Grand Canyon
JF-Expert Member
- Jan 2, 2020
- 457
- 927
Majuzi gari langu lilipata shida. Nilianza kupita maduka ya spea kutafuta spea za gari. Nilishangaa kuona taa tu ya baadhi ya magari zianauzwa hadi milioni 1.5. Tena si magari ya bei mbaya kwamba ikiwa alinunua gari milioni 100 hashindwi taa ya 1.5 m. Baadhi ya magari ni ya bei ya kawaida 15-30 m.
Sasa ikitokea taa za mbele zimepata shida na bima ni 3rd part huu ni mtihani .
Gereji nilikuta magari mengi sana. Fundi alinitajia baadhi ya changamoto ya magari hayo. Moja ni Peugeot bado mpya ila ina shida ya sensor, na sensor imetafutwa bila mafanikio. Gari imeanza kupata kutu.
Nilichojifunza:
Unapotaka kununua gari ni vizuri kwanza kujua upatikanaji wa spea na gharama zake la sivyo ikipata shida itatelekezwa gereji.
Sasa ikitokea taa za mbele zimepata shida na bima ni 3rd part huu ni mtihani .
Gereji nilikuta magari mengi sana. Fundi alinitajia baadhi ya changamoto ya magari hayo. Moja ni Peugeot bado mpya ila ina shida ya sensor, na sensor imetafutwa bila mafanikio. Gari imeanza kupata kutu.
Nilichojifunza:
Unapotaka kununua gari ni vizuri kwanza kujua upatikanaji wa spea na gharama zake la sivyo ikipata shida itatelekezwa gereji.