Naiomba Serikali yetu itunge sheria kali ya kuwalinda wanyama wa majumbani eg. Paka, Mbwa n.k

Mjanja M1

JF-Expert Member
Oct 7, 2018
3,706
12,532
Mimi Mjanja M1 sikuwahi kuwaza kama kuna siku nitaandika uzi kwaajili ya wanyama hususani wanyama wa majumbani eg. Paka, Mbwa na wengine ambao tunawafuga.

Kwenye pilika zangu nimekutana na Vitoto vya Paka vikiwa vimetupwa jalalani na muhusika (Mfugaji) hajulikani. NILIUMIA SANA šŸ˜¢

Ukiachana na suala la kutupa wanyama wanapozaa eg. Paka na Mbwa bado kuna suala la kuwatesa wanyama kwa kuwapiga pindi watu wanapowaona mitaani, kama wewe ni mmoja wa watu waliowahi kuona Mbwa au paka akiwa na shida kwenye mwili wake basi tambua kuwa kuna katili amemnyanyasa mnyama kwa kumrushia mawe au kumpiga na silaha nyengine.

Ninaumia sana ninapoona wanyama wa majumbani wananyanyasika bila ya kuwa na mtetezi wao, Mimi Mjanja M1 kwa kutumia Platform hii ya Jamiiforums naamini ombi langu litafanyiwa kazi na serikali yetu ili wanyama wawe salama zaidi.

Ningependa pia kuiomba Serikali yetu iwe inatoa ruhusa kwa wenye uwezo pekee kuishi na wanyama na sio kila mtu yoyote, Mateso wanayoyapitia wanyama wa majumbani ni makubwa maana wakiumwa wamiliki wanashindwa hata kuwapeleka hospital kwaajili ya matibabu.

NAAMINI OMBI LANGU LITAFANYIWA KAZI, NA PIA WEWE UNAESOMA HAPA NAKUOMBA SANA UUSAMBAZE UJUMBE HUU ILI TUWALINDE WANYAMA WA MJUMBANI NA MATESO.

ASANTENI SANA! šŸ™
 
Serikali imeshindwa kutunga sheria kali kuwalinda watoto wanaoishi mazingira magumu ije ihangaike na mbwa na paka,huu uzungu uishie ulaya nasio Afrika na tena Tanzania

Napinga hoja
 
Kweli kabisa
Mbona wanalinda wanyapori na waharibifu kama tembo, fisi, mbwa mwitu , chui , kanga
Ambao ni wakorofi

Unakuta mtu anamtenda visivyo paka, mbwa, kuku na kadhalika
Nadhani tuwe na utu tupende viumbe wengine wanyama na mimea
 
Sheria ipo Mkuu ya kitambo tu ni vile haifuatiliwi. Sheria ya ustawi wa wanyama ikishirikiana na sheria ya magonjwa ya mifugo, jumlishia hapo sheria ya madaktari wa mifugo ongezea pia sheria ya ufugaji nyuki, na ile ya samaki aisee zipo nyingi sana.

Siku Tanzania ikifuata sheria itakuwa ni nchi ngumu sana.

Huwa najiuliza Utii wa sheria unarahisisha maisha/utawala ila kwanini Tanzania utovu wa sheria ndio unarahisisha maisha/utawala?.
Tanzania hadi mtawala lazima apindishe au upuuzie baadhi ya sheria ili nchi itawalike. Sijui kwanini tumezitunga na kuzikopa ilihali zinatutesa na mbaya zaidi hatuziwezi.
 
Naunga mkono hoja hii,kipindi nchi Ina heshima na adabu,tulikua na chama kilichojihusisha kulinda haki za wanyama,nakumbuka kwa Dar ofisi yao ilikua karibu na mnazi mmoja primary school,bila shaka mafisadi wameshachukua lile jengo,scouts pia walisaidia sana,inasikitisha kuona mtu amembeba kuku kwa miguu na kichwa chini ni ushenzi at its best
 
Punda ndio hasa natamani nione wakiwekewa sheria kali zaidi . Kama umewahi kukaa umasaini na singida ndipo utajua punda ni mnyama wanyumbani anaeteseka zaidi šŸ˜­
 
Back
Top Bottom