Aramun
Senior Member
- Nov 8, 2023
- 182
- 800
Hali ya mvua jijini Dar si shwari kabisa, hii ni siku ya 5 sasa mvua zinanyesha nonstop. Kwa miundombinu ya hili jiji ilivyo mibovu ingekuwa busara shule zifungwe kwa muda, hasa shule za msingi, japo yale madarasa ya chini la kwanza mpaka la nne.
Hivi ninavyoandika hapa mvua imenyesha usiku kucha, na sipati picha huko mitaani hali ikoje. Watu wazima tu leo kufika kazini ni kwa mshikemshike sana, sembuse hawa watoto wadogo?
Na hii yote inasababishwa na serikali kutokuwa serious na miundombinu ya ndani ya miji, 90% ya jiji la Dar halina barabara za mitaani. Ukitoka tu kwenye barabara kuu zenye lami ukaingia mtaani basi unakutana na vijibarabara vya tope ambavyo vingi vimechongwa na wananchi wenyewe, havina hata standard ya kuitwa barabara za vumbi.
Hivi ninavyoandika hapa mvua imenyesha usiku kucha, na sipati picha huko mitaani hali ikoje. Watu wazima tu leo kufika kazini ni kwa mshikemshike sana, sembuse hawa watoto wadogo?
Na hii yote inasababishwa na serikali kutokuwa serious na miundombinu ya ndani ya miji, 90% ya jiji la Dar halina barabara za mitaani. Ukitoka tu kwenye barabara kuu zenye lami ukaingia mtaani basi unakutana na vijibarabara vya tope ambavyo vingi vimechongwa na wananchi wenyewe, havina hata standard ya kuitwa barabara za vumbi.