Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,690
- 29,909
Hakika haki ya kweli ipo Mbinguni🤣Binti (Miaka 19) yupo kwa Basi, anatoka zake Dar kwenda Uyulo-Mbeya kumsalimu Shangazi yake, anawasiliana nae kwa Simu akiwa safari, lakini anafika Iringa Simu inakata Chaji.
Binti anamuomba Simu Jamaa aliyekaa pembeni yake aitwaye MAPINDUZI NGALLA, lakini anapiga Simu Shangazi hapatikani. Jamaa anamchombeza Binti kwani unaenda wapi?
Binti anajibu Uyole-Mbeya,
Jamaa anamwambia mmh! pale Uyole usiku kuna wauaji, twende ukalale kwangu Mbalali kisha kesho utamalizia safari yako, Binti anamuuliza kwako unakaa na Familia?
Jamaa anajibu ndio.Basi Jamaa anamchukua Binti anaenda nae kwake kijiji cha URUNDA- Mbarali, , kumbe Jamaa anakaa peke yake, wanalala chumba tofauti, lakini usiku Jamaa anaenda chumbani kwa Binti, anadai penzi, Binti anakataa lakini Jamaa ana force kingi - anambaka Binti, kesho inafika Jamaa anamfungia Binti ndani, usiku anambaka tena, kesho yake Jamaa anasahau kufunga mlango Binti anafanikiwa kutoka ndani, baadae Jamaa anakamatwa kwa ubakaji.Jamaa ameshinda kesi. Unajua kwanini? Kifungu -130(1)(2)(b)- ambacho alishtakiwa nacho kinaelezea ubakaji ambao Mwanamke anakubali kufanya mapenzi lakini kukubali kwake kunatokana na kutishiwa kuuliwa, kuumizwa... lakini hii kesi ushahidi wa Binti ulikuwa kwamba alilazimishwa kufanya mapenzi bila ridhaa (consent) yake, hii kitu inaangukia kifungu kingine tofauti -130(1)(2)(a) cha Kanuni ya Adhabu.
Mahakama ya Rufaa chini ya Jaji MASHAKA imemuachia jamaa aliyekuwa amefungwa miaka 30 na mahakama kuu.
Jaji :- Mashaka
Wakili wa Serikali 1 .Edgar Luoga.
2. Devise Msanga.
Nani alaumiwe?
shangazi aliyepotea hewani. Mapinduzi[mbakaji]? Binti[Tunda]? Mawakili wa Serikali waliokosea vifungu vya sheria? Mungu aliyeshindwa kumfanya jama adindishe? Serikali inayosajili mawakili chini ya viwango?