Mzee wa old school
JF-Expert Member
- May 16, 2021
- 578
- 919
Jana jioni kabla ya usingizi nilikuwa natafari kwa kujilaumu na kulalama... Nakuona kuwa maisha ni magumu sana, niliumia zaidi kuona watoto na mke wananitegemea, wazazi pia tena zaidi wanaamini kijana wetu msomi... Daaaah!
Nikapiga hesabu muda niliotumia shule... Miaka 7 msingi + miaka 4 sekondari + jumlisha miaka 3 diploma au 2 kwa kidato cha sita + 3, 4 au 5 degree kutegemea na course uliyo soma.
Sasa hapa tufanye mtu kapita form six 2 miaka na chuo miaka 3
7+4+2+3= 16
Tufanye umeanza shule na miaka 7.. sasa hiyo 7+16 = 23.
Hebu fikiria hadi unamaliza shule una miaka 23... Hujaanza maisha zaidi ya kujitia msomi, huna maarifa ya kazi za mikono kwa madai ya kwamba hizo kazi za wasio soma.... Sasa sisi TULIO soma tunajua nini? Tunajua newton law? Archimedes principle? Historia ya wazungi kuja kututawala?
Turejee kwenye mada... Sasa umri huo wa miaka 23 kijana deni board ya MKOPO limefika mil 25, Hana kazi, Hana mbele wa nyuma... Kapambana hapa na pale anakuja kupata kazi ana miaka 30 hadi 35..... Ndo anaanza life... Ile mshahara unsingia tu... Panga linapita shwaaa! Bodi ya MKOPO..... Mshahara anaanza kupokea nusu.. mara huku pay as you earn, mara chama cha wafanya kazi n.k,, kuja kushtuka umri umeenda kabakiza miezi 2 astahafu...
PENDEKEZO/TUJIULIZE
1.Kwanini serikali isupunguze muda wa wanafunzi kukaa mashuleni?
2. Kwanini wizara husika isibadili mtaala wa elimu?
Vyote viwili ni muhimu.
Tuanze na 1. Muda wa miaka kwa wanafunzi upungue kukaa mashuleni.. badala ya miaka 16 walau basi miaka 10.
Badala mtoto aanze shule ya msingi miaka 7 basi aanze na miaka 4, yaani miaka 4 chekechea akiwa na 5 anaanza shule ya msingi. Hadi miaka 8 kamaliza shule ya msingi, miaka 11 kamaliza sekondari baada ya hapo college ama chuo cha kati kusoma ujuzi miaka 2 na akitaka degree sasa hapo ndo yeye miaka 3 na kuendelea... Akimaliza college ana miaka 13 walau ana muda wa kujitafuta na kama akiendelea degree atamaliza na miaka ,16 walau bado tena ana muda.. na zile kozi za miaka kama udaktari atamaliza akiwa na miaka 18 bado muda anao....
Kwa minajiri hiyo basi, miaka ya madarasa iwe hivi.
*Chekechea mwaka 1
*Msingi miaka 4
*Sekondari 3
*Chuo cha kati yaani college miaka 2
* Chuo kikuu miaka 3 hadi 5
Jambo la 2. Kwa nini wizara husika isibadili mtaala wa elimu? Badala watu kusoma nadharia wasomee wakiwa karakana, mahospitali, mahakamani, viwandani, masomoni n.k? Kama ni historia basi tusome historia yetu ya kweli.... Yenye asili yetu! Badala ya kusoma dawa za wazungu... Kwa nini tusitumie miti Mungu alotupatia tuongeze elimu ya madawa na matibabu ya kikwetu? Kwanini China Russia waliweka utaratibu wao na waliweza?
Hebu viongozi fikirieni nje ya box....
Mfano wa kweli: siku moja shileni kwetu wazungu kutoka nchi Fulani walitutembelea(maana ile ilikuwa shule ya diocese Fulani) katika kujitambulisha kuna mmoja alisema wasifu wake kwamba anasoma masters ya chemistry halafu alikuwa na miaka 18... Wakati shileni kuna mijamaa ipo form ina miaka 18 na mengine form 6 ina miaka 19 hadi 20....
Ni hayo tu.... Moderator wakati mwingine huwa anaficha post zangu watu hawaoni... Basi naomba huu muuruhusu
Nikapiga hesabu muda niliotumia shule... Miaka 7 msingi + miaka 4 sekondari + jumlisha miaka 3 diploma au 2 kwa kidato cha sita + 3, 4 au 5 degree kutegemea na course uliyo soma.
Sasa hapa tufanye mtu kapita form six 2 miaka na chuo miaka 3
7+4+2+3= 16
Tufanye umeanza shule na miaka 7.. sasa hiyo 7+16 = 23.
Hebu fikiria hadi unamaliza shule una miaka 23... Hujaanza maisha zaidi ya kujitia msomi, huna maarifa ya kazi za mikono kwa madai ya kwamba hizo kazi za wasio soma.... Sasa sisi TULIO soma tunajua nini? Tunajua newton law? Archimedes principle? Historia ya wazungi kuja kututawala?
Turejee kwenye mada... Sasa umri huo wa miaka 23 kijana deni board ya MKOPO limefika mil 25, Hana kazi, Hana mbele wa nyuma... Kapambana hapa na pale anakuja kupata kazi ana miaka 30 hadi 35..... Ndo anaanza life... Ile mshahara unsingia tu... Panga linapita shwaaa! Bodi ya MKOPO..... Mshahara anaanza kupokea nusu.. mara huku pay as you earn, mara chama cha wafanya kazi n.k,, kuja kushtuka umri umeenda kabakiza miezi 2 astahafu...
PENDEKEZO/TUJIULIZE
1.Kwanini serikali isupunguze muda wa wanafunzi kukaa mashuleni?
2. Kwanini wizara husika isibadili mtaala wa elimu?
Vyote viwili ni muhimu.
Tuanze na 1. Muda wa miaka kwa wanafunzi upungue kukaa mashuleni.. badala ya miaka 16 walau basi miaka 10.
Badala mtoto aanze shule ya msingi miaka 7 basi aanze na miaka 4, yaani miaka 4 chekechea akiwa na 5 anaanza shule ya msingi. Hadi miaka 8 kamaliza shule ya msingi, miaka 11 kamaliza sekondari baada ya hapo college ama chuo cha kati kusoma ujuzi miaka 2 na akitaka degree sasa hapo ndo yeye miaka 3 na kuendelea... Akimaliza college ana miaka 13 walau ana muda wa kujitafuta na kama akiendelea degree atamaliza na miaka ,16 walau bado tena ana muda.. na zile kozi za miaka kama udaktari atamaliza akiwa na miaka 18 bado muda anao....
Kwa minajiri hiyo basi, miaka ya madarasa iwe hivi.
*Chekechea mwaka 1
*Msingi miaka 4
*Sekondari 3
*Chuo cha kati yaani college miaka 2
* Chuo kikuu miaka 3 hadi 5
Jambo la 2. Kwa nini wizara husika isibadili mtaala wa elimu? Badala watu kusoma nadharia wasomee wakiwa karakana, mahospitali, mahakamani, viwandani, masomoni n.k? Kama ni historia basi tusome historia yetu ya kweli.... Yenye asili yetu! Badala ya kusoma dawa za wazungu... Kwa nini tusitumie miti Mungu alotupatia tuongeze elimu ya madawa na matibabu ya kikwetu? Kwanini China Russia waliweka utaratibu wao na waliweza?
Hebu viongozi fikirieni nje ya box....
Mfano wa kweli: siku moja shileni kwetu wazungu kutoka nchi Fulani walitutembelea(maana ile ilikuwa shule ya diocese Fulani) katika kujitambulisha kuna mmoja alisema wasifu wake kwamba anasoma masters ya chemistry halafu alikuwa na miaka 18... Wakati shileni kuna mijamaa ipo form ina miaka 18 na mengine form 6 ina miaka 19 hadi 20....
Ni hayo tu.... Moderator wakati mwingine huwa anaficha post zangu watu hawaoni... Basi naomba huu muuruhusu