Zaidi Ya Watumishi Hewa 17,100 Wafukuzwa Serikalini

Jamani naombeni msaada au ufafanuzi nini maana ya hewa au watumishi hewa? Maana nijuavyo mimi ni kwamba unaposema watumishi hewa maana yake ni wafanyakazi ambao hawapo kazini kiuhalisia lakini mishahara na stahiki zingine zimekuwa bado zinatolewa ama wanachukua wao au wajanja wachache.

Tunaposema watumishi hewa wamefukuzwa kazini nashidwa kuelewa maana yake. Maana mimi kwa uelewa wangu unaposema watumishi hewa maana yake hawapo kazini. Msaada jamani
 
Hii idadi uliyoionyesha hapa mbona ni kubwa, au hawa viongozi wanaficha idadi halisi
Ndio maana tukamwambia mleta uzi aandike vizuri, inaonekana alikosea figure.
Lakini hata 17,000 lakini bado tunaambiwa matumizi katika ujira yameongezeka!
 
Nikitegemea kichwa kiwe "zaidi ya watumishi 17100 waliokuwa wanapokea mishahara ya wanaodaiwa wafanyakazi hewa wamefukuza"
 
Katika ya sinema bora awamu hii ni "Watumishi Hewa" maana serikali imepata sababu ya kujitetea na kila kikao lazima wataje figure tofauti maana kaka yao ana idadi yake na wadogo zake wana idadi yao na siku wakijichanganya kusema sinema imeisha hakika wafanyakazi wataanzisha sinema yao hapo ndipo patachimbika...Alhamdullilah kura yangu inanifariji mpaka leo kua sikufanya makosa hata kama maumivu kwa wote.
 
Amesema kuwa zoezi la uhakiki lililoanza march hadi september mwaka 2016 limebaini watumishi hewa 17100 limeisababishia hasara serikali kubwa pia waziri simbachawe amekili kuwa zoezi la uhakiki wa watumishi hewa limechelewesha ajira mpya kwa kiasi kikubwa

======

Serikali imewabaini na kuwafukuza zaidi ya watumishi hewa 17100 katika kipindi cha miezi sita huku watumishi hao wakitajwa kunufaika na fursa mbalimbali ikiwemo kupata mikopo kwa njia zisizo za halali na kulisababishia taifa hasara kubwa.

Waziri wa nchi ofisi ya rais Menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora Mhe Angela Kairuki anatoa takwimu hizo za watumishi hewa katika hafla ya kuwaapisha wakurugenzi wapya wa halmashauri 13 walioteuliwa na rais John Magufuli hivi karibuni ambapo amesema kwa kipindi cha mwezi March hadi September idadi hiyo imebainika huku zoezi hilo likitajwa kuwa endelevu.

Kwa upande wake waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa Mhe George Simbachawene amesema kubainika kuwepo kwa watumishi hewa kumechangia kwa kiasi kikubwa kuchelewesha ajira mpya huku akionya baadhi ya watu wanaotumia vibaya mitandao ya kijamii kupotosha umma kuhusu ajira waache mara moja kabla hawajachukuliwa hatua

Nao baadhi ya wakurugenzi hao wapya baada ya kula kiapo cha maadili ya viongozi wa umma wamesema wamepokea uteuzi huo na wako tayari kufanya kazi kwa kuzingatia maagizo ya rais katika maeneo yao.


Chanzo: ITV
Jamani hata Kiswahili kumbe ni kigumu namna hii?
Unaposema Wafanyakazi Hewa maana yake ni kuwa hao wafanyakazi hawapo ni wakubuni tu. Kuna watu walibuni kua kuna wafanyakazi hao na Pesa za mishahara zilikuwa zinaingia mifukoni mwa watu hao wachache.
Leo anapotokea waziri akasema wafanyakazi 17100 hewa wamewafukuza kazi wamewafukuza vipi wakati hawapo?
Wasitudanganye, watueleze ni akina nani walikuwa wanafanya vitendo hivyo vya udanganyifu mpaka serikali ikaingia hasara kiasi hicho?
Pili watueleze wamechukuliwa hatua gani za kisheria?
 
Amesema kuwa zoezi la uhakiki lililoanza march hadi september mwaka 2016 limebaini watumishi hewa 17100 limeisababishia hasara serikali kubwa pia waziri simbachawe amekili kuwa zoezi la uhakiki wa watumishi hewa limechelewesha ajira mpya kwa kiasi kikubwa

======

Serikali imewabaini na kuwafukuza zaidi ya watumishi hewa 17100 katika kipindi cha miezi sita huku watumishi hao wakitajwa kunufaika na fursa mbalimbali ikiwemo kupata mikopo kwa njia zisizo za halali na kulisababishia taifa hasara kubwa.

Waziri wa nchi ofisi ya rais Menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora Mhe Angela Kairuki anatoa takwimu hizo za watumishi hewa katika hafla ya kuwaapisha wakurugenzi wapya wa halmashauri 13 walioteuliwa na rais John Magufuli hivi karibuni ambapo amesema kwa kipindi cha mwezi March hadi September idadi hiyo imebainika huku zoezi hilo likitajwa kuwa endelevu.

Kwa upande wake waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa Mhe George Simbachawene amesema kubainika kuwepo kwa watumishi hewa kumechangia kwa kiasi kikubwa kuchelewesha ajira mpya huku akionya baadhi ya watu wanaotumia vibaya mitandao ya kijamii kupotosha umma kuhusu ajira waache mara moja kabla hawajachukuliwa hatua

Nao baadhi ya wakurugenzi hao wapya baada ya kula kiapo cha maadili ya viongozi wa umma wamesema wamepokea uteuzi huo na wako tayari kufanya kazi kwa kuzingatia maagizo ya rais katika maeneo yao.


Chanzo: ITV
Mmm mbona kwenye majeshi bado?
 
kwenye vyombo vyetu vya ulinzi hakuna? basi huko safi sana wapo makini sana hongereni
 
Serikali ya Jk wala na siasa za watumishi hewa ili kukosesha ajira vijana huku mawaziri wakila keki ya Taifa.

Rais Magufuli ni muda muafaka sasa uajiri vijana wako, nao waone matunda ya elimu zao na uongozi wao.


Uhakiki wa watumishi hewa, uendelee huku vijana wakiwa kazini
 
Halafu kama kweli idadi ya waliofukuzwa ni hiyo iliyotajwa mbona malipo ya mishahara imeongezeka? Kuna nini hapa
 
Back
Top Bottom