GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 57,134
- 110,489
Ama hakika kwa Wimbo huu na hasa ulivyo Mtamu na unavyochangamsha hata Kuucheza JB Mpiana kaamu kufanya Kweli. Unaambiwa sasa iwe ni Congo DR au Congo Brazaville au Angola au Cameroon au Zambia au Ufaransa au Ubelgiji au Marekani ( hasa Mji wenye Wakongo wengi wa Dallas ) au Rwanda na Burundi habari ya Mjini ni huu Wimbo mpya na wenye Style mpya ya Kucheza wa ZEBUKA.
Humo Atalaku au Mghani au Kizungu mnawaita Rappers na kwa Kifaransa wanaitwa Animateurs Mwamba kabisa GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE ( majina halisi Pitshou Lisimo ) kafanya Balaa Kubwa kama kawaida yake na ndiyo maana sasa anaheshimika kama Champion Le Animateur du Congo DR ( yaani Rapa Bingwa Congo DR ) kutokana na kujua Kutunga maneno na Kucheza kwa Ustadi'
Pia Atalaku ( Mghani ) huyu GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE katika huu Wimbo Gumzo sasa uitwao ZEBUKA ambao upatikana katika Album ya BALLE DE MATCH kasaidiwa vyema sana na Wasaidizi wake Wawili akina Pajo na Fusse De Guere ( Kombora la Vita ) huku Gitaa la Solo likikung'utwa vyema kabisa na Veteran Guitarist Ficarre Mwamba a.k.a wanamuitwa Mitre ( wakimaanisha Mwalimu ) wa Wapiga Magitaa Congo DR.
Hata hivyo kwa Masikitiko makubwa baada ya Kuutoa Wimbo huu wa ZEBUKA Bendi ya Wenge BCBG imepata Pigo Kubwa sana la Kuondokewa na Dancer wake maaufu sana wa Kiume ambaye amekuwa Kivutio Kikubwa kila waendako aitwae Mulala Djo Muloxy ambaye alifariki ghafla. R.I.P Kwake Dancer Mulala Djo hakika umeacha Pengo Kubwa Bendini na ndiyo maana hata JB Mpiana kakulilia sana Msibani.
Kwa wale Bana Wenge BCBG Wenzangu JF tafadhali nendeni YouTube ili mkauone huu Wimbo mtamu wa ZEBUKA.
Humo Atalaku au Mghani au Kizungu mnawaita Rappers na kwa Kifaransa wanaitwa Animateurs Mwamba kabisa GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE ( majina halisi Pitshou Lisimo ) kafanya Balaa Kubwa kama kawaida yake na ndiyo maana sasa anaheshimika kama Champion Le Animateur du Congo DR ( yaani Rapa Bingwa Congo DR ) kutokana na kujua Kutunga maneno na Kucheza kwa Ustadi'
Pia Atalaku ( Mghani ) huyu GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE katika huu Wimbo Gumzo sasa uitwao ZEBUKA ambao upatikana katika Album ya BALLE DE MATCH kasaidiwa vyema sana na Wasaidizi wake Wawili akina Pajo na Fusse De Guere ( Kombora la Vita ) huku Gitaa la Solo likikung'utwa vyema kabisa na Veteran Guitarist Ficarre Mwamba a.k.a wanamuitwa Mitre ( wakimaanisha Mwalimu ) wa Wapiga Magitaa Congo DR.
Hata hivyo kwa Masikitiko makubwa baada ya Kuutoa Wimbo huu wa ZEBUKA Bendi ya Wenge BCBG imepata Pigo Kubwa sana la Kuondokewa na Dancer wake maaufu sana wa Kiume ambaye amekuwa Kivutio Kikubwa kila waendako aitwae Mulala Djo Muloxy ambaye alifariki ghafla. R.I.P Kwake Dancer Mulala Djo hakika umeacha Pengo Kubwa Bendini na ndiyo maana hata JB Mpiana kakulilia sana Msibani.
Kwa wale Bana Wenge BCBG Wenzangu JF tafadhali nendeni YouTube ili mkauone huu Wimbo mtamu wa ZEBUKA.