bagabe
JF-Expert Member
- May 8, 2014
- 483
- 603
Wakuu kuna binti nimekua nae kwenye mahusiano almost miaka mitano. Tumepitia changamoto nyingi kwenye maisha lakini still tuko pamoja. Sababu kubwa iliyonileta hapa ni kuomba ushauri wenu ndugu zangu juu ya hili suala.
Huyu binti nimeshatoa barua kwao ilibaki mahali tu ili nifunge nae pingu za maisha. Aliamua kuhamia kwangu mazima tutafute maisha wote huku mambo mengine yakiendelea.
Lakini nilitoa barua kutokana na shinikizo la mtoto alijifingua bahati mbaya akafariki nikaona nitoe barua kwao kuonesha uungwana. Sasa kwa kipindi chote nimeishi nae nimegundua sina hisia nae kabisa yani akili yangu ipo kutoka nje ya huu mfumo nataka niwe huru.
Nadhani ujauzito ulikua shinikizo kubwa sana la mimi kua karibi nae. Tatizo linakuja tayari anajulikana na familia yangu yote na kila mtu wangu wa karibu anamjua na mimi kila mtu wao wa karibu ananijua.
Naombeni ushauri nataka nianze maisha yangu mapya bila uwepo wake ila sina pa kuanzia niafanyaje ndugu zangu wana JF?
Huyu binti nimeshatoa barua kwao ilibaki mahali tu ili nifunge nae pingu za maisha. Aliamua kuhamia kwangu mazima tutafute maisha wote huku mambo mengine yakiendelea.
Lakini nilitoa barua kutokana na shinikizo la mtoto alijifingua bahati mbaya akafariki nikaona nitoe barua kwao kuonesha uungwana. Sasa kwa kipindi chote nimeishi nae nimegundua sina hisia nae kabisa yani akili yangu ipo kutoka nje ya huu mfumo nataka niwe huru.
Nadhani ujauzito ulikua shinikizo kubwa sana la mimi kua karibi nae. Tatizo linakuja tayari anajulikana na familia yangu yote na kila mtu wangu wa karibu anamjua na mimi kila mtu wao wa karibu ananijua.
Naombeni ushauri nataka nianze maisha yangu mapya bila uwepo wake ila sina pa kuanzia niafanyaje ndugu zangu wana JF?