JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Miaka ya hivi karibuni, matumizi ya dawa za uzazi wa mpango (Vidonge na Sindano) yameongezeka sana, hali inayozua wasiwasi wa usalama wake miongoni mwa watumiaji. Baadhi wameonesha wasiwasi wao kuwa dawa hizi husababisha kupata watoto wa kiume wenye homoni nyingi za kike, au hata kupata watoto wa kike wenye kiasi kikubwa cha homoni za kike hivyo kuwafanya wakomae mapema kabla ya umri sahihi. Mathalani, mdau mmoja wa JamiiForums.com amekiri kuwahi kusikia kuwa matumizi ya muda mrefu ya dawa hizi yanaweza kusababisha mama kupata binti ambaye akifikisha umri wa miaka 8 matiti yake yanaweza kuwa makubwa, yaliyolala. Ukweli kuhusu athari za dawa hizi ukoje?
Mdau wa JamiiForums amedai kuwa jamii za wafugaji ni warefu kwasababu wanakunywa sana maziwa tofauti na jamii za watu wasiotumia maziwa. Amebainisha baadhi ya sababu ni kutokana na maziwa kuwa na madini ya calcium na vitamini D ambavyo husaidia kutengeza na kuimarisha mifupa. Kinyume chake kwa jamii za wakulima ambazo hazitumii sana maziwa huwa wanakuwa wafupi. Jambo hili lina ukweli kiasi gani?
Matumizi ya muda mrefu ya mafuta ya nywele aina ya body luxe (body luxe hair oil) husababisha mvi kuota kwa kasi katika umri mdogo. Hapa nazungumzia haya mafuta ya nywele ya body luxe yenye kopo la pink lenye picha ya mwanamke ana nywele ndefu. Picha: Muonekano wa chupa za mafuta ya Body Luxe kwa upande wa mbele Picha: Chupa ya mafuta ya Body Luxe ikionesha sehemu ya Viambato (Ingredients) Hii ni kutokana na uzoefu wangu (personal experience) kwangu mwenyewe, kaka yangu na jamaa mwingine ambaye tunaishi naye mtaa mmoja. Wote tumeota mvi katika umri mdogo na tumekuja kugundua shida ni haya mafuta. Mimi nilikuwa sijajua, nimeambiwa na kaka yangu jana kuwa mafuta ya nywele yanasababisha kuota mvi, nilioomuuliza alikuwa anatumia...
Back
Top Bottom