Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 914
- 4,262
Leo imetolewa hoja kwamba magari ya serikali yapaki saa kumi na mbili. Unajiuliza hawa watu wanapotoa haya matamko wanashindwaga nini kufanya tathimini?
Nchi hii inawaza kuendesha shughuli zake masaa ishirini na nne; Mama anawaza kuona soko la Kariakoo linafanya kazi masaa ishirini na nne kuendana na ratiba ya vyombo vya usafiri.
Tunaelewa kwamba kadri muda wakutoa huduma unavyoongezeka ndivyo serikali inapanua muda wa usimamizi. Leo walevi kipaki magari bar imekuwa ni agenda inayopelekea mteule wa Rais kusema magari yapaki saa kumi na mbili?
Huyu Mbunge aliyetoa hoja alishindwa kupiga picha gari husika akamtumia waziri Dreva au bosi akawajibishwa tukasonga mbele?
Mimi naamini kila gari linasimamiwa na Kiongoz aliyepewa dhamana na serikali. Likitumika vibaya kiongozi anapaswa kushughulikiwa lakini siyo waovu wachache warudishe juhudi za serikali kutoa huduma saa ishirini na nne.
Mnapotoa matamko na makatazo someni sera ya nchi kwanza. Mimi ningesema tumelipokea na tutalifanyia kazi then you go back to the office and communicate.
Ulaya nidhamu imejengwa kwenye uwajibishaji wa watovu wa nidhamu. Tuangaike na tatizo na siyo kufanya vitu jumla.
Mwisho, najiuliza hao watakaotembea usiku na gari za serikali watakamatwa na polisi na kuzuiwa?
Nchi hii inawaza kuendesha shughuli zake masaa ishirini na nne; Mama anawaza kuona soko la Kariakoo linafanya kazi masaa ishirini na nne kuendana na ratiba ya vyombo vya usafiri.
Tunaelewa kwamba kadri muda wakutoa huduma unavyoongezeka ndivyo serikali inapanua muda wa usimamizi. Leo walevi kipaki magari bar imekuwa ni agenda inayopelekea mteule wa Rais kusema magari yapaki saa kumi na mbili?
Huyu Mbunge aliyetoa hoja alishindwa kupiga picha gari husika akamtumia waziri Dreva au bosi akawajibishwa tukasonga mbele?
Mimi naamini kila gari linasimamiwa na Kiongoz aliyepewa dhamana na serikali. Likitumika vibaya kiongozi anapaswa kushughulikiwa lakini siyo waovu wachache warudishe juhudi za serikali kutoa huduma saa ishirini na nne.
Mnapotoa matamko na makatazo someni sera ya nchi kwanza. Mimi ningesema tumelipokea na tutalifanyia kazi then you go back to the office and communicate.
Ulaya nidhamu imejengwa kwenye uwajibishaji wa watovu wa nidhamu. Tuangaike na tatizo na siyo kufanya vitu jumla.
Mwisho, najiuliza hao watakaotembea usiku na gari za serikali watakamatwa na polisi na kuzuiwa?