngazi ya jamii yaani Vijiji, Mitaa na Kata.

Changamoto za mifarakano katika familia imesababisha malezi duni na uangalizi hafifu wa watoto na matokeo hasi kwenye maendeleo na ustawi wa watoto mfano wa kike kuanza ngono katika umri mdogo na kupata mimba za utotoni. Wa kiume nao hujiingiza kwenye tabia hatarishi na kushindwa kutimiza ndoto zao.

Julai, 2023 hadi Aprili, 2024 jumla ya mashauri 14,600 ya kifamilia yaliripotiwa yakiwemo ya migogoro ya ndoa 5,306 (36%), migogoro ya matunzo ya Watoto 5,944 (41%) na ya matunzo ya watoto wa nje ya ndoa 3,350 (23%).

Aidha, kati ya hayo, jumla mashauri 3,411 yalifikishwa ustawi wa jamii na kufanyiwa kazi ambapo, 1,642 (48%) yalipatiwa ufumbuzi na 443 yanaendelea kufanyiwa kazi. Yaliyopata rufaa kwenda mahakamani ni 921 na yaliyosalia 405 yalikabidhiwa kwenye mabaraza ya Kata na Mabaraza ya Jumuiya.

Hakika Maafisa Ustawi wa Jamii wameendelea kufanya kazi kubwa kuhusu utengamao wa familia. TUWAPONGEZE 🙋

Wito kwa viongozi wa Dini kutumia vipindi vya ibada kutoa ujumbe mahsusi kuhusu umuhimu wa malezi bora ya watoto katika kujenga familia imara na Taifa imara la Tanzania.

Wito kwa Wakuu wa Mikoa kupitia watendaji kuratibu elimu ya malezi chanya kwa watoto na wazazi au walezi ngazi za Jamii.

Kaulimbiu ya maadhimisho hayo mwaka huu ni "Tukubali Tofauti Zetu kwenye Familia; Kuimarisha Malezi ya Watoto."

.... kwa taarifa zaidi tafadhali karibu utembelee kurasa mbalimbali za wizara ya maendeleoyajamii online

Heri ya Siku ya Familia, jiandae, adhimisha kwa furaha wewe na familia yako 🙋🇹🇿

 
Mheshimiwa sisi tunaopigwa na wake zetu tukienda ustawi wa jamii au dawati la jinsia mnaegemea upande wa mwanamke zaidi kwanini?

Hizi kesi nimeziona mara nyingi sana..

Mnamkingia kifua mwanamke zaidi badala ya kuleta suluhu ili Familia iendelee kuwa na Amani
 
Mheshimiwa sisi tunaopigwa na wake zetu tukienda ustawi wa jamii au dawati la jinsia mnaegemea upande wa mwanamke zaidi kwanini?

Hizi kesi nimeziona mara nyingi sana..

Mnamkingia kifua mwanamke zaidi badala ya kuleta suluhu ili Familia iendelee kuwa na Amani
Habari za asubuhi. Pole Sana kwa kadhia hii. Umeziona mara nyingi je ngapi umetuletea tufanye review ndugu yangu? Tumetangaza call center yetu hadi namba zangu binafsi unatuma ujumbe. Hebu Leo lete sasa tufanye review tuone nani huyo anakiuka huduma kwa usawa. Shukrani
 
Habari za asubuhi. Pole Sana kwa kadhia hii. Umeziona mara nyingi je ngapi umetuletea tufanye review ndugu yangu? Tumetangaza call center yetu hadi namba zangu binafsi unatuma ujumbe. Hebu Leo lete sasa tufanye review tuone nani huyo anakiuka huduma kwa usawa. Shukrani
Sijawahi kuipenda CCM ila bado kuna watu wachache wazuri ndani yake,wewe ni mmoja wapo...hongera saana mama endeleza mapambano kusaidia jamii yetu
 
Mama hongera sana kwa kazi zako, nimeona kesi nyingi unafatilia na kuzitolea ufafanuzi.... Tunahitaji viongozi wanaotatua kero za wananchi maana sisi ndo waajiri wenu
 
Napenda unavyowasiliana moja kwa moja na wananchi kujua kero zao. Kula 5 mheshimiwa. Nakubali sana.
Ngoja tumshauri mama akikaa na viongozi wenzake canteen za bunge awashauri waache porojo za kusifia Sifia wajikite kwenye kutatua matatizo ya wananchi😃
 
View attachment 2967880Wasaalam Wana Jukwaa wote.

Tunaelekea Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Familia hapo Mei 15, 2024 ambapo, nchi yetu tutaungana na zingine duniani kuadhimisha.

Familia ni chanzo cha jamii yetu hivyo, ni kiungo muhimu sana kwa maendeleo na ustawi wa jamii. Malezi bora kwa watoto ndani ya familia ni chanzo cha jamii iliyo njema na yenye Baraka.

Lengo la maadhimisho ni kutathmini nafasi ya familia katika ustawi na maendeleo yao na mchango wao kwa taifa.

Mwaka 2024 maadhimisho yatafanyika kimikoa kwa kugusa ngazi ya jamii yaani Vijiji, Mitaa na Kata.

Changamoto za mifarakano katika familia imesababisha malezi duni na uangalizi hafifu wa watoto na matokeo hasi kwenye maendeleo na ustawi wa watoto mfano wa kike kuanza ngono katika umri mdogo na kupata mimba za utotoni. Wa kiume nao hujiingiza kwenye tabia hatarishi na kushindwa kutimiza ndoto zao.

Julai, 2023 hadi Aprili, 2024 jumla ya mashauri 14,600 ya kifamilia yaliripotiwa yakiwemo ya migogoro ya ndoa 5,306 (36%), migogoro ya matunzo ya Watoto 5,944 (41%) na ya matunzo ya watoto wa nje ya ndoa 3,350 (23%).

Aidha, kati ya hayo, jumla mashauri 3,411 yalifikishwa ustawi wa jamii na kufanyiwa kazi ambapo, 1,642 (48%) yalipatiwa ufumbuzi na 443 yanaendelea kufanyiwa kazi. Yaliyopata rufaa kwenda mahakamani ni 921 na yaliyosalia 405 yalikabidhiwa kwenye mabaraza ya Kata na Mabaraza ya Jumuiya.

Hakika Maafisa Ustawi wa Jamii wameendelea kufanya kazi kubwa kuhusu utengamao wa familia. TUWAPONGEZE 🙋

Wito kwa viongozi wa Dini kutumia vipindi vya ibada kutoa ujumbe mahsusi kuhusu umuhimu wa malezi bora ya watoto katika kujenga familia imara na Taifa imara la Tanzania.

Wito kwa Wakuu wa Mikoa kupitia watendaji kuratibu elimu ya malezi chanya kwa watoto na wazazi au walezi ngazi za Jamii.

Kaulimbiu ya maadhimisho hayo mwaka huu ni "Tukubali Tofauti Zetu kwenye Familia; Kuimarisha Malezi ya Watoto."

.... kwa taarifa zaidi tafadhali karibu utembelee kurasa mbalimbali za wizara ya maendeleoyajamii online

Heri ya Siku ya Familia, jiandae, adhimisha kwa furaha wewe na familia yako 🙋🇹🇿
View attachment 2967878
View attachment 2967879
Mh.Imefika wakati sasa sheria itamke wazi na kama haipo itungwe kulinda haki za watoto wa kiume,mana vitendo vya ukatili na ulawiti vinazidi kuongezeka sana ni kama vile jamii imemtazama sana bint wa kike na kumsahau mtoto wa kiume.
 
Mh hongera,huwa ukipata jambo la kushughulikia huwa unatekeleza kwa haraka nakupongeza kwa hilo_Ongeza juhudi zaidi kwani matatizo bado yapo.
 
Mheshimiwa Gwajima,hongera sana kwa namna unavyojitahidi kutekeza majukumu yako. Una ukaribu mkubwa na wananchi na unatatua changamoto nyingi zinazowasilishwa kwako kupitia mitandao ya kijamii.
Mungu akutie nguvu uendelee na ari hiyo ya kazi
 
Back
Top Bottom