KERO Walimu Sekondari JM Kikwete ya Tunduma waache kulazimisha Wanafunzi kununua karanga

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Mwalimu MWALUKASA wa Shule ya Sekondari JM KIKWETE, Halmshauri ya Mji Tunduma Mkoani Songwe anayefanyabiashara ya kuuza karanga shuleni analalamikiwa na Wanafunzi kuwalazimisha kununua karanga na kuwachapa viboko wanaoshindwa kufanya hivyo.

Inadaiwa Mwalimu huyo anayefundisha Somo la Kiswahili katika shule hiyo amekuwa akitumia makosa ya Wanafunzi kama mtaji wa Biashara yake.

Inadaiwq kuwa Siku ya Aprili 23, 2024 aliingia katika madarasa ya Kidato cha Kwanza na kuanza kuwaadhibu Wanafunzi wote akidai wamefeli Somo la Kiswahili huku akiwataka kununua karanga ili wapunguziwe adhabu.

Wanafunzi walionunua karanga kuanzia za Sh 300 walisamehewa adhabu na wale walioshindwa walichapwa fimbo kuanzia 10 na kuendelea.

Wakati akitoa adhabu ya viboko kwa ambao walishindwa kununua karanga waliadhibiwa viboko zaidi ya 10 kwani aliwaalika Walimu wenzie wawili akiwemo Mwalimu OBOTE na MALIVA na kutoa adhabu kama ifuatavyo katika madarasa ya Kidato cha Kwanza A na B.

Mwalimu Mwalukasa aliwachapa viboko 7.
Sir Obote 4.
Maliva 3.

Je, ni Sawa Waalimu kufanya biashara Shuleni?
Je, ni sawa Mwanafunzi kuadhibiwa viboko zaidi ya vitatu kwa kosa anauliza Mdau?

Picha kwa msaada wa pronga69.blogspot
Mambo madogo hayo
 
Ni kama tu vile mchungaji anapoamua kula vya madhabauni kaka, na sidhani kma mtoto akisema hana hela huyo mwalimu atalazimisha kuingiza mikono mifukoni kwa mwanafunzi.
 

Mwalimu MWALUKASA wa Shule ya Sekondari JM KIKWETE, Halmshauri ya Mji Tunduma Mkoani Songwe anayefanyabiashara ya kuuza karanga shuleni analalamikiwa na Wanafunzi kuwalazimisha kununua karanga na kuwachapa viboko wanaoshindwa kufanya hivyo.

Inadaiwa Mwalimu huyo anayefundisha Somo la Kiswahili katika shule hiyo amekuwa akitumia makosa ya Wanafunzi kama mtaji wa Biashara yake.

Inadaiwq kuwa Siku ya Aprili 23, 2024 aliingia katika madarasa ya Kidato cha Kwanza na kuanza kuwaadhibu Wanafunzi wote akidai wamefeli Somo la Kiswahili huku akiwataka kununua karanga ili wapunguziwe adhabu.

Wanafunzi walionunua karanga kuanzia za Sh 300 walisamehewa adhabu na wale walioshindwa walichapwa fimbo kuanzia 10 na kuendelea.

Wakati akitoa adhabu ya viboko kwa ambao walishindwa kununua karanga waliadhibiwa viboko zaidi ya 10 kwani aliwaalika Walimu wenzie wawili akiwemo Mwalimu OBOTE na MALIVA na kutoa adhabu kama ifuatavyo katika madarasa ya Kidato cha Kwanza A na B.

Mwalimu Mwalukasa aliwachapa viboko 7.
Sir Obote 4.
Maliva 3.

Je, ni Sawa Waalimu kufanya biashara Shuleni?
Je, ni sawa Mwanafunzi kuadhibiwa viboko zaidi ya vitatu kwa kosa anauliza Mdau?

Picha kwa msaada wa pronga69.blogspot
Mtoa mada unaonekana una tabia za kikuda, majungu na wivu. Na walimu wa aina yako, mara nyingi ni wale wa kupenda sana kujipendekeza kwa Mkuu wa shule, na pia kuwachongelezea walimu wengine ili mfikiriwe kwenye zile fursa za kusimamia na pia kusahihisha mitihani.

Watu wa aina yako mara nyingi huwa mnaishi kwa kutegemea mshahara kwa 100%. Ndiyo mnaoshinda shule kuanzia saa 12 asubuhi mpaka saa 4 usiku! Huwa mnakuwa ni viherehere sana! Na ndiyo mnaosababisha kada ya ualimu idharauliwe hata na watu ambao hawajasoma!!

Ishu kama hii ilikuwa inaishia tu kwenye vikao vyenu vya staff. Wala hukuwa na sababu ya kuja kuileta humu jukwaani.
 
Hiyo ndiyo staili ambayo walimu wanatumia kufikisha ujumbe kwa Serikali!
Kazi ni kwetu sisi wenye watoto!
 
Viboko vinasababisha walimu wanyanyase wanafunzi. Vinatengeneza mazingira mabaya sana. Kuna mwalimu wetu wa shule ya msingi alikuwa anaogopeka sana kwa fimbo, akatumia kuogopeka huko kutaka kumbaka mwanafunzi ofisini.
 
Back
Top Bottom