Nilikuwa naangalia mitandao mbalimbali ya magari ambayo wanaleta magari used hapa Tanzania. Bahati nikapata mtandao ambao umenivutia, una magari yanayoonekana ni mazuri kwa picha, lakini kwa kuwa uelewa wangu juu ya biashara hii ya magari ni mdogo, naomba wenye ufahamu mnisaidie.
Je, Toyota Opa ni gari ambayo haisumbui spares? Je, ina ugonjwa wowote wa kudumu? Wao wamesema Bei ni FOB US$ 2,200/=. Je, mpaka ikifika hapa Dar kwa uzoefu wenu kwa makadirio itanipasa niwe na kiasi cha Tsh ngapi?
Baadhi ya taarifa ni hizi:
- Year / Month2001/12
- Odometer38,000 km
- Displacement1,800 cc
- Steering Right
- Transmission Automatic
- Fuel Gasoline/Petrol
- Model codeTA-ZCT10
Unachopaswa kuzingatia ni bei ya CIF (Cargo In Freight) ambayo huwa tofauti kulingana na mahali gari itakaposhushwa. FOB (Freight On Board) ni bei ya gari KABLA ya kutumwa, maana yake, on Board (tayari kwa kutumwa). Kumbuka FREIGHT na BOARD ni vitu viwili tofauti.
Kwa hiyo unapaswa kupata bei ya CIF Dar es Salaam, kisha uende TRA (inategemea uko wapi), wao ndio watakupa makadirio mazuri zaidi.
Gharama za ushuru hukokotolewa kutokana na Ujazo wa Injini (CC), mwaka ambao gari ilitengenezwa, na kama inatumia mafuta ya dizeli au petroli. Kama umri wa gari ni zaidi ya miaka kumi, kuna ada ya ziada ambayo utatozwa, nadhani ni asilimia 15. Kiwango hiki kimewekwa ili kuepusha magari machakavu kuingizwa nchini. Minimum unapaswa kuwa na gari ambayo imetengenezwa kuanzia mwaka 2000. Ifikapo mwaka 2011, basi, kiwango hiki kinasogea hadi mwaka 2001.
Nakutakia mafanikio mema. Naipenda sana hii gari, kwa hiyo uniambie wapi ulipopewa bei nzuri kama hiyo, na mwisho wake, umelipia jumla ya gharama kiasi gani mpaka ikawa ON THE ROAD! Usiwasikilize watu wanaoongea bila kuwa na uhakika wa wanachokisema.
-> Mwana wa Haki
Cha msingi ndugu ni kusoma reviews za wataalamu kupitia car reviews websites ambapo utapata detailed information kuhusu gari husika na kutoka hata kwa wanaotumia gari ya aina hiyo. Ila elewa kuwa gari yeyotec ni matunzo yako tu japo OPA haifai sana kwa njia zetu za Bongo kwa kuwa ipo chini na bodi yake ni very right.
Toyota Opa -Frist Impressions
Kuhusu gharama halisi, kwa mitandao ya wauza magari unaweza kufanya mahesabu mwenyewe kupitia bei za FOB na unakujua CIF kwa bandari utakayosushia ni ngapi kisha ukaipeleka katika bei za madafu. Kwa mfano ukienda katika mtandao wa Tradecar view.
http://www.tradecarview.com/used_car/japan car/toyota/opa/967478/ AU Japan Partner Toyota OPA Used Cars - Japan Partner - Japan Partner Wanakuonyesha bei halisi CIF na ipo nyingine unapewa kwa madafu ukitaka.
Kuhusu kodi na gharama za utoaji gari bandarini hizo waweza kupata kwa madafu.
Kodi tembelea mtandao wa TRA utapata details zote. Hapa link.
http://www.tra.go.tz/documents/Motor Vehicle Tax Computation.doc
Kutoa gari check na mawakala wa kutoa mizigo (clearing and forwading Agents).
Yard nyingi wanacheza na adometer, yaani gari imetembea 200,000km inarudishwa hadi 70,000km then unauziwa mbuzi kwenye gunia, gari nyingi huwa zimetumika hapa bongo then wamiliki wanazidisplay yard then ikiuzwa wanamlipa commission yule mwenye yard. vile vile gari nyingi huwa zinatoka uarabuni "Dubai" ambako wao sio wazalishaji wa magari, huwa wananunua gari used kutoka Japan au UK, wanaitumia then wana recondition kwa hiyo wewe unakuwa "third hand"
Niliagiza gari zangu Nissan civillian bus mara tatu kupitia kampuni moja ya Japan. kila gari ikifika sikuamini macho yangu kwa jinsi ilivyo nzima. Pia kuagiza gari ni risk sana kama hauna uzoefu. watu wengi wamelia, "sikutanii"
Zaidi ya hapo nakuhakikishia gharama ya kununua hilo gari itakua chini kwa zaidi ya 3 million ukilinganisha na bei za yard.