Mwalimu wa Zamu Tz
JF-Expert Member
- Jan 2, 2021
- 1,041
- 2,717
Utangulizi.
Habari wanajamvi.Katika karne hii ya Teknolojia na Utandawazi,asilimia kubwa ya watu hutamani kujitupa kwenye Uandishi wa habari.Uwepo wa mitandao ya kijamii ndio umezidi kurahisisha uwasilishwaji wa habari.hii inapelekea kila mtu atamani kutoa habari bila kujali amesomea au hajasomea ilimradi tu awe wa kwanza kutoa 'habari za hivi punde' (Breaking news).Yapo mambo mengi yanayoiathiri Sekta hii nyeti ya uandishi wa habari.
CHANGAMOTO ZINAZOKUMBA UANDISHI WA HABARI.
1.Uwasilishwaji mbovu wa habari.
uandishi wa habari ni sekta inayohitaji Nia.Waandishi wengi wamekosa NIA ya kutafuta habari nyeti na maarifa.Mwandishi anapaswa atafute ukweli afanye Tafiti za kutosha kabla ya kutoa habari.Bahati mbaya Waandishi wengi wanakosa Nia na hivyo kupelekea wengi kuweka Taarifa za kukurupuka na kuigiliziana(copy&paste) bila kuhakiki kama inaukweli.
2.Uwezo mdogo wa uandishi(writting skills).
Waandishi wengi wanauwezo mdogo wa uandishi.ikiwemo kuchanganya herufi kubwa na ndogo,Kutopanga kazi katika mpangilio,Unasoma habari huelewi mwanzo na mwisho wake.Makosa ya kiuandishi(Typing error) na makosa ya kisarufi
3.Wanahabari kukosa jukwaa(Platform) binafsi.
Hapa kuna mambo ya kuelewa kidogo.Hasa waandishi waliojariwa wanakosa Jukwaa.Mfano waandishi mashuhuri duniani kama mwanamama Christiane Amanpour,Bob Woodward utakuta wana blog zao ambazo ndio majukwaa yao ya kuweka habari zao nje ya vituo vy Habari.Mambo ni tofauti kwetu unakuta mwanahabari hana platform(Website/Blog/Application n.k).Platform sio kuwa na Akaunti za mitandao ya kijamii tu.
4.Uanzishwaji holela wa vyombo vya habari maarufu kama 'Online Tv'
Kuna haja ya mamlaka(TCRA) kufanyia kazi sheria ya usajili wa vyombo vya habari.Kwasasa hali inazidi kuwa mbaya kila atakaejisikia tu anafungua TV yake youtube na kuanza kazi ya kutupatia habari.Hii ni hatari sana kwani Taarifa za upotoshaji zinakuwa kwa kasi kutokana na wanahabari hawa wasio na vigezo na wasiofata masharti.
5.Uwezo mbovu wa kufanya mahojiano.(Interviewing skills)
Waandishi wengi wamekosa maarifa ya mahojiano(Interview).Unaweza kusikiliza au kuangalia mahojiano ukaishia kunung'unika tu.Waandishi wana uwezo mdogo wa kuuliza maswali ya kiudadisi na wengine kushindwa kuuliza maswali ya msingi.
6.Wanahabari wasio na taaluma ya uandishi wa habari
Mwandishi mashuhuri Anderson Cooper alinukuliwa akisema "....Sio kila mwanahari ni mwandishi wa habari,lakini kila mwandishi wa habari anaweza kuwa mwanahabari..." Akimaanisha Uandishi wa habari ni Taaluma na sio kila mtu anaweza kuwa nayo.Unakuta mtu hana taaluma ya michezo ila kaajiriwa kama mchambuzi wa michezo.
7.Wanahabari wengi kukosa ubunifu
Uandishi ni sanaa,Na sanaa ni Ubunifu.Waandishi wengi wanakosa ubunifu wa kazi yao.Unakuta akishaajiriwa anafata njia zilezile za aliowakuta na mwisho huishia hapohapo bila kutafakari 'Nje ya boksi' Ubunifu huu ni pamoja na kutembelea maeneo mbalimbali na kutafuta maarifa zaidi.
8.Kuchangia mmomonyo wa maadili na Tamaduni za mwaafrika.
Kupitia Uandishi wa habari.Kumekuwa na upotoshaji na kuchangia kuongezeka mmomonyoko wa maadili.Kuanzia mavazi,Tamthilia zioneshwazo na kuhamasisha kamari.Ukiuliza kwanini vituo vingi vinahamasisha Kamari utaambiwa ni vyanzo vya mapato.Hii haikubaliki ndipo tunaporudi kwenye pointi ya 7(kukosa ubunifu) hivyo vituo vyote vinahamasisha vitendo vya kamari.
9.Jinamizi la Matabaka.
Katika uandishi kuna Jinamizi hatari limeibuka na kuikuma Sekta hii adhimu ya habari.Unakuta kituo A kinajipendekeza kwa chama X cha Siasa na kituo B vivyo hivyo.Kama sio siasa utakuta Kituo A au waandishi hujipendekeza kwa timu X za Soka au viongozi wa nchi.Hii ni hatari sana na imekuwa ikisababisha Matabaka.Pia utakuta kituo X kinaajiri kwa ukabila au udini hii pia haifai hata kidogo.
10.Kukosa msimamo na kutojua mipaka ya kazi.
Kwenye Tasnia ya habari wapo watakaokutikisa 'kukutoa relini' vilevile wapo watakaokulipa pesa au Mali ili tu upotoshe au utoe habari kwa matakwa yao.Hivyo kukosa misimamo na mipaka ya kazi kumepelekea waandishi wengi kukamatika kwenye mtego huo.
11.Kukosa umahiri,Nia na kutojiamini
Kwanza lazima utambue usipojiamini basi na hadhira unayoifikishia ujumbe haitokuamini kamwe.Umahiri ni pamoja na kuzingatia Muda na kufata ratiba(panctuality),Kuwa mcheshi na mkarimu.Vilevile kuwa na heshima na maadili ya kazi ya uandishi wa Habari.
.Kwa bahati mbaya jinamizi limekumba waandishi wengi.Hawajali muda na ratiba,Hawana heshima na sio waugwana.
NINI KIFANYIKE?
•Mamlaka husika zisimamia uendeshwaji wa vyombo vya habari ipasavyo.
Ikiwemo kusimamia usajili wa vyombo vya habari.Kufanya tathmini ya uwezo wa wanahabari hao wanaotaka kuanzisha 'online TV'
•Kuhakikisha sheria za habari zinafatwa
Vilevile,Mamlaka ihakiki Sheria za Habaru zinafatwa bila shuruti.Na kutoa onyo au Adhabu kali kwa wanahabari au wasio wanahabari wavunjapo sheria.Hii itasaidia kutoacha sintofahamu kwenye jamii kutokana na habari za upotoshaji
•Kuwa na nidhamu,Heshima na uadilifu katika kazi.
Hapa itawahusu wanahabari walioajiriwa kwenye vyombo rasmi.Kuepuka dharau na majigambo wanapokuwa hewani kwenye vipindi. vilevile kuhakikisha utiifu na unadhifu wa mavazi katika vipindi vinavyorushwa hewani.
•Vyombo viajiri watu wenye taaluma ya uwanahabari na vitoe fursa kwa wanahabari wapya.
Ni muhimu vyombo kuajiri watu wenye ubobevu badala kuajiri watu wenye porojo na majina tu.Kuna waandishi mahiri sana wanakosa kazi kutokana na utitiri wa vyombo kuajiri watu wasio na taaluma ya habari kwa ujumla.
•Kuwe na mashindano ya mwanahabari bora.
Kuanzishwe mashindano ambapo wanahabari watashiriki na washindi watapewa Tuzo.Hii itakuwa kama chachu ya maendeleo kwenye Tasnia ya Uandishi wa habari.Vilevile kuongeza ubunifu na nidhamu.
.
HITIMISHO.
Ni vyema kwa wanahabari kuzingatia sheria na kujua mipaka yao katika kazi.Pia wawe na misimamo na wasioneshe kuegemea upande fulani wa kisiasa,kidini au tamaduni.Tetesi za kwamba wanahabari wananyimwa uhuru sio za kweli.Ni vile wanahabari wengi tunakosa ubunifu wa kazi yetu hivyo kuona kama mamlaka zinatuminya.
Lakini pia,Waandishi watengeneze tabia ya kufanya tafiti na kujua mambo wasiyoyajua.Uwanahabari ni azi ya kutenganisha ukweli na uongo na hivyo kusaidia kutoacha sitofahamu kwenye jamii.
La mwizho,kuhakiki makala ya taarifa,kuhakikisha unasahihisha makosa madogo ya kiuandishi kama makosa ya kisarufi,pia kutumia lugha nyepesi kwenye uwasilishaji wa habari.Habari isiyo na ukweli ndani yake ugeuka Hatari.
Natanguliza shukrani.
Asante kwa kusoma bandiko hili,Naomba kura yako kwa kubonyeza alama ya vote hapo chini.
Habari wanajamvi.Katika karne hii ya Teknolojia na Utandawazi,asilimia kubwa ya watu hutamani kujitupa kwenye Uandishi wa habari.Uwepo wa mitandao ya kijamii ndio umezidi kurahisisha uwasilishwaji wa habari.hii inapelekea kila mtu atamani kutoa habari bila kujali amesomea au hajasomea ilimradi tu awe wa kwanza kutoa 'habari za hivi punde' (Breaking news).Yapo mambo mengi yanayoiathiri Sekta hii nyeti ya uandishi wa habari.
CHANGAMOTO ZINAZOKUMBA UANDISHI WA HABARI.
1.Uwasilishwaji mbovu wa habari.
uandishi wa habari ni sekta inayohitaji Nia.Waandishi wengi wamekosa NIA ya kutafuta habari nyeti na maarifa.Mwandishi anapaswa atafute ukweli afanye Tafiti za kutosha kabla ya kutoa habari.Bahati mbaya Waandishi wengi wanakosa Nia na hivyo kupelekea wengi kuweka Taarifa za kukurupuka na kuigiliziana(copy&paste) bila kuhakiki kama inaukweli.
2.Uwezo mdogo wa uandishi(writting skills).
Waandishi wengi wanauwezo mdogo wa uandishi.ikiwemo kuchanganya herufi kubwa na ndogo,Kutopanga kazi katika mpangilio,Unasoma habari huelewi mwanzo na mwisho wake.Makosa ya kiuandishi(Typing error) na makosa ya kisarufi
3.Wanahabari kukosa jukwaa(Platform) binafsi.
Hapa kuna mambo ya kuelewa kidogo.Hasa waandishi waliojariwa wanakosa Jukwaa.Mfano waandishi mashuhuri duniani kama mwanamama Christiane Amanpour,Bob Woodward utakuta wana blog zao ambazo ndio majukwaa yao ya kuweka habari zao nje ya vituo vy Habari.Mambo ni tofauti kwetu unakuta mwanahabari hana platform(Website/Blog/Application n.k).Platform sio kuwa na Akaunti za mitandao ya kijamii tu.
4.Uanzishwaji holela wa vyombo vya habari maarufu kama 'Online Tv'
Kuna haja ya mamlaka(TCRA) kufanyia kazi sheria ya usajili wa vyombo vya habari.Kwasasa hali inazidi kuwa mbaya kila atakaejisikia tu anafungua TV yake youtube na kuanza kazi ya kutupatia habari.Hii ni hatari sana kwani Taarifa za upotoshaji zinakuwa kwa kasi kutokana na wanahabari hawa wasio na vigezo na wasiofata masharti.
5.Uwezo mbovu wa kufanya mahojiano.(Interviewing skills)
Waandishi wengi wamekosa maarifa ya mahojiano(Interview).Unaweza kusikiliza au kuangalia mahojiano ukaishia kunung'unika tu.Waandishi wana uwezo mdogo wa kuuliza maswali ya kiudadisi na wengine kushindwa kuuliza maswali ya msingi.
6.Wanahabari wasio na taaluma ya uandishi wa habari
Mwandishi mashuhuri Anderson Cooper alinukuliwa akisema "....Sio kila mwanahari ni mwandishi wa habari,lakini kila mwandishi wa habari anaweza kuwa mwanahabari..." Akimaanisha Uandishi wa habari ni Taaluma na sio kila mtu anaweza kuwa nayo.Unakuta mtu hana taaluma ya michezo ila kaajiriwa kama mchambuzi wa michezo.
7.Wanahabari wengi kukosa ubunifu
Uandishi ni sanaa,Na sanaa ni Ubunifu.Waandishi wengi wanakosa ubunifu wa kazi yao.Unakuta akishaajiriwa anafata njia zilezile za aliowakuta na mwisho huishia hapohapo bila kutafakari 'Nje ya boksi' Ubunifu huu ni pamoja na kutembelea maeneo mbalimbali na kutafuta maarifa zaidi.
8.Kuchangia mmomonyo wa maadili na Tamaduni za mwaafrika.
Kupitia Uandishi wa habari.Kumekuwa na upotoshaji na kuchangia kuongezeka mmomonyoko wa maadili.Kuanzia mavazi,Tamthilia zioneshwazo na kuhamasisha kamari.Ukiuliza kwanini vituo vingi vinahamasisha Kamari utaambiwa ni vyanzo vya mapato.Hii haikubaliki ndipo tunaporudi kwenye pointi ya 7(kukosa ubunifu) hivyo vituo vyote vinahamasisha vitendo vya kamari.
9.Jinamizi la Matabaka.
Katika uandishi kuna Jinamizi hatari limeibuka na kuikuma Sekta hii adhimu ya habari.Unakuta kituo A kinajipendekeza kwa chama X cha Siasa na kituo B vivyo hivyo.Kama sio siasa utakuta Kituo A au waandishi hujipendekeza kwa timu X za Soka au viongozi wa nchi.Hii ni hatari sana na imekuwa ikisababisha Matabaka.Pia utakuta kituo X kinaajiri kwa ukabila au udini hii pia haifai hata kidogo.
10.Kukosa msimamo na kutojua mipaka ya kazi.
Kwenye Tasnia ya habari wapo watakaokutikisa 'kukutoa relini' vilevile wapo watakaokulipa pesa au Mali ili tu upotoshe au utoe habari kwa matakwa yao.Hivyo kukosa misimamo na mipaka ya kazi kumepelekea waandishi wengi kukamatika kwenye mtego huo.
11.Kukosa umahiri,Nia na kutojiamini
Kwanza lazima utambue usipojiamini basi na hadhira unayoifikishia ujumbe haitokuamini kamwe.Umahiri ni pamoja na kuzingatia Muda na kufata ratiba(panctuality),Kuwa mcheshi na mkarimu.Vilevile kuwa na heshima na maadili ya kazi ya uandishi wa Habari.
NINI KIFANYIKE?
•Mamlaka husika zisimamia uendeshwaji wa vyombo vya habari ipasavyo.
Ikiwemo kusimamia usajili wa vyombo vya habari.Kufanya tathmini ya uwezo wa wanahabari hao wanaotaka kuanzisha 'online TV'
•Kuhakikisha sheria za habari zinafatwa
Vilevile,Mamlaka ihakiki Sheria za Habaru zinafatwa bila shuruti.Na kutoa onyo au Adhabu kali kwa wanahabari au wasio wanahabari wavunjapo sheria.Hii itasaidia kutoacha sintofahamu kwenye jamii kutokana na habari za upotoshaji
•Kuwa na nidhamu,Heshima na uadilifu katika kazi.
Hapa itawahusu wanahabari walioajiriwa kwenye vyombo rasmi.Kuepuka dharau na majigambo wanapokuwa hewani kwenye vipindi. vilevile kuhakikisha utiifu na unadhifu wa mavazi katika vipindi vinavyorushwa hewani.
•Vyombo viajiri watu wenye taaluma ya uwanahabari na vitoe fursa kwa wanahabari wapya.
Ni muhimu vyombo kuajiri watu wenye ubobevu badala kuajiri watu wenye porojo na majina tu.Kuna waandishi mahiri sana wanakosa kazi kutokana na utitiri wa vyombo kuajiri watu wasio na taaluma ya habari kwa ujumla.
•Kuwe na mashindano ya mwanahabari bora.
Kuanzishwe mashindano ambapo wanahabari watashiriki na washindi watapewa Tuzo.Hii itakuwa kama chachu ya maendeleo kwenye Tasnia ya Uandishi wa habari.Vilevile kuongeza ubunifu na nidhamu.
HITIMISHO.
Ni vyema kwa wanahabari kuzingatia sheria na kujua mipaka yao katika kazi.Pia wawe na misimamo na wasioneshe kuegemea upande fulani wa kisiasa,kidini au tamaduni.Tetesi za kwamba wanahabari wananyimwa uhuru sio za kweli.Ni vile wanahabari wengi tunakosa ubunifu wa kazi yetu hivyo kuona kama mamlaka zinatuminya.
Lakini pia,Waandishi watengeneze tabia ya kufanya tafiti na kujua mambo wasiyoyajua.Uwanahabari ni azi ya kutenganisha ukweli na uongo na hivyo kusaidia kutoacha sitofahamu kwenye jamii.
La mwizho,kuhakiki makala ya taarifa,kuhakikisha unasahihisha makosa madogo ya kiuandishi kama makosa ya kisarufi,pia kutumia lugha nyepesi kwenye uwasilishaji wa habari.Habari isiyo na ukweli ndani yake ugeuka Hatari.
Natanguliza shukrani.
Asante kwa kusoma bandiko hili,Naomba kura yako kwa kubonyeza alama ya vote hapo chini.