Waziri Jerry Silaa ana kitu, atafika mbali, abarikiwe

Salaam, Shalom!!

Nimefuatilia Kwa ukaribu jinsi waziri Jerry Slaa anavyofanya katika utatuzi wa migogoro ya ardhi, japo Bado ni mapema sana kusema kuwa anafanya vizuri, lakini Kwa sasa itoshe kusema ana kitu kinachoonekana, na atafika mbali, tuendelee kumwombea.

Nimesikiliza Kwa Umakini jinsi alovyotatua case ya Tajiri aitwaye Mzee Mmassy aliyenunua nyumba Kwa marehemu aliyeko kaburini, yaani document zinaonyesha marehemu akiwa kaburini alisaini mauziano na kumuuzia nyumba tajiri Mmassy,na jinsi alivyotatua case Ile Kwa uwazi Kwa kutumia nyaraka halali katika ofisi ya ardhi, na jinsi alivyoweza kuwarudishia nyumba watoto na mke wa marehemu nyumba Yao, kiukweli Mungu aendelee kumjalia uhai na AFYA na baraka kiongozi huyu.

Nilifanikiwa pia kufuatilia jinsi alivyosaidia kutatua mgogoro ulioletwa na Msama, Kwa kutomtendea HAKI yake mama yule aliyedai kiwanja chake, pia nimeona ufuatiliaji, uthubutu na uchapakazi wa Waziri huyu kijana Jerry Slaa.

Ni maombi yangu, akae chini na viongozi wenzie katika wizara yake na kuja na mpango MIKAKATI wa kutatua migogoro ya ardhi Nchi nzima bila kuwepo haja ya kusafiri huku na huko, uwepo mfumo mzuri na WA haraka zaidi kuwafikia wananchi na kutatua migogoro hiyo ya ardhi.

So far, KAZI imeonekana inafanyika,

Mungu Mbariki Waziri huyu Jerry Slaa,

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Ameeen.

Source: Milard Ayo tv.

Karibuni🙏
Hatari yake ipo huko huko ofisini kwake; na atakapokanyaga waya zinazogusa wateuzi wake, habari yake hutaisikia tena.

Naungana nawe katika kumtakia mafanikio. Wizara hiyo ni ngumu sana; lakini kijana anapambana vizuri sana kwa sasa.
 
Huyo hamna kitu, ana-deal na kiki ambazo akikutana na mbabe anakwama, yaani uje mtaani umtoe mtu kwenye nyumba, hiyo ni kazi yako kama waziri? Anatafuta yale yaliyomkuta Mwamwindi wa Iringa.

Wizara ina mambo makubwa ya kisera ya kufanya, hayafanyii kazi.

Kuna tatizo kubwa la utawala wq ardhi (land administration) hasa kwa kuwa asilimia kubwa ya nchi yetu haijapimwa. Sheria ya ardhi namba 4/1999 inajishughulisha na ardhi yenye hati, lakini wangapi mjini wqna hati? Wale wasio na hati wanakuwa regulated vipi? Wizara imetoa muongozo kwa uhamishaji wa miliki ambazo hazina hati?

Wizara ina mpango gani kuunga mifumo ya kibenki na usajili wa ndoa ili mali za dhamana wakopeshaji wajue hali ya mkopaji?

Kulikuwa na mradi wa hati za kidigitali, umekwama wapi?

Benki ya dunia walitoa bilioni 350 kufadhili mradi wa wizara ya ardhi ambao unajumuisha ujenzi wa majengo ya taasisi za ardhi kila mkoa, mbona bajeti inaisha, majengo hayapo? Na hata vifaa walivyosema watanunua kwa ajili ya kila mkoa ili kupima ardhi havipo? Hizo hela zimeenda wapi?

Mamlaka zinapoingiza vijiji mjini, wizara imetoa muongozo kuhusu ardhi iliyokuwa ya vijiji? Kuna namna au mfumo wa vijiji kukabidhi ardhi kwa Halmashauri? Au ndio inaachwa kwa viongozi wa mitaa mipya wajiuzie wanavyotaka?

Hatumuoni katika migogoro ya hifadhi za taifa na wananchi, anazurura mijini tu. Kapima vijiji vingapi mwaka huu? Amegawa hati za kimila ngapi?

He is just a petty politician ambaye alitakiwa ajenge josho ili kuosha wanyama kwq maelfu, yeye kaamua kuchambua manyoya ya mnyama mmoja mmoja ili awe anatoa kupe
Pumba tupu umeandika!!
 
Kiongozi anajenga mifumo, hakuna mfumo aliojenga mpaka sasa, angekuwa na mfumo, asingekuwa na haja ya kutembea mpaka vyumbani mwa watu.

and land justice, kama ilivyo haki yoyote ile, huwezi kuifanya kwa mfumo wa mob justice, unakusanya vijitu mtaani, unasikiliza unaamua, hakuna due process halali ya kisheria ambayo itafanya haki ionekane inatendeka. Kuna mahala atakutana na jambo, yeye binafsi atadhalilika, na serikali itadhalilika.
Poyoyoo wwe! Hujui ulisemalo kaa kimya!!
 
Yaani ni hopeless kabisa.katika viongozi wa hovyo tulio nao huyu jamaa ni namba moja.
Hajiamini kabisa.anatumia jeshi la polisi kutisha watu.
Sijui kwa nini raisi anaendelea na huyu jamaa. Kamuabisha shehe kariakoo. Hata sheria za wakfu hazifahamu.
Tanganyika law society, tume ya haki za binadamu, mwanasheria mkuu pamoja na mahakama wanatakiwa watoe tamko kukemea huu ujinga
Wwe lazima utakua wakili wa mchongo,na unae ishi kwa kesi za.Mchongo, nyinyi ndiyo kina mzee.mmasi mkisha zulumu.mnakimbilia Mahakamani ili kuhalalisha zuluma zenu!
 
Wwe lazima utakua wakili wa mchongo,na unae ishi kwa kesi za.Mchongo, nyinyi ndiyo kina mzee.mmasi mkisha zulumu.mnakimbilia Mahakamani ili kuhalalisha zuluma zenu

Wwe lazima utakua wakili wa mchongo,na unae ishi kwa kesi za.Mchongo, nyinyi ndiyo kina mzee.mmasi mkisha zulumu.mnakimbilia Mahakamani ili kuhalalisha zuluma zenu!
We choko nini...kafie mbali huko
 
Nikaona kuwa kuomba Mmassy ana experience ya kuhonga mawaziri Ili wapotoe HAKI.

Nchi hii tunawahitaji viongozi waliookoka Kweli Kweli wenye HOFU ya Mungu bila kujali vyama vya siasa watokako.
Ee Mwenyezi Mungu endelea kumbariki na kumlinda Mhe. Jerry Slaa, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi kwa kazi kubwa ya kumsaidia kazi Rais wa JMT.

Asante sana kwa utendaji kazi uliotukuka katika kipindi kifupi tu baada ya kuteuliwa kuiongoza Wizara ya Ardhi.

Mfano hai ni Mama mjane wa Mjini Tanga aliyehangaishwa na mpangaji katika nyumba kwa miaka mingi mara baada ya mumewe kufariki dunia akitaka kumdhulumu mali halali waliyokuwa wanaimiliki na marehemu mumewe wakati wa uhai wake.

Ndugu zangu haki ya mtu haipotei, ndipo Serikali ya JMT kupitia Waziri mwenye dhamana ameagiza mama mjane arejeshewe nyumba yake mara moja baada ya Mhe. Waziri kukagua hati za umiliki wa ardhi na kujiridhisha kuwa nyumba ni mali halali ya mama mjane.

Wote twapaswa kuwa na hofu ya MUNGU hivyo tukumbuke na kuzingatia kuwa haki huinua Taifa bali dhuluma ni aibu kwa watu wote !
 
Nenda kasome Hukumu ya Mahakama Kuu ndiyo utajua issue ni jinai au siyo junai!!
Katika hao wote waliokamatwa mpaka sasa hivi ni yupi aliyefikishwa mahakamani?
Au anataka awapeleke jela moja kwa moja. Kwa sababu anaogopa akiwapeleka mahakamani watahonga majaji washinde kesi.
Yaani sijui watanzania ni nani katuloga..nahisi tulipata uhuru mapema sana..namlaumu chief mariale kwa nini aliacha kuendelea kudai uhuru wa kaskazini kwetu...huenda sasa hivi tungekuwa mbali sana.hili lichama la waswahili wa kariakoo linatuangusha sana
 
Huyo hamna kitu, ana-deal na kiki ambazo akikutana na mbabe anakwama, yaani uje mtaani umtoe mtu kwenye nyumba, hiyo ni kazi yako kama waziri? Anatafuta yale yaliyomkuta Mwamwindi wa Iringa.

Wizara ina mambo makubwa ya kisera ya kufanya, hayafanyii kazi.

Kuna tatizo kubwa la utawala wq ardhi (land administration) hasa kwa kuwa asilimia kubwa ya nchi yetu haijapimwa. Sheria ya ardhi namba 4/1999 inajishughulisha na ardhi yenye hati, lakini wangapi mjini wqna hati? Wale wasio na hati wanakuwa regulated vipi? Wizara imetoa muongozo kwa uhamishaji wa miliki ambazo hazina hati?

Wizara ina mpango gani kuunga mifumo ya kibenki na usajili wa ndoa ili mali za dhamana wakopeshaji wajue hali ya mkopaji?

Kulikuwa na mradi wa hati za kidigitali, umekwama wapi?

Benki ya dunia walitoa bilioni 350 kufadhili mradi wa wizara ya ardhi ambao unajumuisha ujenzi wa majengo ya taasisi za ardhi kila mkoa, mbona bajeti inaisha, majengo hayapo? Na hata vifaa walivyosema watanunua kwa ajili ya kila mkoa ili kupima ardhi havipo? Hizo hela zimeenda wapi?

Mamlaka zinapoingiza vijiji mjini, wizara imetoa muongozo kuhusu ardhi iliyokuwa ya vijiji? Kuna namna au mfumo wa vijiji kukabidhi ardhi kwa Halmashauri? Au ndio inaachwa kwa viongozi wa mitaa mipya wajiuzie wanavyotaka?

Hatumuoni katika migogoro ya hifadhi za taifa na wananchi, anazurura mijini tu. Kapima vijiji vingapi mwaka huu? Amegawa hati za kimila ngapi?

He is just a petty politician ambaye alitakiwa ajenge josho ili kuosha wanyama kwq maelfu, yeye kaamua kuchambua manyoya ya mnyama mmoja mmoja ili awe anatoa kupe
kweli binadamu hana shukrani,hata ukimbeba mgongoni na kumlisha atakutukana tu..
 
Mahakamani zinafanywa analysis nyingi kabla ya hukumu, huyo Silaa anayekaa vichochoroni usiku ana muda wa kutoshaha kufanya hivyo, kama jamaa aliingia kwa nguvu ya mahakama, huyo mama hatamaliza mwezi ndani ya nyumba hiyo, mahakama itamtoa, na Jerry akikoroma ataitwa mahakamani ajieleze kwa nini asifungwe kwa kudharau mahakama.

Mambo ya alikufa lini, kama hakuyasema mahakamani, ni kazi bure kwa sasa

Nvhimbi na Makala wamesema mambo ya Mahakamani yasiingiliwe, yeye anajitoa akili
Subiri siku ukifa wwe ndiyo utajua ukweli wote!!
 
Kama suala liko mahakamani, Silaa ana haki ipi ya kuliingilia? Huo ndio upumbavu nilikuwa nausema.
Slahaa, Msajili wa.Hati pamoja na Commissioner wa Aridhi ndiyo wenye mamlaka na Aridhi na siyo Mahakama, Mahakama yake ni migogoro! Commissioner na Msajili wa Hati ndiyo wenye final say kwenye swala zima la Aridhi kuhusu umiliki wa Aridhi iliopimwa!!
 
Katika hao wote waliokamatwa mpaka sasa hivi ni yupi aliyefikishwa mahakamani?
Au anataka awapeleke jela moja kwa moja. Kwa sababu anaogopa akiwapeleka mahakamani watahonga majaji washinde kesi.
Yaani sijui watanzania ni nani katuloga..nahisi tulipata uhuru mapema sana..namlaumu chief mariale kwa nini aliacha kuendelea kudai uhuru wa kaskazini kwetu...huenda sasa hivi tungekuwa mbali sana.hili lichama la waswahili wa kariakoo linatuangusha sana
Migogoro mingi ya ardhi chanzo ni wizara yake,

Na nafasi ya Waziri na maamuzi yake kupitia vikao na taarifa Ofisini kwake Ina umuhimu mkubwa.

Wengi hukosa HAKI wizara ya ardhi ndipo huenda mahakamani.

Kwa case ya Mmassy, tayari imetatuliwa Kwa 50%, mama yule atatumia utatuzi wa Waziri kama mojawapo ya ushahidi na kupata ushindi.

Si lazima kupinga Kila kitu.
 
Hatari yake ipo huko huko ofisini kwake; na atakapokanyaga waya zinazogusa wateuzi wake, habari yake hutaisikia tena.

Naungana nawe katika kumtakia mafanikio. Wizara hiyo ni ngumu sana; lakini kijana anapambana vizuri sana kwa sasa.
Ni kheri unafanya KAZI miezi SITA Kwa ubora ukafukuzwa kuliko kufanya miaka 5, na kisionekane chochote.

Wananchi tunatunza kumbukumbu Kwa matumizi ya baadae.
 
Back
Top Bottom