Umeumiza watu halafu unataka kuokoka bila kuwaomba msamaha uliowaumiza, hilo haliwezekani!

Utasikia, fulani alikuwa jambazi hapo zamani kwa sasa kaokoka, fulani alikuwa tapeli sugu hapo zamani kaamua kuokoka au fulani alikuwa mbakaji hapo zamani kaamua kuokoka. NONSENSE, UJINGA! Mnakosea sana, mnjidanganya, mambo hayendi hivyo!

1. TUACHE MASIKHARA KWA MUNGU WA HAKI

Huwezi kuroga watu wakapatwa magonjwa na matatizo mengine halafu uanze kutafuta wokovu eti unasalimisha matunguli yako kanisani yachomwe, Mungu wa haki hawezi kukubali huo msamaha !! anza kwa kuwaomba msamaha uliowachawia na utegue vifungo !!

Umedhulumu shamba la mtu kisa masikini, unavuna kila mwaka huku familia yake wanalala njaa ama chakula hakiwatoshi kwajili yako, Unajidai kupeleka sadaka kanisani kwa mavuno ya shamba la wizi eti unatafuta wokovu, Mungu wa haki hawezi kukubali huo msamaha !! anza kwa kurudisha shamba na uombe msamaha


Huwezi kudhulumu mali ya masikini au yatima halafu uanze kutafuta wokovu, Mungu wa haki hawezi kukubali huo msamaha !! anza kwa kurudisha ulivyoiba na kuwaomba msamaha wahusika !!

Huwezi kufarakanisha wanandoa wakaachana halafu uanze kutafuta wokovu, Mungu wa haki hawezi kukubali huo msamaha !! anza kwa kuwaomba msamaha uliowafarakanisha !!

Huwezi kuua watu wanaacha familia zao halafu uanze kutafuta wokovu, Mungu wa haki hawezi kukubali huo msamaha !! anza kwa kuwaomba msamaha wanafamilia wake !!

shinda kanisani muda wote, sikiliza gospel siku nzima, toa sana sadaka, vaa mashati ya vitenge, n.k. Mungu wa haki hawezi kukubali msamaha wako, anzia kwanza kwenye chanzo cha watu uliowaumiza !!

2. MIFANO

Baada ya Daudi kushika madaraka nchi ikawa ina majanga, alipomuuliza Mungu nini chanzo, aliambiwa utawala uliopita wa Sauli uliua wana watu wa Gibeon hivyo waende kwao wayamalize, baada ya hapoataitakasa nchi, walipoenda huko wa Gibeon waliwambia wao hawataki dhahabu wala Silver, wanataka kulipiza kisasi, wawape wana wa Sauli wa kiume saba wawaue na walipofanya hivyo nchi ilitakaswa.

Mfano mwingine Yesu mwenyewe aliwaambia wanafunzi wake kwamba kabla ya kutoa sadaka kaweke kwanza mambo sawa na uliowakosea, pia alishauri patana na mshitaki wako kwanza kabla hamjafika kwa hakimu.

Mfano mwingine wa zakayo alikumbuka dhambi zake na akasema atawarejeshea mara kumi aliowadhulumu, bda ya hapo ndipo aliweza kupokea wokovu.

Mfalme Daudi alimuua Uria ili Daudi aweze kumuoa mke Uria. Kilichotokea ili kulipa hyo dhambi mtoto wake wa kwanza aliyezaa na mke wa Uria alikufa ndo Daudi akapata msamaha wa Mungu.

3. AGANO LA KALE LILIRUHUSU JICHO KWA JICHO, JIPYA JE?

Agano la kale liliruhusu kulipiza jino kwa jino lakini haimaanishi agano jipya limefuta kila kitu, agano jipya linatusihi zaidi tupendane hivyo kilichobadilika ni kwamba mtu aliekukosea akija kukuomba msamaha haupaswi kulipiza jino kwa jino, ni aidha umsamehe au kama roho inasita wewe mwambie wazi tu huwezi, hakuna haja ya kulipiza.

Na kwa mawazo yangu navyoona kwamba mwenye dhambi kama hajabatizwa anaweza kusamehewa dhambi zake moja kwa moja ikiwa yupo tayari kumpkea Yesu, lakini baada ya hapo kigezo chako cha kusamehewa kinakuwa kizito zaidi, na kumbuka kubatizwa huwa ni mara moja tu

4. HAIWEZEKANI KUOKOKA BILA KUPATA TIKETI YA MSAMAHA WA ULIOWAUMIZA

Ni hivi, Mungu sio dhalimu,wewe unaweza kukuta umenitendea mabaya halafu unaenda kanisani kuokoka lakin unasahau mimi kila asubuh naamka na majereaha uliyoniachia aidha umeniibia duka nimefirisika, umeua watu wangu wa karibu naumia, umeniibia mke ndoa ilivunjika, umenidhulumu kiwanja sina nyumba, n.k.

Mungu hawezi kusahau uovu ulionifanyia kisa eti umebadilika, unaenda sana kanisani, unatoa sadaka (zikiwemo pesa ulizonidhulumu ), n..k NEVER !!!! Na kuhakikishia Mungu ni wa haki hata sikia sala yako ya kuokoka kama hutotubu maovu yako kwa uliowaumiza, Mungu haongeki!

5. MWISHO KABISA

Huwezi kumruka mtu uliyemuumiza na kukurupuka kukimbilia kanisani kwa mchungaji akuwekee mikono kichwani kukuombea msamaha kwa Mungu huo ni upotofu, mambo hayaendi hivyo!. Toba ya kweli ni kuanza kupatana na uliyemkosea na sio huu upumbavu wa kwenda kutubu kanisani na kumhonga mchungaji sadaka huku uliowaumiza wakiendelea kuumia.
Ukipata ufahamu wa kuokoka ni vyema kufata mchakato huu....
 
Mungu huyo hawezi kujidhihirisha mwenyewe kwamba yupo wala hawezi kujitetea mwenyewe.

Huu ni uthibitisho tosha kwamba Mungu huyo hayupo.

Kama yupo aje hapa ani prove wrong.

Vinginevyo Mungu huyo mmemuumba vichwani mwenu tu wala hana uhalisia wowote ule.
Kwani Mungu ndie kakwambia uthibitishe?
Mimi ndie nimetaka unithibitishie kutokuwepo kwake. Kusema kama yupo aje kuku prove wrong, unakuwa haujanipa proof ya madai yako.
 
Haimanishi ivyo cha msingi n kuwa na hali ya kutaka usafisho na kuweza kumshirikisha Mungu huyo mtu alipo akusamehee.Na kweli utasamehewa
Swali langu lilitokana na kauli yao kuwa Mungu hasamehi dhambi zisizomhusu, anaepaswa kukusamehe ni yule uliemkosea.
 
Sijui lolote kuhusu huyo Makonda ila hadi uokoke ni mpaka upewe wokovu, anaekupa wokovu hawezi kukubariki ikiwa watu uliowakosea hujawaomba msamaha na kurudisha ulichokichukua.

Kuokoka ni siri ya mtu japo anaweza kuhadaa wengi machoni
{}
 
Kwani Mungu ndie kakwambia uthibitishe?
Mimi ndie nimetaka unithibitishie kutokuwepo kwake. Kusema kama yupo aje kuku prove wrong, unakuwa haujanipa proof ya madai yako.
Nita kuthibitishiaje kitu ambacho hakipo?

Wewe unayejua kipo ndio unatakiwa uthibitishe kipo.
 
Back
Top Bottom