Madai ya fidia ya dola milioni Moja ya Erick Kabendera dhidi ya Vodacom yakienda mahakamani tutarajie nini?

FbUser

JF-Expert Member
Oct 22, 2014
431
626
Mimi kwa uzoefu wangu wa kesi za jinai na madai, naona kuna vitu vya kisheria vitajitokeza au kuibuliwa kabla ya kesi ya msingi maana hatujui Kabendera atafungua Shauri la kudai fidia la aina gani. Je, ni la madhara ya kimadai? (Tortious Liability), je ni madhara ya kijinai? (Criminal Liability and Tresspass to person).

Mdai atakuwa na ushahidi gani iwapo Vodacom wanao utetezi wa kutakiwa kushirikiana na Jeshi la Polisi au Takukuru au TISS kumtia nguvuni mtuhumiwa wa uhalifu. Ndiyo awali niliona umuhimu wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) kuunganishwa. Hata hivyo linaweza kuzuka swali mahakamani namna AG au Serikali itakavyounganishwa. Mdai akiomba kurekebisha hati ya mashitaka kumuingiza AG, ataambiwa kuishitaki Serikali lazima kuanza na notisi ya siku 90 hivyo mashitaka yaondolewe yote akaanze upya. Atakapoanza na hiyo notisi, atapigwa PO (Preliminary Objection on Point of Law) kwamba kesi za madhara (law of tort) hufunguliwa Mahakama Kuu ndani ya miaka mitatu tangu madhara yapotokea.

Kwa Wakili wa Serikali na Wakili wa Vodacom ataomba mahakama iondoe àu kufuta hiyo kesi kwani ni imepitwa na muda (the suit is time barred). Maana ktk hali halisi tangu 2019 to 2024 ni zaidi ya miaka mitatu. Mdai na wakili wake wanaweza kuomba kuongezewa muda na kuzingatia muda uliopotea wakati akiwa mahabusu gerezani. Kwa hiyo, Wakili Madeleka na Mteja wake Kabendera, watakutana vikwazo vingi vya kiufundi (legal technicalities) vya namna hiyo. Kuna kuchoshana kwa mapingamizi mengi ya kisheria wakati shauri la msingi linasumama kuanza.

Halafu kwa kumbukumbu zangu Vodacom haijawahi kushindwa kesi za namna hii kwani ina misuli ya kifedha na wanahisa wazito wafanyabiashara wakubwa na viongozi wastaafu wazito wenye ushawishi mkubwa!!!

AAK Jnr, SC, Esq.
27th April 2024
19:42 Hrs EAT


Pia soma: Erick Kabendera aitaka Vodacom imlipe Dola Milioni 1 kwa kufanikisha kutekwa kwake 2019
 
Nchi ambayo ni corrupted!!!Ndio maana wanapandisha vifurushi kila wakati huku wakijua nchi haifuati sheria!!!Namshauri mwanasheria na jopo lake waende kimataifa zaidi ili Vodacom wakomeshwe Kwa kutoa Siri za wateja ambao ni Sisi .Kisheria hilo ni kosa kubwa ,nakushauri kabendera nenda UK ,AMERICA haitapita hata wiki moja Kwa Tanzania watakimbia haraka sana .Vitendo wanavyofanya hawa makampuni ya simu kwa Raia wa Tanzania ni dhambi kubwa ambayo CCM na wahuniiiiii wengine wanatumika kuwakandamiza Raia .Tumeona kesi ya MBOWE mtandao hii ya simu imekuwa kondom ya kupitishia ujinga na uharamia wake !!Halafu kesho utasikia tunataka wawekeza ?Mwekezaji gani ambaye atakuja kwenye nchi ambayo hakuna haki zinazofuatwa au sheria?KATIBA MPYA NI SASA
 
Corrupt n
Nchi ambayo ni corrupted!!!Ndio maana wanapandisha vifurushi kila wakati huku wakijua nchi haifuati sheria!!!Namshauri mwanasheria na jopo lake waende kimataifa zaidi ili Vodacom wakomeshwe Kwa kutoa Siri za wateja ambao ni Sisi .Kisheria hilo ni kosa kubwa ,nakushauri kabendera nenda UK ,AMERICA haitapita hata wiki moja Kwa Tanzania watakimbia haraka sana .Vitendo wanavyofanya hawa makampuni ya simu kwa Raia wa Tanzania ni dhambi kubwa ambayo CCM na wahuniiiiii wengine wanatumika kuwakandamiza Raia .Tumeona kesi ya MBOWE mtandao hii ya simu imekuwa kondom ya kupitishia ujinga na uharamia wake !!Halafu kesho utasikia tunataka wawekeza ?Mwekezaji gani ambaye atakuja kwenye nchi ambayo hakuna haki zinazofuatwa au sheria?KATIBA MPYA NI SASA
Mjingq kama babayako ndio maana unakesha huku mitandaoni tu ,namwonea huruma mamayako alieza kinyesi kama wewe.
 
Corrupt n

Mjingq kama babayako ndio maana unakesha huku mitandaoni tu ,namwonea huruma mamayako alieza kinyesi kama wewe.
Nchi hii rais ndio anaamua sheria zifuatwe vipi. Hakuna haki yoyote atapata huyo Kabendera maana yale maagizo yalikuwa ni maagizo ya mlevi wa madaraka Magufuli. Kabendera akitaka aende mahakama za kimataifa, huko atapata haki yake.
 
Sidhani kama Kabendera anatarajia kupata hiyo milioni moja.

Anachokitaka ni ukweli kuwa wazi, kesi ikiwa mahakamani watu watalazimika kutoa ushahidi chini ya kiapo, vielelezo vitalazimika kuletwa, na mambo mengi ya siri yatakuwa wazi.
 
Sidhani kama Kabendera anatarajia kupata hiyo milioni moja.

Anachokitaka ni ukweli kuwa wazi, kesi ikiwa mahakamani watu watalazimika kutoa ushahidi chini ya kiapo, vielelezo vitalazimika kuletwa, na mambo mengi ya siri yatakuwa wazi.
Waliomtia nyavuni kipindi hicho hawana nguvu za kumfikia kipindi hiki?
 
Mimi kwa uzoefu wangu wa kesi za jinai na madai, naona kuna vitu vya kisheria vitajitokeza au kuibuliwa kabla ya kesi ya msingi maana hatujui Kabendera atafungua Shauri la kudai fidia la aina gani. Je, ni la madhara ya kimadai? (Tortious Liability), je ni madhara ya kijinai? (Criminal Liability and Tresspass to person).

Mdai atakuwa na ushahidi gani iwapo Vodacom wanao utetezi wa kutakiwa kushirikiana na Jeshi la Polisi au Takukuru au TISS kumtia nguvuni mtuhumiwa wa uhalifu. Ndiyo awali niliona umuhimu wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) kuunganishwa. Hata hivyo linaweza kuzuka swali mahakamani namna AG au Serikali itakavyounganishwa. Mdai akiomba kurekebisha hati ya mashitaka kumuingiza AG, ataambiwa kuishitaki Serikali lazima kuanza na notisi ya siku 90 hivyo mashitaka yaondolewe yote akaanze upya. Atakapoanza na hiyo notisi, atapigwa PO (Preliminary Objection on Point of Law) kwamba kesi za madhara (law of tort) hufunguliwa Mahakama Kuu ndani ya miaka mitatu tangu madhara yapotokea.

Kwa Wakili wa Serikali na Wakili wa Vodacom ataomba mahakama iondoe àu kufuta hiyo kesi kwani ni imepitwa na muda (the suit is time barred). Maana ktk hali halisi tangu 2019 to 2024 ni zaidi ya miaka mitatu. Mdai na wakili wake wanaweza kuomba kuongezewa muda na kuzingatia muda uliopotea wakati akiwa mahabusu gerezani. Kwa hiyo, Wakili Madeleka na Mteja wake Kabendera, watakutana vikwazo vingi vya kiufundi (legal technicalities) vya namna hiyo. Kuna kuchoshana kwa mapingamizi mengi ya kisheria wakati shauri la msingi linasumama kuanza.

Halafu kwa kumbukumbu zangu Vodacom haijawahi kushindwa kesi za namna hii kwani ina misuli ya kifedha na wanahisa wazito wafanyabiashara wakubwa na viongozi wastaafu wazito wenye ushawishi mkubwa!!!

AAK Jnr, SC, Esq.
27th April 2024
19:42 Hrs EAT


Pia soma: Erick Kabendera aitaka Vodacom imlipe Dola Milioni 1 kwa kufanikisha kutekwa kwake 2019
Akishinda Kesi tutarajie kwamba watumiaji wa huduma za mitandao ya simu privacy zao zitalindwa kikamilifu. Watoa huduma za mitandao ya simu wataongeza umakini ktk kulinda taarifa za wateja wao dhidi ya uharamia wa kimtandao.
 
Back
Top Bottom