Umeumiza watu halafu unataka kuokoka bila kuwaomba msamaha uliowaumiza, hilo haliwezekani!

Utasikia

fulani alikuwa jambazi hapo zamani kwa sasa kaokoka
Fulani alikuwa tapeli sugu hapo zamani kaamua kuokoka
Fulani alivunja ndoa za wengi hapo zamani kaamua kuokoka

NONSENSE, UJINGA!!

Mnakosea sana, Mnjidanganya, Mambo hayendi hivyo !!



1. TUACHE MASIKHARA KWA MUNGU WA HAKI

Ulikuwa jambazi umeibia watu, wameshindwa kuendelea kwajili yako, Mungu wa haki hawezi kukutakasa bila wewe kupata msamaha wa uliowaibia

Ulikuwa mzinzi, umekuwa chanzo cha ndoa za watu kuvunjika, Mungu wa haki hawezi kukutakasa bila wewe kupata msamaha wa mme / mke uliemvunjia ndoa

Ulikuwa muuaji, umeua baba, familia zinateseka, Mungu wa haki hawezi kukutakasa bila wewe kupata msamaha wa uliewaulia baba

Ulikuwa dhulumati, umedhulumu watu, wanaishi maish ya dhiki, Mungu wa haki hawezi kukutakasa bila wewe kupata msamaha wa uliowadhulumu

2. MIFANO

Baada ya Daudi kushika madaraka nchi ikawa ina majanga, alipomuuliza Mungu nini chanzo, aliambiwa utawala uliopita wa Sauli uliua wana watu wa Gibeon hivyo waende kwao wayamalize,baada ya hapoataitakasa nchi, walipoenda huko wa Gibeon waliwambia wao hawataki dhahabu wala Silver, wanataka kulipiza kisasi, wawape wana wa Sauli wa kiume saba wawaue na walipofanya hivyo nchi ilitakaswa.

Mfano mwingine Yesu mwenyewe aliwaambia wanafunzi wake kwamba kabla ya kutoa sadaka kaweke kwanza mambo sawa na uliowakosea, pia alishauri patana na mshitaki wako kwanza kabla hamjafika kwa hakimu

Mfano mwingine wa zakayo alikumbuka dhambi zake na akasema atawarejeshea mara kumi aliowadhulumu, bda ya hapo ndipo aliweza kupokea wokovu

3. AGANO LA KALE LILIRUHUSU JICHO KWA JICHO, JIPYA JE ?

Agano la kale liliruhusu kulipiza jino kwa jino kama huo mfano wa kwanza wa kulipiza kisasi kwa kuua lakini haimaanishi agano jipya limefuta kila kitu, kilichobadilika ni kwamba mtu aliekukosea akija kukuomba msamaha haupaswi kulipizajino kwa jino, ni aidha umsamehe au kama roho inasita wewe mwambie wazi tu huwezi, hakuna haja ya kulipiza kwa jinsi alivyokuumiza

4. HAIWEZEKANI KUOKOKA BILA KUPATA TIKETI YA MSAMAHA WA ULIOWAUMIZA

Ni hivi, Mungu sio dhalimu,wewe unaweza kukuta umenitendea mabaya halafu unaenda kanisani kuokoka lakin unasahau mimi kila asubuh naamka na majereaha uliyoniachia aidha umeniibia duka nimefirisika, umeua watu wangu wa karibu naumia, umeniibia mke ndoa ilivunjika, umenidhulumu kiwanja sina nyumba, n.k.

Mungu hawezi kusahau uovu ulionifanyia kisa eti umebadilika, unaenda sana kanisani, unatoa sadaka (zikiwemo pesa ulizonidhulumu ), n..k NEVER !!!! Na kuhakikishia Mungu ni wa haki hata sikia sala yako ya kuokoka kama hutotubu maovu yako kwa uliowaumiza, Mungu haongeki !!!


5. MWISHO KABISA

Mwenyezi Mungu anachukizwa mno na dhambi, hakikisha unajizuia sana kutenda dhambi kuumiza wengine na ukifanya hivyo fanya uwezavyo uwaombe msamaha, ndio tiketi pekee ya kuomba msamaha kwa Mungu
Tuache kuhukumiana mungu ni mwingi wa kusamehe binaadamu wana nongwa wengine hawajuu kusamehe hata wakiombwa msamaha, mtu kama ametubu toba ya kweli kwa mungu wake tuna amini amrsamehewa mungu hana roho mbaya kama yako ya kutopenda kusamehe siyo lazima mtu akufuate kuna mazingira mengine hayaruhusu hayo huwezi kuwafuata wote uliyowahibkuwakosea, hakuna binadamu aliyekamilika
 
Unajua maana ya kahaba?
Si kila kahaba ana lengo la kuiba mume, wengine hulazimishwa sio kwa hiari, Pale mwananyamala Kahaba analala na wanaume 20 kwa siku, hana habari yoyote ya kuiba mume wa mtu na wala hawajui wake zao wala hajui kama wana wake.
 
Mungu anaweza kukusamehe dhambi zako binafsi tu zisizodhuru wengine ama ambazo mmeshirikiana watu kwa hiari yenu bila kudhuru, mfano kulewa kivyako, umezini na kahaba, kujichua, n.k.

Hizo dhmbi zingine za kuwaumiza wengine yeye anahusika baada ya kuwaomba msamaha uliowakosea,
Siyo mungu tunaemwabu katika Kristo yesu,dhambi ni dhambi na yesu alisema yote yamkwisha yaan yote ni yote,ila wewe unatakiwa ufaate utaratibu wa kisheria namna ya kuondoa zambi ulizonazo, kiufupi ishu ya daudi ile ilikuwa ni adhabu na ilikuwa kwenye cheo yoyote atakaye tawala lazima alikuwa akutane nayo na baada ya kujulishwa kuhusu adhabu walitumia utaratibu WA kipindi kundoa adhabu iliyokuwepo na ikaondoka, so hata Leo watu wanatembelea adhabu weng tu bila kujua lakin ukisoma bible visuru ukaijua Sheria unaondoa zote,
 
Kwahiyo kama tulitoka ndo tuendelee kuumizana kisa ukienda kutubu kwa Mungu unasamehewa? Wakristo tulilogwa na nani kwa mafundisho kama haya? Kama Mungu anaruhusu watu wengine waendelee kukaa kwenye maumivu yaliyosababishwa na watu wengine kisa kapewa sadaka na kuombwa msamaha basi hiyo itakuwa ni rushwa na uminywaji wa haki. Mungu akiwa hakimu wa haki anatakiwa amuadhibu muuaji na sio kusamehe wakati kuna kiumbe chake kingine kinaumia.
Sasa mambo ya kusema mungu kasamehe kisha kapewa sadaka mi sijasema ,ila nachojua mungu ameweka utaratibu WA kufuta zambi haijalishi ni ya namna gani ,na huo utaratibu unamaamuzi wa kuufwata au ubaki ukiona mungu anaonea watu
 
Utasikia, fulani alikuwa jambazi hapo zamani kwa sasa kaokoka, fulani alikuwa tapeli sugu hapo zamani kaamua kuokoka au fulani alivunja ndoa za wengi hapo zamani kaamua kuokoka, nonsense, ujinga! Mnakosea sana, mnjidanganya, mambo hayendi hivyo!

1. TUACHE MASIKHARA KWA MUNGU WA HAKI

Ulikuwa jambazi umeibia watu, wameshindwa kuendelea kwajili yako, Mungu wa haki hawezi kukutakasa bila wewe kupata msamaha wa uliowaibia.

Ulikuwa mzinzi, umekuwa chanzo cha ndoa za watu kuvunjika, Mungu wa haki hawezi kukutakasa bila wewe kupata msamaha wa mme/mke uliemvunjia ndoa.

Ulikuwa muuaji, umeua baba, familia zinateseka, Mungu wa haki hawezi kukutakasa bila wewe kupata msamaha wa uliewaulia baba.

Ulikuwa dhulumati, umedhulumu watu, wanaishi maish ya dhiki, Mungu wa haki hawezi kukutakasa bila wewe kupata msamaha wa uliowadhulumu.

2. MIFANO

Baada ya Daudi kushika madaraka nchi ikawa ina majanga, alipomuuliza Mungu nini chanzo, aliambiwa utawala uliopita wa Sauli uliua wana watu wa Gibeon hivyo waende kwao wayamalize, baada ya hapoataitakasa nchi, walipoenda huko wa Gibeon waliwambia wao hawataki dhahabu wala Silver, wanataka kulipiza kisasi, wawape wana wa Sauli wa kiume saba wawaue na walipofanya hivyo nchi ilitakaswa.

Mfano mwingine Yesu mwenyewe aliwaambia wanafunzi wake kwamba kabla ya kutoa sadaka kaweke kwanza mambo sawa na uliowakosea, pia alishauri patana na mshitaki wako kwanza kabla hamjafika kwa hakimu.

Mfano mwingine wa zakayo alikumbuka dhambi zake na akasema atawarejeshea mara kumi aliowadhulumu, bda ya hapo ndipo aliweza kupokea wokovu.

3. AGANO LA KALE LILIRUHUSU JICHO KWA JICHO, JIPYA JE?

Agano la kale liliruhusu kulipiza jino kwa jino kama huo mfano wa kwanza wa kulipiza kisasi kwa kuua lakini haimaanishi agano jipya limefuta kila kitu, kilichobadilika ni kwamba mtu aliekukosea akija kukuomba msamaha haupaswi kulipizajino kwa jino, ni aidha umsamehe au kama roho inasita wewe mwambie wazi tu huwezi, hakuna haja ya kulipiza kwa jinsi alivyokuumiza.

4. HAIWEZEKANI KUOKOKA BILA KUPATA TIKETI YA MSAMAHA WA ULIOWAUMIZA

Ni hivi, Mungu sio dhalimu,wewe unaweza kukuta umenitendea mabaya halafu unaenda kanisani kuokoka lakin unasahau mimi kila asubuh naamka na majereaha uliyoniachia aidha umeniibia duka nimefirisika, umeua watu wangu wa karibu naumia, umeniibia mke ndoa ilivunjika, umenidhulumu kiwanja sina nyumba, n.k.

Mungu hawezi kusahau uovu ulionifanyia kisa eti umebadilika, unaenda sana kanisani, unatoa sadaka (zikiwemo pesa ulizonidhulumu ), n..k NEVER !!!! Na kuhakikishia Mungu ni wa haki hata sikia sala yako ya kuokoka kama hutotubu maovu yako kwa uliowaumiza, Mungu haongeki!

5. MWISHO KABISA

Mwenyezi Mungu anachukizwa mno na dhambi, hakikisha unajizuia sana kutenda dhambi kuumiza wengine na ukifanya hivyo fanya uwezavyo uwaombe msamaha, ndio tiketi pekee ya kuomba msamaha kwa Mungu.
Mbona umetumia muda mwingi kumpangia Mungu namna ya kusamehe wadhambi?😎
 
Mtoa uzi una akili sana. Nafikiri tunapaswa kujiongeza na sisi wenyew hapa. Nakazia hapa pia, Mfalme Daudi alimuua Uria ili Daudi aweze kumuoa mke Uria. Kilichotokea ili kulipa hyo dhambi mtoto wake wa kwanza aliyezaa na mke wa Uria alikufa ndo Daudi akapata msamaha wa Mungu.
 
zambi = dhambi. Hayo mafundisho ya kumruka mtu uliyemkosea na kwenda kumwomba Mungu msamaha ni mafundisho ya upotofu. Hata biblia imeandika kama humpendi ndugu yako unayemwona utawezaje kumpenda Mungu usiyemwona? Toba ya kweli ni kuanza kupatana na uliyemkosea na sio huu upumbavu wa kwenda kutubu kanisani na kumhonga mchungaji sadaka huku uliowaumiza wakiendelea kuumia.
Pointi iko ivi mwenye zambi kama hajaokoka imean haja repent anasamehewa dhambi zake bila kigezo chochote ,lakini ukiokoka kigezo chako cha kusamehewa kinakuwa Sawa na wew unavyosamea wengine
 
Kuna jamaa alikua jambazi akaokoka, na akasalimisha bunduki kanisani kilichofata polisi wakamdaka
 
Acha upotoshaji. Yesu hakuja kuruhusu maovu kwa kisingizio cha kufa msalabani. Alichofanya Yesu ni kuondoa zile taratibu za zamani kwamba ukitubu lazima uchinje kondoo umteketeze kwa moto. Pia kwenye huo mchakato kulikuwa na mtu aitwae kuhani ambaye alikuwa akiingia chumba cha ndani walipokuwa wanaabudia. Kulikuwa na pazia linatenganisha wanapoabudu waumini wa kawaida na kule anapoingia kuhani. Baada ya kifo cha Yesu lile pazia lilichanika lenyewe ndo ukawa mwisho wa hizo mambo. Kwa sasa hakuna haja ya kuhani kwasaababu kiimani tayari Yesu kashafanya hiyo kazi. Kwa sasa kama una dhambi unatubu direct kwa Mungu. Natumaini umenielewa.
You have much to learn bro
 
kin
Utasikia, fulani alikuwa jambazi hapo zamani kwa sasa kaokoka, fulani alikuwa tapeli sugu hapo zamani kaamua kuokoka au fulani alivunja ndoa za wengi hapo zamani kaamua kuokoka, nonsense, ujinga! Mnakosea sana, mnjidanganya, mambo hayendi hivyo!

1. TUACHE MASIKHARA KWA MUNGU WA HAKI

Ulikuwa jambazi umeibia watu, wameshindwa kuendelea kwajili yako, Mungu wa haki hawezi kukutakasa bila wewe kupata msamaha wa uliowaibia.

Ulikuwa mzinzi, umekuwa chanzo cha ndoa za watu kuvunjika, Mungu wa haki hawezi kukutakasa bila wewe kupata msamaha wa mme/mke uliemvunjia ndoa.

Ulikuwa muuaji, umeua baba, familia zinateseka, Mungu wa haki hawezi kukutakasa bila wewe kupata msamaha wa uliewaulia baba.

Ulikuwa dhulumati, umedhulumu watu, wanaishi maish ya dhiki, Mungu wa haki hawezi kukutakasa bila wewe kupata msamaha wa uliowadhulumu.

2. MIFANO

Baada ya Daudi kushika madaraka nchi ikawa ina majanga, alipomuuliza Mungu nini chanzo, aliambiwa utawala uliopita wa Sauli uliua wana watu wa Gibeon hivyo waende kwao wayamalize, baada ya hapoataitakasa nchi, walipoenda huko wa Gibeon waliwambia wao hawataki dhahabu wala Silver, wanataka kulipiza kisasi, wawape wana wa Sauli wa kiume saba wawaue na walipofanya hivyo nchi ilitakaswa.

Mfano mwingine Yesu mwenyewe aliwaambia wanafunzi wake kwamba kabla ya kutoa sadaka kaweke kwanza mambo sawa na uliowakosea, pia alishauri patana na mshitaki wako kwanza kabla hamjafika kwa hakimu.

Mfano mwingine wa zakayo alikumbuka dhambi zake na akasema atawarejeshea mara kumi aliowadhulumu, bda ya hapo ndipo aliweza kupokea wokovu.

3. AGANO LA KALE LILIRUHUSU JICHO KWA JICHO, JIPYA JE?

Agano la kale liliruhusu kulipiza jino kwa jino kama huo mfano wa kwanza wa kulipiza kisasi kwa kuua lakini haimaanishi agano jipya limefuta kila kitu, kilichobadilika ni kwamba mtu aliekukosea akija kukuomba msamaha haupaswi kulipizajino kwa jino, ni aidha umsamehe au kama roho inasita wewe mwambie wazi tu huwezi, hakuna haja ya kulipiza kwa jinsi alivyokuumiza.

4. HAIWEZEKANI KUOKOKA BILA KUPATA TIKETI YA MSAMAHA WA ULIOWAUMIZA

Ni hivi, Mungu sio dhalimu,wewe unaweza kukuta umenitendea mabaya halafu unaenda kanisani kuokoka lakin unasahau mimi kila asubuh naamka na majereaha uliyoniachia aidha umeniibia duka nimefirisika, umeua watu wangu wa karibu naumia, umeniibia mke ndoa ilivunjika, umenidhulumu kiwanja sina nyumba, n.k.

Mungu hawezi kusahau uovu ulionifanyia kisa eti umebadilika, unaenda sana kanisani, unatoa sadaka (zikiwemo pesa ulizonidhulumu ), n..k NEVER !!!! Na kuhakikishia Mungu ni wa haki hata sikia sala yako ya kuokoka kama hutotubu maovu yako kwa uliowaumiza, Mungu haongeki!

5. MWISHO KABISA

Mwenyezi Mungu anachukizwa mno na dhambi, hakikisha unajizuia sana kutenda dhambi kuumiza wengine na ukifanya hivyo fanya uwezavyo uwaombe msamaha, ndio tiketi pekee ya kuomba msamaha kwa Mungu.
kinyume chake, hiyo ni hukumu ya kibinadamu, ila kwa Mungu, anasamehe dhambi na hategemei mwanadamu asamehe kwanza ndio yeye akusamehe. wewe ukitenda dhambi, ni sahihi kwamba unatakiwa kutengeneza na wale uliowakosea, ila kufanya hivyo sio gharantee kwamba wasipokupokea hautasamehewa, anayesamehe ni Mungu, wanadamu hawajashikilia msamaha wako. anayesamehe na kusafisha ni Mungu tu.

hii ndio sababu Yesu alisema unapoenda kusali samehe wale waliokukosea, ili na Mungu akusamehe, kama hautawasamehe walokukosea na wewe hautasamehewa. ingelikuwa msamaha wangu umeshikiliwa mikononi mwa wanadamu, what if wasiponisamehe, ina maana Mungu hatakusamehe? wewe mwanadamu una nini au ni nani hasa hata ushikilie msamaha wa watu kwa Mungu pale wanapotubu wakati wewe mwenyewe umejaa madhaifu na dhambi tu?

dhambi yeyote hata kama ni ya kuua, unasamehewa. hata kama dhambi ni nyekundu kama damu, ukitubu kwa kumaanisha kuacha dhambi Mungu anakusamehe bure, tena wala hauhitaji kutoa pesa.
 
zambi = dhambi. Hayo mafundisho ya kumruka mtu uliyemkosea na kwenda kumwomba Mungu msamaha ni mafundisho ya upotofu. Hata biblia imeandika kama humpendi ndugu yako unayemwona utawezaje kumpenda Mungu usiyemwona? Toba ya kweli ni kuanza kupatana na uliyemkosea na sio huu upumbavu wa kwenda kutubu kanisani na kumhonga mchungaji sadaka huku uliowaumiza wakiendelea kuumia.
Kama uliyemkosea hayupo (ulimuua) je bible inasemaje ukitaka kutubu utasamehewa au mpaka nawe ufe ukamuombe huko msamaha?
 
"Mwenyezi Mungu anachukizwa mno na dhambi"


Mwenyezi Mungu ni mwepesi wa kusamehe

Mungu ni mwepesi sana wa kusamehe zile dhambi zinazomuhusu moja kwa moja mfano:
Hujaenda Msikitini/kanisani, hujatoa sadaka, nk lakini kama umetendea watu mabaya OMBA KWANZA MSAMAHA WAKUSAMEHE ndio urudi kwa Mungu; tofauti na hapo Msamaha wako kwa Mungu ni bahati nasibu.
Huwezi kuchukua shamba la mtu halafu uombe Mungu Msamaha? Huwezi kula mali ya masikini/ Mayatima halafu unaomba msamaha kwa Mungu bila kurudisha mali uliyo Iba?
Mtu anaiba Milioni mia halafu anatoa sadaka laki moja au hata Milioni moja....hiyo ni kumdhihaki Mungu kwa kumhonga mali ya WIZI!
Watu wengi wata angamia kwa kukosa maarifa!!!
 
Mungu ni mwepesi sana wa kusamehe zile dhambi zinazomuhusu moja kwa moja mfano:
Hujaenda Msikitini/kanisani, hujatoa sadaka, nk lakini kama umetendea watu mabaya OMBA KWANZA MSAMAHA WAKUSAMEHE ndio urudi kwa Mungu; tofauti na hapo Msamaha wako kwa Mungu ni bahati nasibu.
Huwezi kuchukua shamba la mtu halafu uombe Mungu Msamaha? Huwezi kula mali ya masikini/ Mayatima halafu unaomba msamaha kwa Mungu bila kurudisha mali uliyo Iba?
Mtu anaiba Milioni mia halafu anatoa sadaka laki moja au hata Milioni moja....hiyo ni kumdhihaki Mungu kwa kumhonga mali ya WIZI!
Watu wengi wata angamia kwa kukosa maarifa!!!
Kama niliemnyang'anya shamba nilimuua nitampata wapi ili kumuomba msamaha?
Mtazamo wako unaangalia watu walio kafibu na wewe tu, na bado wako hai.
 
Pointi iko ivi mwenye zambi kama hajaokoka imean haja repent anasamehewa dhambi zake bila kigezo chochote ,lakini ukiokoka kigezo chako cha kusamehewa kinakuwa Sawa na wew unavyosamea wengine
Amen, Point nzito sana hii
 
Mungu ni mwepesi sana wa kusamehe zile dhambi zinazomuhusu moja kwa moja mfano:
Hujaenda Msikitini/kanisani, hujatoa sadaka, nk lakini kama umetendea watu mabaya OMBA KWANZA MSAMAHA WAKUSAMEHE ndio urudi kwa Mungu; tofauti na hapo Msamaha wako kwa Mungu ni bahati nasibu.
Huwezi kuchukua shamba la mtu halafu uombe Mungu Msamaha? Huwezi kula mali ya masikini/ Mayatima halafu unaomba msamaha kwa Mungu bila kurudisha mali uliyo Iba?
Mtu anaiba Milioni mia halafu anatoa sadaka laki moja au hata Milioni moja....hiyo ni kumdhihaki Mungu kwa kumhonga mali ya WIZI!
Watu wengi wata angamia kwa kukosa maarifa!!!
watu wanachukulia vitu rahisi rahisi sana hawa, Mtu bado kashikilia mali alizodhulumu eti anajipeleka kanissani kuomba wokovu, Dah!!
 
Kama niliemnyang'anya shamba nilimuua nitampata wapi ili kumuomba msamaha?
Mtazamo wako unaangalia watu walio kafibu na wewe tu, na bado wako hai.
Tafuta mabaki yake / watoto ama ndugu wa damu walioumizwa na ulichomfanyia nduguye
 
Kwahiyo hata bashite akitaka kuokoka aende kumuomba lissu kwa kutaka kumtoa uhai
Iwe ni yeye au wewe au mimi kwa aliehusika kwa tukio lile hakuna shortcut ya kuokoka, hata uzunguke makanisa yote ni kujisumbua tu, ni mpaka uende kwa Lissu umuombe msamaha
 
Back
Top Bottom