SoC04 Tutengeneze msingi ulio bora kuhimili dhoruba zitakazo tukabili baadae

Tanzania Tuitakayo competition threads

DMmasi

JF-Expert Member
Nov 28, 2020
437
670
Naam kilicho bora na imara hujengwa katika misingi iliyo bora na imara
Tanzania tunayoitaka iko mikononi kwa wazee ambapo yapaswa kukabidhiwa kwa vijana na watoto, maarifa na ujuzi ni vitu muhimu vya kutuvusha kuifikia Tanzania tunayoitaka.

Elimu itolewayo mashuleni izidi kuboreshwa isiishie tuu kwenye kutafuta ufaulu kwa kukariri bali iwajenge watoto katika hali ya kuwa jasiri, kujiamini,kutii, kuheshimu na upendo.

Yapo ya muhimu ya kuyafundisha mashuleni watoto serikali iwe na utaratibu ambao mtoto atakaye maliza elimu ya msingi ajue walau sheria mama ya nchi inasomekaje, huduma za dharura zinatolewaje.
Nasiyo kupima uwezo kwa maswali ya kuowanisha (safu A,mwaka 1807 unaenda kuangalia safu B, ninini kilitokea miaka iyo) elimu ya kukariri.

Serikali itengeneze mifumo wezeshi na mazingira yatakayo wafanya wanafunzi wafurahi kuwepo shuleni kwanzia rasilimali watu,fedha na viwezeshi vingine shule isiwe ni madarasa, vyoo,maabara na madawati bali ibebe na jukumu la kumfundisha wanafunzi uwajibikaji walai kuwepo na mashamba darasa.

Serikali inaundwa na watu na watu ndiyo sisi turudi kwa upande wa jamii
wanasema kijiji bila wazee ni mateso

Naamu nitoe rahi kwa wazazi hasa wazazi wa siku hizi waleeni watoto kama mlivyolelewa ninyi tuache kuyatafakari maisha tuliyolelewa kama maisha magumu na mateso na tuifute ile kauli ya "sitaki mtoto wangu ateseke".
Wazee wanasema "Nyakati ngumu zinamtengeneza mtu imara na mtu imara anazitengeneza nyakati rahisi, alafu nyakati rahisi zinamtengeneza mtu dhaifu na mtu dhaifu anatengeneza nyakati ngumu"
wazazi waleeni watoto kwa kuwatoa kwenye icho kiota kama ninyi mmekwisha fanikiwa basi watengenezeni kwenye mfumo wa wao kufanikiwa mara mbili yenu.

Wafungulieni watoto wakutane na watoto wengine siyo wasinde na televisheni na kuingia mitandaoni wanakitana na vitu vizito vinavyotulemea hadi sisi

Nidhamu, heshima, adabu, usafi na kujituma na kujitumikia iwe dhima ya malezi kwa watoto wetu. Jamii hii tunayoiyogopa yenye madhila na maasi mengi ndiyo jamii tunayozidi kuitengeneza

Nimalize kwa kusema jamii iliyo bora Ina Mila na tamaduni zetu. Naamu tumetengenezewa fikra ya kwamba elimu za jando na unyago ni Mila Potofu tumekumbatia "my name is doctor living stone" matokeo yake ndo haya ya familia zisizokuwa na msingi hata wanyama na ndege porini wanazaa nakulea watoto wao pamoja.

Tuzikumbuke na kuzienzi Mila na tamaduni zetu wazee walifunzwa kuheshimu na jamii iliweza kulea mtoto,
kwa nyakati hizi tunaogopa jamii kumlea mtoto sababu siyo sehemu salama watoto wanafichwa ndani hatutaki kurekebisha jamii ila tumekimbilia ndani vipi kesho shida ikiwa ni familia tutakimbilia wapi.

Wapeni muda watoto, waleeni katika misingi ya familia (baba na mama)
niliwahi kumsikia Dr Chris Mauki akisema maleza ya mama ni yakubembeleza na ya baba ni yakuelekeza na watoto wanayahitaji yote.

Tusiwalee watoto kwa kuwakandamiza bali tuwemarafika wakuzungumza wawe huru siyo kujikunyata na kushindwa kuzungumza.

ASANTENI
mwana jamii
Mmasi Dismas
 
Naamu nitoe rahi kwa wazazi hasa wazazi wa siku hizi waleeni watoto kama mlivyolelewa ninyi tuache kuyatafakari maisha tuliyolelewa kama maisha magumu na mateso na tuifute ile kauli ya "sitaki mtoto wangu ateseke".
Wazee wanasema "Nyakati ngumu zinamtengeneza mtu imara na mtu imara anazitengeneza nyakati rahisi, alafu nyakati rahisi zinamtengeneza mtu dhaifu na mtu dhaifu anatengeneza nyakati ngumu"
wazazi waleeni watoto kwa kuwatoa kwenye icho kiota kama ninyi mmekwisha fanikiwa basi watengenezeni kwenye mfumo wa wao kufanikiwa mara mbili yenu.
Akili kubwa hii, umetambua nini tunataka.

Wazazi lazima wawafundishe watoto uwajibikaji kama sifa ya msingi. Hii kauli ya sitaki mwanangu ateseke ndiyo wazungu wanawaita hao wazazi "helicopter parents' imewaharibu vijana na tayari wameishai'flag' sasa wazazi wanajitambua kuiepuka.
Lakini kwetu ninaona bado tatizo lipo. Lile kundi la wanaoipitiliza kauli ya kuwaandalia vizazi vyake maisha mazuri hadi wanaharibu na wanajiona wapo sawa ni hatari sana.
Ahsante kwa elimu na tuendelee kuelimishana zaidi.

Wapeni muda watoto, waleeni katika misingi ya familia (baba na mama)
niliwahi kumsikia Dr Chris Mauki akisema maleza ya mama ni yakubembeleza na ya baba ni yakuelekeza na watoto wanayahitaji yote.
Yas, maelekezo toka kwa baba ili mtoto ishi maisha ya baraka, na maonyo toka kwa mama ili mtoto asilaanike.......

Insha yako ni nzuri sana, kwa sababu tunafahamu misingi ndiyo ya muhimu u apojenga kitu chochote. Na ndiyo watoto na familia bora itapelekea taifa bora kwa ujumla. Saaafi
 
sometimes,unaweza kuwaza positive but unfortunatly your community thinking negatively

unaweza kutupia lawama kwa serikali ila unakuta tatizo lipo kwa wananchi after government taking corrective measures,unaweza ukaitupia lawama jamii ila tatizo lipo kwa mzazi ambaye kwa kiasi kikubwa cha matatizo yanaanzia hapa.

kuna kanuni na misingi muhimu ya ulimwengu tumeishaiacha na kwa bahati mbaya media na vyombo vengine vimetia nguvu katika hili,hakuna wa kumtupia lawama zaidi ya kupambana na hali zetu.
 
Akili kubwa hii, umetambua nini tunataka.

Wazazi lazima wawafundishe watoto uwajibikaji kama sifa ya msingi. Hii kauli ya sitaki mwanangu ateseke ndiyo wazungubwqnawaita hao wazazi "helicopter parents' imewaharibu vijana na tayari wameishai'flag' sasa wazazi wanajitambua kuiepuka.
Lakini kwetu ninaona bado tatizo lipo. Lile kundi la wanaoipitiliza kauli ya kuwaandalia vizazi vyake maisha mazuri hadi wanaharibu na wanajiona wapo sawa ni hatari sana.
Ahsante kwa elimu na tuendelee kuelimishana zaidi.


Yas, maelekezo toka kwa baba ili mtoto ishi maisha ya baraka, na maonyo toka kwa mama ili mtoto asilaanike.......

Insha yako ni nzuri sana, kwa sababu tunafahamu misingi ndiyo ya muhimu u apojenga kitu chochote. Na ndiyo watoto na familia bora itapelekea taifa bora kwa ujumla. Saaafi
ndugu yangu Uhakika Bro nashukura sana kwa mapokeo mazuri nafurahi kuona bado kuna watu wanaoyaona haya maisha ya utandawazi na ufahari tunayoyaishi kwamba kuna namna tunakosea

wasiwasi wangu unabaki palepale kama nyakati hizi tunalea watoto kifamilia siyo kijamii tukiamini jamii siyo sehemu salama ikifika nyakati na familia kumechafuka tutawalea wapi
 
sometimes,unaweza kuwaza positive but unfortunatly your community thinking negatively

unaweza kutupia lawama kwa serikali ila unakuta tatizo lipo kwa wananchi after government taking corrective measures,unaweza ukaitupia lawama jamii ila tatizo lipo kwa mzazi ambaye kwa kiasi kikubwa cha matatizo yanaanzia hapa.

kuna kanuni na misingi muhimu ya ulimwengu tumeishaiacha na kwa bahati mbaya media na vyombo vengine vimetia nguvu katika hili,hakuna wa kumtupia lawama zaidi ya kupambana na hali zetu.
ni kwelii kabisa kuna mdau mmoja alisema tunalalamika serikali ni wezi ila hakuna wezi kama wananchi na situnakubaliana serikali ni mfumo ni kwamba kunawalio amua kujinufaisha kupitia mfumo huo

Bado serikali ikitilia mkazo kwenye baadhi ya mambo itaweza kuwaongoza wananchi kwenye uwelekeo inayotaka

Jamii haina shida ila ni wanaopaswa kuishi kama jamii wanashindwa kuaminiana na niwazi binadamu tunaishi kwa kutegemeana wakati mimi ninakuwa ukitaka kufanya mautundu Yale ya kitoto unakwepa macho mengi ila sikuizi watoto wanakwepa tuu macho ya wazazi wao wasipo onekana na wazazi wao wako huru kutenda wapendalo
 
wasiwasi wangu unabaki palepale kama nyakati hizi tunalea watoto kifamilia siyo kijamii tukiamini jamii siyo sehemu salama ikifika nyakati na familia kumechafuka tutawalea wapi
Sijui ni nini tutafanya kurudisha udugu wa kijamii wa kitaifa (brotherhood) maana mataifa yanayofanya vizuri yana hicho kitu sana mfano ISRAEL, hata URUSI na INDIA kwa kiasi. Wana namna fulani kama watoto wa mama mmoja hivyo wanajaliana, wanarekebishana na kuchanana laivu.

Kuna wakati nnawaza labda kitu kidooogo tu katika falsafa ya nchi mfano kuchukulia nchi kama mama mkuu( Mother Russia, Vande mataram) inapelekea wananchi wake kuwa na udugu kitaifa na kusimama kama jamii moja, we unaonaje? Hatua gani tunaweza zichukua kama jamii?
 
Back
Top Bottom