kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,331
- 12,647
Manufaa ya muungano tumeyaona, ni matamu sana kwa watanzania walio wengi. Kila kijana mzanzibar anatamani kwenda kuishi Tanzania bara, na wako watanzania bara ambao wanatamani kwenda Zanzibar kwasababu moja au nyingine. manufaa ya muungano kila mtu anaweza kuyasimulia bila kuambiwa wala kusoma pahala popote.
Mwalimu Nyerere na Karume nina uhakika wote au mmojawapo alitaka muungano wa serikali moja, na wako wazee ambao wanajua dhamira ya muungano na aina ya muungano ambayo waasisi waliukusudia lakini kwa unafiki na woga wao wamenyamaza kimya na hatimaye kufa na siri hiyo.
Wazee wa hivi hawafai kupewa heshima tunayowapa, maana ni wanafiki, waoga na wasioona mbele. Nyerere sio mjinga kuifuta serikali ya Tanganyika na asiifute ya Zanzabar, lazima kuna jambo ambalo tunafichwa na kupewa sababu za kijinga na uongo juu ya muungano wa serikali mbili. G55 hawakuwa wajinga kudai kuirudisha serikali ya Tanganyika; bila shaka ilikuwa kujibu mkwamo wa kupata serikali moja.
Wakati tunaelekea kuadhimisha sikukuu ya Muungano ni aibu nchi moja kuwa na serikali kamili mbili bila kuwepo ya Tanganyika. Wazee kama Pius Msekwa, Warioba, Butiku, Mongella, Malecella, Msuya, Sumaye, Kikwete, na wengine ambao wanafahamu sababu za kweli na halisi juu ya kwanini serikali ya tanganyika ilifutwa na ya zanzibar akabakizwa hadi Sasa waitoe siri hiyo kabla hawajaiaga dunia na kuondoka nayo hata kama kwakufanya hivyo kutaleta shida kwao. maana watoto wajao hawataujua ukweli halisi juu ya kwanini kuna serikali 2 badala ya 1 au 3.
Muungano wa aina hii utahojiwa na kila kijana wa leo na wa kesho mwenye akili timamu. Hii haitaleta afya ya muungano siku zijazo wakati wazee wote wanaoijua siri ya muungano watakapokuwa wameondoka duniani. Vijana watatafuta njia zao za kusawazisha ujinga, uzembe na woga wa mababu zao.
Mwalimu Nyerere na Karume nina uhakika wote au mmojawapo alitaka muungano wa serikali moja, na wako wazee ambao wanajua dhamira ya muungano na aina ya muungano ambayo waasisi waliukusudia lakini kwa unafiki na woga wao wamenyamaza kimya na hatimaye kufa na siri hiyo.
Wazee wa hivi hawafai kupewa heshima tunayowapa, maana ni wanafiki, waoga na wasioona mbele. Nyerere sio mjinga kuifuta serikali ya Tanganyika na asiifute ya Zanzabar, lazima kuna jambo ambalo tunafichwa na kupewa sababu za kijinga na uongo juu ya muungano wa serikali mbili. G55 hawakuwa wajinga kudai kuirudisha serikali ya Tanganyika; bila shaka ilikuwa kujibu mkwamo wa kupata serikali moja.
Wakati tunaelekea kuadhimisha sikukuu ya Muungano ni aibu nchi moja kuwa na serikali kamili mbili bila kuwepo ya Tanganyika. Wazee kama Pius Msekwa, Warioba, Butiku, Mongella, Malecella, Msuya, Sumaye, Kikwete, na wengine ambao wanafahamu sababu za kweli na halisi juu ya kwanini serikali ya tanganyika ilifutwa na ya zanzibar akabakizwa hadi Sasa waitoe siri hiyo kabla hawajaiaga dunia na kuondoka nayo hata kama kwakufanya hivyo kutaleta shida kwao. maana watoto wajao hawataujua ukweli halisi juu ya kwanini kuna serikali 2 badala ya 1 au 3.
Muungano wa aina hii utahojiwa na kila kijana wa leo na wa kesho mwenye akili timamu. Hii haitaleta afya ya muungano siku zijazo wakati wazee wote wanaoijua siri ya muungano watakapokuwa wameondoka duniani. Vijana watatafuta njia zao za kusawazisha ujinga, uzembe na woga wa mababu zao.