Profesa Janabi kama Dr. Fauci wa Marekani

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,842
46,603
Dr. Anthony Fauci alikuwa ni Mkurugenzi wa taasisi ya kitaifa ya Marekani ya magonjwa ya mzio na kuambukiza(NIAID) kwa takribani miaka 20 na jina kubwa katika masuala ya Afya Marekani kama alivyo Janabi hapa Tanzania.

Wakati wa mlipuko wa COVID anakumbukwa zaidi kwa jinsi alivyokuwa akitoa elimu dhidi ya conspiracies na myths nyingi zilizohusiana na COVID-19 na chanjo zake baadaye.

Fauci alichukiwa sana na kudhihakiwa na wapinga chanjo(anti-vaxxers) pamoja na wapenda story za nadharia za njama(conspiracists) kwa sababu kila mara alikuwa akienda kinyume nao na matamanio yao. Ilifikia hadi mahali usalama wake ukatishiwa ikabidi apewe ulinzi wa ziada.

Mashambulizi na dhihaka dhidi ya nguli Profesa Janabi kwa elimu anayoitoa kwa umma ni kama vinafuata mkondo wa Dr. Fauci.
 
1713927864933.jpg

UJUMBE MUHIMU: USIPOFIKA UUME, MKONGA UTAFIKA
 
Sawa mkuu. Ila Janabi kiasi flan anazingua, japo namheshimu saana nguli huyu katika medani za afya
 
Kwamba tule kipande kimoja cha mhogo kwa siku bila kujali kama wewe ni sedentary worker, mzee, kijana, mtoto, n.k.?
 
Janabi simfuati wala kumsikiliza, huwezi kuniambia mie nabeba zege nile kipande kimoja cha muhogo, nisinywe maji mengi(serious) yaani nisinywe maji mpaka nitakapopata kiu. 😂🤣
 
Ndivyo
Janabi simfuati wala kumsikiliza, huwezi kuniambia mie nabeba zege nile kipande kimoja cha muhogo, nisinywe maji mengi(serious) yaani nisinywe maji mpaka nitakapopata kiu. 😂🤣
alivyosema? Hata KWA Watu wa kazi ngumu?
 
Janabi anaelimisha nchi yenye makundi ya wajinga...

Na yeye Janabi anaongea kienyeji sana...aweke elimu yake kwenye maandishi...na source ya maelezo yake ili wenye maswali tumuulize...

Je vyakula organic vina madhara kama haya ya vyakula hivi vyenye sumu za madawa?
Mtu anaekula organic...ale tofauti?

Why siku hizi vyakula vinaleta magonjwa Sana kuliko zamani?

Maswali ni mengi
 
Back
Top Bottom