Je kwa mtaji wa 2M naweza fungua biashara hizi mbili?

Dogo acha maneno mengi ambayo ni pumba tupu mimi naitwa mnachihanguu nipo soko la mtwara nina duka la viatu na duka la vifaa vya ujenzi na mji wa tunduru nako nina duka la pembejeo za kilimo kwahiyo ninapokuambia kuwa biashara ni mtaji uwe unajua unaeongea nae ni mtu wa aina gani...kama wapo wa mtwara humu watakuwa wanayajua maduka yangu kwasababu ni maarufu hapa sokoni,Mimi sijasomea nadharia za kipuuzi kama zako bali mimi nipo uwanja wa vita kabisa
Mkuu hujui kama hujui unadhani ujuzi mpaka uende kusoma shule ? Hivi hii mada ni ya nani ni mfanyabiashara au ana nini ? Unajua maana ya Ujuzi ? Achana na story za maduka yako hio hapa ni immaterial na wala haimsaidii mtu turudi kwenye mada mimi nimekupa mifano kwanini Ujuzi unatrump Pesa wewe unakuja na hadithi za kwamba hauhitaji ujuzi (kwahio naweza kusema hujui maana ya haya maneno au unadhani mtaji ni Pesa pekee)

By the way kwanini duka lako lipo sokoni au hilo la pembejeo lipo huko lilipo na sio pengine ? (location)...; Kwahio mkuu hata kama wewe ndio ungekuwa ndio mgunduzi wa Biashara duniani au hapa naongea na Mo au Bhakresa au Dangote ukileta story za kwamba ujuzi hauna faida kwenye biashara ni kupotosha UMMA na hatuwezi tukakaa kimya sababu una duka la viatu, pembejeo na ni mfanyabiashara mkubwa...
 
Mkuu hujui kama hujui unadhani ujuzi mpaka uende kusoma shule ? Hivi hii mada ni ya nani ni mfanyabiashara au ana nini ? Unajua maana ya Ujuzi ? Achana na story za maduka yako hio hapa ni immaterial na wala haimsaidii mtu turudi kwenye mada mimi nimekupa mifano kwanini Ujuzi unatrump Pesa wewe unakuja na hadithi za kwamba hauhitaji ujuzi (kwahio naweza kusema hujui maana ya haya maneno au unadhani mtaji ni Pesa pekee)

By the way kwanini duka lako lipo sokoni au hilo la pembejeo lipo huko lilipo na sio pengine ? (location)
Hahahaha hebu nikuambie kitu njoo sokoni halafu uwaulize wafanyabiashara kuwa changamoto kubwa kwao ni nini halafu uone majibu watakayokupa...na kama ungekuwa mtwara ungejuwa ni kwanini prashant anauza sana kuliko mtu yeyote yule na pia ungejua kwanini chambila pharmacy anauza kuliko pharmacy yeyote mkoa huu wa mtwara
 
Hahahaha hebu nikuambie kitu njoo sokoni halafu uwaulize wafanyabiashara kuwa changamoto kubwa kwao ni nini halafu uone majibu watakayokupa...na kama ungekuwa mtwara ungejuwa ni kwanini prashant anauza sana kuliko mtu yeyote yule na pia ungejua kwanini chambila pharmacy anauza kuliko pharmacy yeyote mkoa huu wa mtwara
Ndio maana nakwambia tatizo lako kubwa hujui maana ya maneno....

Kwa hao wafanyabiashara kujua changamoto au huyu mleta uzi kuja kuuliza anatafuta information (ujuzi / knowledge) Ndio maana kuna msemo usimuulize muuza butcher biashara ya almasi....

Na sijasema pesa haitakiwi, bali nimesema kuna vitu katika biashara huenda ni muhimu kuliko mtu kukuwekea mapesa..., mimi nikija huko na matrilioni bila kufanya research au kujua kwanini huo prashant au sijui nani anauza zaidi kuliko mwingine pesa yangu itapotea (alafu unaongelea pharmacy ambayo inahitaji pesa kubwa kupata vibali na kuajiri mpaka mu-farmasia) ni tofauti na biashara ya chips ambayo kuna mbinu tofauti / ni ngumu kupata vibali kwa mali kauli au kuajiri mu-farmasia kwa mali kauli...., kwenye chips nimekuonyesha ni vipi unaweza kufanya hayo bila kuwa na fedha....

Sasa kwa uhai wa mjadala na kuwapatia ufahamu wengine kuliko kuleta umahili na kujinasibu ungeweka hizo siri za urembo za kufanya kazi huko ambazo wewe unazijua na wengine hawazijui (by the way kwa maneno mengine huo ndio unaitwa Ujuzi / experience / knowledge / skills) ambazo wewe unazo kuhusu sehemu unayofanyia kazi na mimi sina (hata nikiwa na pesa lazima wewe utafanikiwa kuliko mimi)
 
Hahahaha hebu nikuambie kitu njoo sokoni halafu uwaulize wafanyabiashara kuwa changamoto kubwa kwao ni nini halafu uone majibu watakayokupa...na kama ungekuwa mtwara ungejuwa ni kwanini prashant anauza sana kuliko mtu yeyote yule na pia ungejua kwanini chambila pharmacy anauza kuliko pharmacy yeyote mkoa huu wa mtwara
Tufahamishe kwanini wanauza zaidi ya wengine?
 
Tufahamishe kwanini wanauza zaidi ya wengine?
Kama huyo prashant nadhani kwa mkoa wote wa mtwara hamna duka lenye mauzo makubwa kumzidi yeye kwasababu huyo anauza spare za kila aina na vifaa vya ujenzi vya kila aina kwasababu ana mtaji wakutisha sana kiasi kwamba watu wanatoka lindi,tunduru,nachingwea,newala,tandahimba, Mozambique,masasi kuja kununua bidhaa walizokosa kwenye miji yao kiufupi prashant hauzi hakuna dukani kwake
 
Kama huyo prashant nadhani kwa mkoa wote wa mtwara hamna duka lenye mauzo makubwa kumzidi yeye kwasababu huyo anauza spare za kila aina na vifaa vya ujenzi vya kila aina kwasababu ana mtaji wakutisha sana kiasi kwamba watu wanatoka lindi,tunduru,nachingwea,newala,tandahimba, Mozambique,masasi kuja kununua bidhaa walizokosa kwenye miji yao kiufupi prashant hauzi hakuna dukani kwake
Naam hapa nadhani tumefika pazuri kuweza kujadiliana kama watu wenye busara na hekima..., na kwa busara hizo ngoja niweke mfano ufuatao ambao kwa uhalisia haumlengi moja kwa moja huyo muhusika....

Tuseme jamaa ana mtaji wa kutisha hivyo kuweza kuleta bidhaa zote tena kwa bei ndogo (kununua kwa jumla).., Jamaa ana watu wanatoka kila mahali mpaka nchi za jirani (ana Jina tayari na watu wanamwamini, wengine hata hawaji wanapiga simu tu yeye anasafirisha mzigo).., jamaa atakuwa anajua siri za urembo na machimbo ya spea na sababu ameshatengeza jina hata mwingine akija na bei ndogo huenda watu wasiende kwenye bei ndogo sababu ameshajenga jina la uaminifu wa spea zake (branding)..; Jamaa huenda anajua njia za panya na kuweka vitabu vyake vizuri hivyo kutokuwafanyia kazi wazee wa Tozo.....

Sasa tuseme jamaa huyu wa kufikirika akifariki watu wakagawana pesa za urithi akabakia mtoto mmoja akapewa lile duka (jina ) na contacts zote za wateja na sehemu za kununua mzigo na ni kina nani mzigo ukija wa kuwaona ili mzigo utoke vizuri (dogo yote hayo anayo ila pesa ndio hivyo nyingi wamechukua ndugu)...; Lakini kwa kutumia jina la duka, na ukubwa wa biashara dogo anaweza kwenda benki kuvuta mpunga au kuwaambia suppliers wampe mzigo kwa credit hata ya mwezi......

Mimi nisiyejua kitu kuona Mdau wa duka amekufa ninaingia kichwa kichwa naweka duka mtaa wa tatu kutoka kwa jamaa nina pesa mara kumi ya pesa za huyu dogo lakini sina knowledge wala wateja / kufahamika kama jamaa (pesa ninamzidi lakini yeye ananizidi ufahamu, wateja na amejijengea jina) ni nani hapo atafaulu ? Naweza kusema spea zote niuze nusu ya bei ili kuvutia watu (ingawa huenda isifanikiwe kwa watu kudhani spea zangu feki)...,

Kwahio mkuu tutakubaliana hata kwa wewe kufanya unachofanya kwa miaka kadhaa huo ni mtaji tosha na wa maana zaidi kuliko hata pesa (hakuna shule ambayo ingekufundisha / itakufundisha experience ya wewe miaka na miaka kufanya vitu practically) na mimi ninayekuja leo siwezi kupata hayo unayojua wewe unless nikufuate uwe mentor (nichukue yako na niongezee ya kwangu)
 
Naam hapa nadhani tumefika pazuri kuweza kujadiliana kama watu wenye busara na hekima..., na kwa busara hizo ngoja niweke mfano ufuatao ambao kwa uhalisia haumlengi moja kwa moja huyo muhusika....

Tuseme jamaa ana mtaji wa kutisha hivyo kuweza kuleta bidhaa zote tena kwa bei ndogo (kununua kwa jumla).., Jamaa ana watu wanatoka kila mahali mpaka nchi za jirani (ana Jina tayari na watu wanamwamini, wengine hata hawaji wanapiga simu tu yeye anasafirisha mzigo).., jamaa atakuwa anajua siri za urembo na machimbo ya spea na sababu ameshatengeza jina hata mwingine akija na bei ndogo huenda watu wasiende kwenye bei ndogo sababu ameshajenga jina la uaminifu wa spea zake (branding)..; Jamaa huenda anajua njia za panya na kuweka vitabu vyake vizuri hivyo kutokuwafanyia kazi wazee wa Tozo.....

Sasa tuseme jamaa huyu wa kufikirika akifariki watu wakagawana pesa za urithi akabakia mtoto mmoja akapewa lile duka (jina ) na contacts zote za wateja na sehemu za kununua mzigo na ni kina nani mzigo ukija wa kuwaona ili mzigo utoke vizuri (dogo yote hayo anayo ila pesa ndio hivyo nyingi wamechukua ndugu)...; Lakini kwa kutumia jina la duka, na ukubwa wa biashara dogo anaweza kwenda benki kuvuta mpunga au kuwaambia suppliers wampe mzigo kwa credit hata ya mwezi......

Mimi nisiyejua kitu kuona Mdau wa duka amekufa ninaingia kichwa kichwa naweka duka mtaa wa tatu kutoka kwa jamaa nina pesa mara kumi ya pesa za huyu dogo lakini sina knowledge wala wateja / kufahamika kama jamaa (pesa ninamzidi lakini yeye ananizidi ufahamu, wateja na amejijengea jina) ni nani hapo atafaulu ? Naweza kusema spea zote niuze nusu ya bei ili kuvutia watu (ingawa huenda isifanikiwe kwa watu kudhani spea zangu feki)...,

Kwahio mkuu tutakubaliana hata kwa wewe kufanya unachofanya kwa miaka kadhaa huo ni mtaji tosha na wa maana zaidi kuliko hata pesa (hakuna shule ambayo ingekufundisha / itakufundisha experience ya wewe miaka na miaka kufanya vitu practically) na mimi ninayekuja leo siwezi kupata hayo unayojua wewe unless nikufuate uwe mentor (nichukue yako na niongezee ya kwangu)
Aisee vijana wa chuo akili zenu zimejengwa kwa mfumo wa kufikirika sana...kinachosababisha prashant anauza sana ni kwamba ana mtaji wa kutosha kiasi kwamba anapofuata bidhaa huwa hajiulizi hii inamzinguko sana au lah bali yeye anabeba tu anajua ipo siku atauza
 
Kitu kigumu ni kupata mtaji dogo
Hata Mimi nilikuwa na mawazo kama yako zamani nikiamini nashindwa kupiga hatua sababu ya kukosa mtaji nikawa nadharau kidogo nilichokuwa nacho kumbe maisha hayapo hivi Kuna elimu inahitajika unawezaje kuwatumia watu wachache wakuzalishie faida kwa kidogo ulichonacho kuwa na mtaji bila elimu una risk yakupoteza pesa nyingi elimu ni nguzo
 
Hata Mimi nilikuwa na mawazo kama yako zamani nikiamini nashindwa kupiga hatua sababu ya kukosa mtaji nikawa nadharau kidogo nilichokuwa nacho kumbe maisha hayapo hivi Kuna elimu inahitajika unawezaje kuwatumia watu wachache wakuzalishie faida kwa kidogo ulichonacho kuwa na mtaji bila elimu una risk yakupoteza pesa nyingi elimu ni nguzo
Mimi naitwa mnachihanguu nafanya biashara mjini mtwara mimi sipo kama wewe mpiga debe tu....kinachowafelisha wengi ni mitaji tu dogo
 
Aisee vijana wa chuo akili zenu zimejengwa kwa mfumo wa kufikirika sana...kinachosababisha prashant anauza sana ni kwamba ana mtaji wa kutosha kiasi kwamba anapofuata bidhaa huwa hajiulizi hii inamzinguko sana au lah bali yeye anabeba tu anajua ipo siku atauza
Kwahio ushauri wako kwa mtu ni kununua bidhaa za aina zote ili mteja akija apate kila kitu under one roof ? Na hilo ndio unadhani linamfanya huyu bwana aweze kufaulu kuliko wengine ?

Kwahio na wewe ukipata mtaji zaidi kwenye duka lako la viatu utaleta kila aina ya kiatu kuanzia Timberland mpaka Katambuga..., bila kujali mambo ya storage costs na labda space yako ya showroom kufanya viatu vingine vyenye faida visionekane ? Je kwa kufanya kwako hivyo na mwingine ambaye ameamua kutumia media za online kwa kuwa na vitu vichache showroom na vingine vyote kuvi-display online hata vile ambavyo hana ni nani yupo efficient ?

Na siongei tu kinadharia nakuja na mifano hai wakati Bookshops za zamani zilikuwa ni majengo kila kitabu kipo mule ndani na watu wanakuja kununua alikuja jamaa mmoja Jeff Bezos hana bookshop wala lolote bali aliweza kupata wateja kwa kuonyesha vitabu na watu wakitaka Bezos anakwenda BookShop ananunua na kuwapelekea wateja..., Muda si muda kutokana na kwamba yeye alikuwa hana overheads kama hizi bookshops (kukodi premises) aliweza kuuza hata kwa bei ndogo kuliko hizo bookshops na hizo bookshops kuanza kumuomba yeye ndio awauzie.....

Mkuu kuna vitu vingi katika mafanikio na wewe hapo huenda hujui ila mafanikio ya elimu yako na ufahamu wako wa hicho unachokifanya, sehemu ya maduka yako yalipo na jina ulilojijengea kwa miaka yote hii ni muhimu kuliko hata hizo pesa ulizonazo.., Unaweza ukapata mtaji zaidi ukasema ufungue branches kila mkoa ila kutokuwepo usimamizi wako maduka yote mengine yaka-flop....
 
Kwahio ushauri wako kwa mtu ni kununua bidhaa za aina zote ili mteja akija apate kila kitu under one roof ? Na hilo ndio unadhani linamfanya huyu bwana aweze kufaulu kuliko wengine ?

Kwahio na wewe ukipata mtaji zaidi kwenye duka lako la viatu utaleta kila aina ya kiatu kuanzia Timberland mpaka Katambuga..., bila kujali mambo ya storage costs na labda space yako ya showroom kufanya viatu vingine vyenye faida visionekane ? Je kwa kufanya kwako hivyo na mwingine ambaye ameamua kutumia media za online kwa kuwa na vitu vichache showroom na vingine vyote kuvi-display online hata vile ambavyo hana ni nani yupo efficient ?

Na siongei tu kinadharia nakuja na mifano hai wakati Bookshops za zamani zilikuwa ni majengo kila kitabu kipo mule ndani na watu wanakuja kununua alikuja jamaa mmoja Jeff Bezos hana bookshop wala lolote bali aliweza kupata wateja kwa kuonyesha vitabu na watu wakitaka Bezos anakwenda BookShop ananunua na kuwapelekea wateja..., Muda si muda kutokana na kwamba yeye alikuwa hana overheads kama hizi bookshops (kukodi premises) aliweza kuuza hata kwa bei ndogo kuliko hizo bookshops na hizo bookshops kuanza kumuomba yeye ndio awauzie.....

Mkuu kuna vitu vingi katika mafanikio na wewe hapo huenda hujui ila mafanikio ya elimu yako na ufahamu wako wa hicho unachokifanya, sehemu ya maduka yako yalipo na jina ulilojijengea kwa miaka yote hii ni muhimu kuliko hata hizo pesa ulizonazo.., Unaweza ukapata mtaji zaidi ukasema ufungue branches kila mkoa ila kutokuwepo usimamizi wako maduka yote mengine yaka-flop....
Dogo wewe unafanya biashara gani?
 
Dogo wewe unafanya biashara gani?
Nadhani umepotea uzi..., Huu sio uzi wa Nani anafanya nini ni uzi wa mtu kuuliza swali kama pesa aliyonayo anaweza kufanya biashara fulani..., Ungekuwa ni uzi wa personality wala nisingesumbuka kujibu chochote....

Kwahio nakuomba tena kwa mara nyingine kwa uhai wa mjadala na mafunzo kwa wasomaji tujikite kwenye hoja..., mimi nimekupa hapo mifano kibao ni vipi mtu mwenye ufahamu / knowledge anaweza kufanikiwa na kwanini pesa sio kila kitu....
 
Salaam Wanajukwaa

Kama ilivyo desturi yetu Wanajf kujuzana, kuelimishana nk..

Leo ningeomba kufahamishwa kwa wenye uzoefu je kwa mtaji wa Milioni 2 naweza fungua biashara hizi mbili
1.Saloon ya kiume
2.Biashara ya chipsi

Kwa wew uliewahi fanya biashara ya chips unaweza toa uzoefu wako mtaji unaweza cost bei gani hadi deal kukamilika
Ishu kama ya jiko, kabati na mazagazaga yote

Vilevile na kwe wew walau unajua A B C biashara ya Saloon toa experience yako

Natanguliza shukrani
Hiyo milion 2 nenda kabetie Kila siku unaeka 1.06 odd tu unapata faida ya laki ko Kila siku utaingiza laki. Odd 1.06 unaeza kuipata Kwa kueka over 0.5 gemu 2 mpaka 3 mfano gemu tatu za odds 1.02 each au gemu mbili za odds 1.03 ko tafuta gemu 2 mpaka 3 siku nzima zinazoeza kutoa goli apo kazi imeisha na usishangae gemu ikaisha 0-0😂
 
Hiyo milion 2 nenda kabetie Kila siku unaeka 1.06 odd tu unapata faida ya laki ko Kila siku utaingiza laki. Odd 1.06 unaeza kuipata Kwa kueka over 0.5 gemu 2 mpaka 3 mfano gemu tatu za odds 1.02 each au gemu mbili za odds 1.03 ko tafuta gemu 2 mpaka 3 siku nzima zinazoeza kutoa goli apo kazi imeisha na usishangae gemu ikaisha 0-0😂
Okay 1.06 hapo ni kwamba kila tshs 100/ unayoweka unapata tshs 6 (hapo bado serikali haijachukua percent kumi ila tuache kwanza hayo)...

kwahio ukiweka laki hapo unapata tshs elfu sita faida..., ili laki yako izae laki inabidi ushinde kama mara 16... yaani hata ushinde mara 32 ukipoteza mara ya 33 na labda 36 mtaji wako wote unakuwa umeliwa....

In short the House eventually always wins..., the odds are stuck against the Punter....
 
Okay 1.06 hapo ni kwamba kila tshs 100/ unayoweka unapata tshs 6 (hapo bado serikali haijachukua percent kumi ila tuache kwanza hayo)...

kwahio ukiweka laki hapo unapata tshs elfu sita faida..., ili laki yako izae laki inabidi ushinde kama mara 16... yaani hata ushinde mara 32 ukipoteza mara ya 33 na labda 36 mtaji wako wote unakuwa umeliwa....

In short the House eventually always wins..., the odds are stuck against the Punter....
Hakuna Cha house win Wala Cha nini we ukiwa na bahati Yako tu unaweza ukala Kila siku tu sasa mpira si unachezwa hazarani unaonekana Yani nmeeka Barcelona win afu akashinda ko apo house itafosi iwin au 😂
 
Mkuu hujui kama hujui unadhani ujuzi mpaka uende kusoma shule ? Hivi hii mada ni ya nani ni mfanyabiashara au ana nini ? Unajua maana ya Ujuzi ? Achana na story za maduka yako hio hapa ni immaterial na wala haimsaidii mtu turudi kwenye mada mimi nimekupa mifano kwanini Ujuzi unatrump Pesa wewe unakuja na hadithi za kwamba hauhitaji ujuzi (kwahio naweza kusema hujui maana ya haya maneno au unadhani mtaji ni Pesa pekee)

By the way kwanini duka lako lipo sokoni au hilo la pembejeo lipo huko lilipo na sio pengine ? (location)...; Kwahio mkuu hata kama wewe ndio ungekuwa ndio mgunduzi wa Biashara duniani au hapa naongea na Mo au Bhakresa au Dangote ukileta story za kwamba ujuzi hauna faida kwenye biashara ni kupotosha UMMA na hatuwezi tukakaa kimya sababu una duka la viatu, pembejeo na ni mfanyabiashara mkubwa...
Hana duka Tunduru huyo
 
Hakuna Cha house win Wala Cha nini we ukiwa na bahati Yako tu unaweza ukala Kila siku tu sasa mpira si unachezwa hazarani unaonekana
Sasa ndio nakwambia odds unazopewa wewe sio halisi kama ni kurusha shilingi badala ya ukishinda nikupe shilingi wewe ukishinda unapewa senti tisini ukishindwa unatoa shilingi moja sasa kama knowledge yenu wote ni sawa ni kwamba wewe umepewa raw deal., kama shilingi itarushwa mara kumi na wewe kushinda tano na yeye mara tano wewe utakuwa na 4.60 yeye atakuwa na 5.40..., Its all in mathematics na probability....
Yani nmeeka Barcelona win afu akashinda ko apo house itafosi iwin au 😂
Naam sababu Barcelona huwa anashinda mara tisa katika kila mechi kumi badala ya kuewa odds za mfano 1.09 unaweza ukapewa 1.08 kwahio ile moja atakayopoteza no matter imetokea game ya ishirini au ya 15 au ya kwanza mtaji wako wote ulioshapata utarudishia the House....
 
Back
Top Bottom