UZUSHI Maziwa fresh ni tiba ya sumu ya vumbi linaloingia kwenye mfumo wa upumuaji

Baada ya tathmini, tumebaini kuwa taarifa hii ni ya uzushi
Umewahi kunywa sumu yoyote ile kimakosa kisha baadhi ya watu wakakushauri utumie maziwa fresh kama sehemu ya tiba?

7C491536-A6B7-4C70-9D10-667D0301585D.jpeg

Madai ya maziwa fresh kuwa na uwezo wa kuondoa sumu mwilini yamekuwepo wa muda mrefu. Katika kujadili ufanisi wake, mdau mmoja wa JamiiForums amekosoa vikali tiba hii kwa kusema kuwa maziwa hayana uwezo wowote katika kuondoa sumu.

Amewashauri watanzania kuacha kufanya mambo kwa mazoea pasipo kuwa na uhakika kwanza wa jambo husika.

Taarifa za kitabibu zinasemaje kuhusu nadharia ya uwezo wa maziwa katika kudhibiti/kutibu sumu mwilini?
Kwa muda mrefu kumekuwa na imani kwamba pale ambapo mtu amepita kwenye vumbi, au amevuta hewa chafu yenye moshi au vumbi jingi basi atakunywa maziwa kwa imani kwamba anakunguza uwezekano wa madhara yanayoweza kujitokeza kwa vumbi hilo kuingia kwenye mfumo wa hewa?

Je, kuna uhusiano wowote kati ya kunywa Maziwa na kusafisha mfumo wa hewa dhidi ya madhara yatokanayo na vumbi na moshi?
 
Tunachokijua
Kwa mujibu wa Idara ya Chakula ya Marekani (USDA), maziwa ni chakula chenye utajiri mkubwa wa virutubisho vinavyohitajika kwa ukuaji bora wa binadamu.

Huwa na madini chuma, protini, nishati, sukari, calcium, magnesium, sodium, zinc, folate, choline pamoja na virutubisho vingine muhimu kwa afya.

Nadharia ya sumu pamoja na tiba zake
Sumu ni kitu chochote kilicho kwenye hali ya kimimika, gesi au yabisi chenye kuleta hatari kwa afya baada ya kupakwa, kumezwa, kuingizwa au kuvutwa mwilini kwa njia ya hewa.

Chakula, madawa pamoja na vinywaji vya kawaida vinavyotumika kila siku vinaweza kugeuka pia kuwa sumu ikiwa vitatumika kwa namna isiyofaa. Hivyo, sumu isiangaliwe kama kemikali mbaya pekee, bali kitu chochote kile chenye uwezo wa kuamsha au kupoozesha mifumo na kinga za mwili hasa kinapotumika vibaya.

Kitaalam, kila aina ya sumu huwa na tiba yake ambayo kwa lugha za kitabibu huitwa Antidotes. Huu ni kama ufunguo kwenye kufuli, ukimaanisha kuwa ni aina moja tu ya funguo ndio inaweza kufungua kufuli husika.

Mfano, sumu ya paracetamol (panadol) hutibiwa kwa N-Acetylcysteine, chuma kwa Deferoxamine, baadhi ya dawa za kulevya kwa Naloxone, Benzodiazepines kwa flumazenil, sumu ya nyoka kwa Anti snake venom, virusi vya mbwa na Anti rabies.

Pia, sumu nyingi za viwandani mathalani Arsenic hutibiwa kwa D-Penicillamine, cyanide kwa Hydroxocobalamine pamoja na copper kwa methylene blue.

Hii inatoa maana kuwa, matibabu ya sumu ni jambo la kuangaliwa kwa tahadhari kubwa kwani siyo kila njia au tiba hufaa kwa aina zote za sumu.

Maziwa katika kutibu sumu
JamiiForums imebaini kuwa Maziwa hayana tofauti na maji katika kutibu sumu. Ni kimiminika kisicho na uwezo wowote katika kuokoa uhai wa mtu aliyekufa kutokana na kumeza aina fulani ya sumu. Pia, hayana uwezo wa kuzuia madhara endelevu ya sumu husika.

Imani ya kunywa maziwa baada ya kumeza dawa kimakosa, kuvuta vumbi au kemikali yoyote kwa lengo la kuepusha madhara haina mantiki kisayansi. Kwa kuwa maziwa huwa na kampaundi fulani hai zenye nguvu kubwa ya kutengeneza muunganiko, unywaji wa maziwa unaweza kusababisha hatari kubwa zaidi ikiwa aina ya sumu husika itakuwa na kampaundi shikizi, zenye uwezo wa kuungana na maziwa.

Kwa maana hiyo, mgonjwa aliyemeza sumu anapaswa kuwahishwa mapema hospitalini ili achunguzwe na kupatiwa msaada wa haraka kuokoa uhai wake.

Huduma ya kwanza kwa mhanga wa sumu
  • Usimlazimishe mgonjwa kutapika, unaweza kuziba mfumo wa hewa na kusababisha kifo.
  • Kama hapumui, msaada wa usaidizi wa upuaji (CPR) wa haraka unahitajika.
  • Kama kameza hiyo sumu, akorogewe na kunyweshwa mkaa uliounguzwa kwenye hewa (Activated charcoal)
  • Kama sumu ipo kwenye macho, yasafishe haraka kwa maji tiririka kwa dakika 20.
  • Kama sumu ipo kwenye ngozi, mvue nguo alizovaa, kisha msafishe kwa maji safi kwa dakika zisizopungua 15.
  • Kama kaivuta kupitia hewa, mhamishie kwenye eneo lililo na hewa safi.
Jitahidi kugundua aina ya sumu hiyo haraka kisha mpeleke hospitalini kwa huduma zaidi.
Kuna mtu humu sijui ni Prof kama sijakosea anatokea pale kileleni jalalani, alikanusha kabisa hii habari
 
Ahsante sana kwa elimu hii. Watu wengi tumekariri kuwa maziwa ni dawa ya kuondoa sumu mwilini. Yatupasa kuwa makini sana.
 
Umewahi kunywa sumu yoyote ile kimakosa kisha baadhi ya watu wakakushauri utumie maziwa fresh kama sehemu ya tiba?


Madai ya maziwa fresh kuwa na uwezo wa kuondoa sumu mwilini yamekuwepo wa muda mrefu. Katika kujadili ufanisi wake, mdau mmoja wa JamiiForums.com amekosoa vikali tiba hii kwa kusema kuwa maziwa hayana uwezo wowote katika kuondoa sumu.

Amewashauri watanzania kuacha kufanya mambo kwa mazoea pasipo kuwa na uhakika kwanza wa jambo husika.

Taarifa za kitabibu zinasemaje kuhusu nadharia ya uwezo wa maziwa katika kudhibiti/kutibu sumu mwilini?
Tuelezee huo mkaa unachafanya kupambana na sumu.
 
Tuelezee huo mkaa unachafanya kupambana na sumu.
Mkuu kwa bahati mbaya baadhi ya maneno ya kisayansi hayana tafsiri rasmi kwa kiswahili hivyo naomba univumilie.

Kiufupi, mkaa huo huwa kama sumaku, huvuta sumu na kuizuia isisambae mwilini. Jaribu kukumbuka namna sumaku huvuta vipande vya chuma kisha ifanye kuwa mkaa, vile vyuma ndio sumu.
 
Duh hii ni uzushi aiseee mbona inatumika tangu zamani
Ukinywa maziwa na be una usumu mwilini yana kawaida ya kubadirika yanakufanya kitu mbaya utasikizia tumbo linavyofanya, maziwa ni chakula sio dawa km asali ndio maana wenye akili hunywa maziwa yalichanganywa na asili ingawa nayo pia ikikutana na kompaundi za sumu zinazosigana huko tumboni utaimba hallelujah
 
Mkuu kwa bahati mbaya baadhi ya maneno ya kisayansi hayana tafsiri rasmi kwa kiswahili hivyo naomba univumilie.

Kiufupi, mkaa huo huwa kama sumaku, huvuta sumu na kuizuia isisambae mwilini. Jaribu kukumbuka namna sumaku huvuta vipande vya chuma kisha ifanye kuwa mkaa, vile vyuma ndio sumu.
Wewe mwambie mkaa huu huu wa kibaba anasaga unga unga anaweka kwenye glass na maji koroga mnyweshe mgonjwa, kingine ni Mlonge majani ya Mlonge ni bonge la tiba ya sumu mwilini ukinywa juice yake au ukitafuna majani yake basi sumu zote zitafyonzwa mwilini na utakua msafi Ila utaharisha vibaya sana na hio ndio pona yako

NB: Mlonge una viondoa sumu 46
 
Ngoja nifafanue kidogo watu waelewe

Mtu anapokunywa sumu na sumu ikishaanza kusambaa mwilini husambaa kwa Kasi kwa hio

Huduma bora ya kwanza ni kupunguza sumu haraka iwezekanavyo. Sio kuondoa sumu au kutibu sumu. Kupunguza maana yake sumu uingia kwa wingi na huanza kusambaa kwa wingi.

Kwa asidi au alkali (bases), mpe mgonjwa maji au ikiwezekana maziwa au ice cream - kikombe kimoja (1) kwa waathirika chini ya miaka mitano (5); au glasi moja (1) hadi mbili (2) kwa wagonjwa zaidi ya miaka mitano (5).

Kila kitu kinachoimarisha kinga ya mwili wako kitasaidia kwa namna fulani kupunguza na kuondoa sumu mwilini. Ikiwa ni bora kula mboga na matunda safi ya kutosha ili kuimarisha Kinga ya mwili.

Na kwa sababu hiyo hiyo inapaswa kuwa bora kunywa maziwa ya binadamu (sio ya Ng'ombe) kabla ya maziwa mengine yoyote pale unapokua umekunywa sumu.

Maziwa au ice cream ni bora kuliko maji kwa sababu hupunguza na husaidia kuondoa sumu mwilini.

Maji hupunguza sumu tu.

Maziwa au Ice cream hufanya dilution & neutralization of poisoning, hii Ina maana kwamba maziwa sio dawa Ila ni huduma ya kwanza, utasikia mpe maziwa! Mpe maziwa!
 
Mara nyingi watu wanaofanya kazi kwenye kazi za kutimua vumbi kama kukoroga zege/kuchanganya mchanga na cement, ujenzi wa barabara kwenye vumbi nk, wanatumia maziwa eti yanasaidia kuzuia kifua kuuma/magonjwa ya kifua kutokana na vumbi. Je dhana hiyo ni kweli na kama ni kweli maelezo ya kisayansi ni yapi?
 
Mganga Mungu Mitishamba imani.

Maziwa kuondoa vumbi ni imani tu.
Nimejaribu kufanya online search sijapata hint yoyote kuwa yanatibu. Soma hiki kipande

The fallacy remains so entrenched that many workers, even the enlightened ones, believe that milk has the ability to dislodge inhaled dust. The basis of this belief is difficult to understand, because physiologically there is nothing to suggest that milk can do this
 
Nimejaribu kufanya online search sijapata hint yoyote kuwa yanatibu. Soma hiki kipande

The fallacy remains so entrenched that many workers, even the enlightened ones, believe that milk has the ability to dislodge inhaled dust. The basis of this belief is difficult to understand, because physiologically there is nothing to suggest that milk can do this

Watu tunaangamia kwa kukosa maarifa ,bora wewe umejiuliza,watu wanalishana matango pori ni kuamini.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom