Je, kuna siasa katika utatutizi wa migogoro ya ardhi unaofanywa na Jerry Silaa?

Pantosha

JF-Expert Member
Sep 22, 2022
370
500
IMG_5316.jpeg
Mimi ni muumini wa watu wote wabunifu wanaopanga kutatua kero za wananchi.

Waziri Slaa anaonekana kuwa mbunifu baada ya kuja na clinic za kutatua kero za migogoro ya ardhi.

Jana akiwa Mbeya alionekana akitoa maamuzi ya mgogoro wa mtu anayeonekana ni Mchina ambaye kwa mujibu wa Waziri watu waliuza nyumba yake kwa TZS 80,000,000.

1. Yaliyonishangaza ni kuona mgogoro huo unatatuliwa mbele ya camera papo kwa hapo. Niliona anamsikiliza mchina na mmoja wa wapangaji na mtu aliyenunua pamoja na mwenyekiti wa s/mtaa. Huenda keshafuatilia huko nyuma kuusu huo mgogoro. Sina uhakika.

2. Mchina huyo Slaa anamtambulisha kama Muwekezaji. Hivi kuna muwekezaji mgeni ambaye kawekeza kiasi hicho kidogo cha pesa? Sheria ya uwekezaji kwa wegeni hairuhusu.

3. Kama hajakidhi vigezo na si Mtanzania, anamilikije ardhi/nyumba? na si muwekezaji?

4. Je hii haikuwa staged? Sina uhakika na siwezi kutoa conclusion.

Nia ya Waziri ni njema sana. Nashauri asichanganye na siasa za kibongo. Achague tu either kuwa mtendaji au mwanasiasa.
 
Ni muwekezaji wa nini? Usije kuta, amewekeza kuuza vyombo vya udongo huko Mbeya
 
Back
Top Bottom