Dalton elijah
JF-Expert Member
- Jul 19, 2022
- 216
- 478
Kampuni hiyo kutoka China imekuwa ikitumia teknolojia inayoiga akili ya binadamu (AI technology) kubuni nafsi ya kidijitali ya aliyefariki na kuwezesha jamaa zake kuwasiliana naye jinsi ilivyokuwa kabla ya kufa kwake.
Teknolojia hiyo imesifiwa na wengi kwa kuwa inawapa waliofiwa faraja ya muda, hasa wakati huu China inapoadhimisha tamasha la kumbukumbu ya wafu maarufu kama "Qingming Festival."
^ME