Myebusi Mweusi
JF-Expert Member
- Jan 23, 2022
- 669
- 1,516
NANAOMBA USHAURI
Habari yako mwana JF mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 30 ninafanya kazi ya bodaboda
Nilikuwa na mpenzi wangu niliyeishi nae kwa miaka 4 sasa na tuna ahadi ya kuoana
Lakini mwaka juzi nilipata abiria MAMA mtu mzima ana miaka kama 45 ni mtu anayejiheshimu na anafanya kazi ya kuuza genge (matunda,nyanya, dagaa na vitu vyengine) tulianza mahusiano ya kibiashara kama bodaboda wake kisha akawa mshauri wangu yaani nikipata tatizo la kutaka ushauri huwa namuona yeye na ananishauri vizur mno maisha yamekwenda hadi akawa mpenzi wangu
Tokea tuwe wapenzi amekuwa mtu muhimu sana katika maisha yangu amenishaur mambo mengi hadi sasa najiona nimepiga hatua kubwa ya kimaisha mwanzoni nilikuwa na pikipiki moja lakin sasa hivi ninazo mbili na pia nimefungua biashara ya kuuza chips na pia nimefungua machine za kuuza juice ya miwa ninakwambia ukweli kabisa mawazo yote haya yametoka kwa huyu mwanamke. Mwanzoni hela yote nilikuwa naimaliza kwa mirungi, kubeti na pombe nashukuru kwa ushauri wake mirungi na kubeti nimeacha kabisa pombe nayo naelekea kuacha kabisa haya yote ni mawazo yake na ushauri wake
Changamoto imekuja kuwa anataka tuoane na mimi sijawahi kumwambia kuwa nina mpenzi mwengine kwa sababu mara nyingi huwa nina lala kwake (mpenzi wangu anaishi kwao)
Napata wakati mgumu wa kufanya maamuzi nifanyeje??
Nampenda huyu Mama kutokana naamini nikiendelea kuwa nae maisha yangu yatazidi kuwa mazuri kutokana na mawazo yake
Lakini pia yule mpenzi wangu nae nampenda sana na ananipenda na nyumbani kwao wananijua japo sio rasmi
WOTE NAWAPENDA SIJUI NIFANYE NINI??
Habari yako mwana JF mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 30 ninafanya kazi ya bodaboda
Nilikuwa na mpenzi wangu niliyeishi nae kwa miaka 4 sasa na tuna ahadi ya kuoana
Lakini mwaka juzi nilipata abiria MAMA mtu mzima ana miaka kama 45 ni mtu anayejiheshimu na anafanya kazi ya kuuza genge (matunda,nyanya, dagaa na vitu vyengine) tulianza mahusiano ya kibiashara kama bodaboda wake kisha akawa mshauri wangu yaani nikipata tatizo la kutaka ushauri huwa namuona yeye na ananishauri vizur mno maisha yamekwenda hadi akawa mpenzi wangu
Tokea tuwe wapenzi amekuwa mtu muhimu sana katika maisha yangu amenishaur mambo mengi hadi sasa najiona nimepiga hatua kubwa ya kimaisha mwanzoni nilikuwa na pikipiki moja lakin sasa hivi ninazo mbili na pia nimefungua biashara ya kuuza chips na pia nimefungua machine za kuuza juice ya miwa ninakwambia ukweli kabisa mawazo yote haya yametoka kwa huyu mwanamke. Mwanzoni hela yote nilikuwa naimaliza kwa mirungi, kubeti na pombe nashukuru kwa ushauri wake mirungi na kubeti nimeacha kabisa pombe nayo naelekea kuacha kabisa haya yote ni mawazo yake na ushauri wake
Changamoto imekuja kuwa anataka tuoane na mimi sijawahi kumwambia kuwa nina mpenzi mwengine kwa sababu mara nyingi huwa nina lala kwake (mpenzi wangu anaishi kwao)
Napata wakati mgumu wa kufanya maamuzi nifanyeje??
Nampenda huyu Mama kutokana naamini nikiendelea kuwa nae maisha yangu yatazidi kuwa mazuri kutokana na mawazo yake
Lakini pia yule mpenzi wangu nae nampenda sana na ananipenda na nyumbani kwao wananijua japo sio rasmi
WOTE NAWAPENDA SIJUI NIFANYE NINI??