Content ya media nyingi sio kwa ajili ya kuelimisha, uchambuzi wa mpira umetamalaki. Kama jamii tunapaswa kubadilika

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
34,747
41,080
Kama wiki mbili hivi sikuwa online kwenye social media hivyo nilipata wasaa wa kusikiliza redio zetu hapa nchini.

Katika wiki zote hizo mbili nilikua natune almost radio zote , ila vipindi vingi vya radio zetu vinafanana na sio elimishi, burudani imechukua sehemu kubwa na hasa uchambuzi wa mpira.

Asubuhi radio zote wanasoma magazeti na kuchambua habari. Hapa watangazaji wanatoa maoni binafsi bila kuwa na utaalam wowote wa maswala wanayoyazungumzia. Uwezekano wa kupotosha watu ni mkubwa sana. Haiwezekani mtu ukawa na ufahamu wa kila kitu, ndio maana media za nje huwa wanaalika wataalam kuzungumzia jambo kulingana na taaluma zao.

Baada ya vipindi vya magazeti, radio zote wataanza kuchambua mpira, mechi zote za ligi ya ndani na nje zitachambuliwa hapo ni masaa mawili.

Itafuatia muziki na porojo nyingine mpaka usiku tena, ambapo watarudia tena uchambuzi wa mpira na muziki.

Katika wiki zote hizo mbili na kusikiliza Radio mbali mbali ni siku moja tu nilibahatika kusikia content ya maana, hii ilikua Radio uhuru na walikua wanazungumza na mkurugenzi wa kampuni inayotoa huduma ya kuwapatia watu wafanyakazi wa ndani. Kile kipindi kilikua kizuri sana, na kilitoa mafunzo mengi mno.

Kwakweli naona kuna haja ya serikali kupitia wizara na taasisi zake kuweka miongozo ya content za media zetu otherwise tutakuwa na jamii yenye watu wa hovyo tu.

Haiwezekani siku nzima ni mijadala isiyokuwa na tija inaendelea kwenye media zetu.

Yaani ni mpira tuu siku nzima. Hii haikubaliki.

Unless tunataka tuwe na jamii ya kubet na mpira basi tuendelee namna hii ila kama tunataka kujenga Taifa lenye watu wanaojielewa na wanafanya mambo ya maana na sio wasindikizaji tu , tunapaswa kubadilika.
 
Media inawapa wanachotaka watanzania. Wewe angalia thread za kula tunda kimasihara zinacomments na views ngapi na zile zenye topic elimishi zina comment ngapi utaelewa. Media ni biashara ukijifanya unaelimisha wasikilizaji haba na matangazo hupati
 
Hio ni kazi ya TBC huwezi kuwapangia wengine content za kuweka ukizingatia huwalipi..., Unachoweza kufanya ni kuanzisha TV / Redio ya kwako na kuweka content unazotaka... Lakini angalizo huenda usipate sponsor wa hizo content...
 
Media inawapa wanachotaka watanzania. Wewe angalia thread za kula tunda kimasihara zinacomments na views ngapi na zile zenye topic elimishi zina comment ngapi utaelewa. Media ni biashara ukijifanya unaelimisha wasikilizaji haba na matangazo hupati
Kama watu hawajielewi ipo haja ya kuwasaidia kujielewa.

Hatuwezi kuendelea kujenga Taifa la hovyo namna hii watu wanajadili mpira asubuhi mchana na usiku.

Hii ndio kazi ya serikali sasa. Na inatakiwa kuact.
 
Hiyo ni Social engineering, hayo mambo hayatokeitokei tu brother. Fungua macho angalia mbele..
 
Kama wiki mbili hivi sikuwa online kwenye social media hivyo nilipata wasaa wa kusikiliza redio zetu hapa nchini.

Katika wiki zote hizo mbili nilikua natune almost radio zote , ila vipindi vingi vya radio zetu vinafanana na sio elimishi, burudani imechukua sehemu kubwa na hasa uchambuzi wa mpira.

Asubuhi radio zote wanasoma magazeti na kuchambua habari. Hapa watangazaji wanatoa maoni binafsi bila kuwa na utaalam wowote wa maswala wanayoyazungumzia. Uwezekano wa kupotosha watu ni mkubwa sana. Haiwezekani mtu ukawa na ufahamu wa kila kitu, ndio maana media za nje huwa wanaalika wataalam kuzungumzia jambo kulingana na taaluma zao.

Baada ya vipindi vya magazeti, radio zote wataanza kuchambua mpira, mechi zote za ligi ya ndani na nje zitachambuliwa hapo ni masaa mawili.

Itafuatia muziki na porojo nyingine mpaka usiku tena, ambapo watarudia tena uchambuzi wa mpira na muziki.

Katika wiki zote hizo mbili na kusikiliza Radio mbali mbali ni siku moja tu nilibahatika kusikia content ya maana, hii ilikua Radio uhuru na walikua wanazungumza na mkurugenzi wa kampuni inayotoa huduma ya kuwapatia watu wafanyakazi wa ndani. Kile kipindi kilikua kizuri sana, na kilitoa mafunzo mengi mno.

Kwakweli naona kuna haja ya serikali kupitia wizara na taasisi zake kuweka miongozo ya content za media zetu otherwise tutakuwa na jamii yenye watu wa hovyo tu.

Haiwezekani siku nzima ni mijadala isiyokuwa na tija inaendelea kwenye media zetu.

Yaani ni mpira tuu siku nzima. Hii haikubaliki.

Unless tunataka tuwe na jamii ya kubet na mpira basi tuendelee namna hii ila kama tunataka kujenga Taifa lenye watu wanaojielewa na wanafanya mambo ya maana na sio wasindikizaji tu , tunapaswa kubadilika.
Hii ni kweli radio nyingi na TV zimejikita kwenye mpira na hata huo mpira wenyewe hawaujui. Tunatengeneza taifa la wajinga haswa maana consumer wengi wa hizi habari za mpira ni wale wa hali ya chini ambao ni wengi sana hapa nchini
 
Kama watu hawajielewi ipo haja ya kuwasaidia kujielewa.

Hatuwezi kuendelea kujenga Taifa la hovyo namna hii watu wanajadili mpira asubuhi mchana na usiku.

Hii ndio kazi ya serikali sasa. Na inatakiwa kuact.
Viongoz wenyewe wanapenda. Mwijaku rahs kuonana na spka kuliko wewe
 
Hii ni kweli radio nyingi na TV zimejikita kwenye mpira na hata huo mpira wenyewe hawaujui. Tunatengeneza taifa la wajinga haswa maana consumer wengi wa hizi habari za mpira ni wale wa hali ya chini ambao ni wengi sana hapa nchini
Makampuni ya betting nayo yanahusika na hii ni biashara kubwa kwao.

Watu hawafanyi tena kazi Maisha yamekua ni kubahatisha bahatisha tu.

Tukiendelea namna hii huko mbeleni watanzania watakuja tawaliwa tena na watu wa mataifa mengine, trust me.
 
Hii ni kweli radio nyingi na TV zimejikita kwenye mpira na hata huo mpira wenyewe hawaujui. Tunatengeneza taifa la wajinga haswa maana consumer wengi wa hizi habari za mpira ni wale wa hali ya chini ambao ni wengi sana hapa nchini
Hio ni kazi ya TBC ambao wanapata Ruzuku hivyo hata kazi ambazo hazina sponsors na hazina wateja wanaweza kuziweka so long as zinafundisha..., wengine hao sababu wapo business oriented wana-cater for the market (kwahio wanafanya kile wateja wanataka)

Anyway kwenye dunia ya sasa ya Video / Content on demand hizo media zenyewe unless zinabadilika ni dead man walking....
 
Hio ni kazi ya TBC ambao wanapata Ruzuku hivyo hata kazi ambazo hazina sponsors na hazina wateja wanaweza kuziweka so long as zinafundisha..., wengine hao sababu wapo business oriented wana-cater for the market (kwahio wanafanya kile wateja wanataka)

Anyway kwenye dunia ya sasa ya Video / Content on demand hizo media zenyewe unless zinabadilika ni dead man walking....
Serikali yeyote makini huwa ina control contents ya media.

Sio afya kuacha hali hii iendelee tunaharibu kizazi kijacho.
 
Hio ni kazi ya TBC ambao wanapata Ruzuku hivyo hata kazi ambazo hazina sponsors na hazina wateja wanaweza kuziweka so long as zinafundisha..., wengine hao sababu wapo business oriented wana-cater for the market (kwahio wanafanya kile wateja wanataka)

Anyway kwenye dunia ya sasa ya Video / Content on demand hizo media zenyewe unless zinabadilika ni dead man walking....
Biashara isiyo na uthibiti ni hatari kwa taifa. Radio ndiyo zilikuwa chanzo cha machafuko Kenya na Rwanda. Lazima zithibitiwe na contents za maudhui lazima yapimwe na kuonekana kama yana faida kwa jamii. Huwezi tu kuanzisha radio na kutangaza mambo unayokata ambayo hayana faida kwa jamii
 
Jambo hili mi nililiona kitambo sana, ila nikadhani labda ndo muongozo wanaopewa huko kwenye vyuo vyao vya uandishi wa habari, basi nikaona isiwe tabu nikaamua kukaa kimya.
 
Serikali yeyote makini huwa ina control contents ya media.

Sio afya kuacha hali hii iendelee tunaharibu kizazi kijacho.
Huwezi kumpangia mtu binafsi aweke contents unazotaka wakati humpi hata senti na hata hizo contents unazotaka aweke huenda hazina sponsor (mwisho wa siku atakufa kifo cha kawaida)

Na kwa kujua hayo ndio maana kuna Redio na TV za taifa ambazo zinapewa Ruzuku ili zifanye hio kazi kwahio mtu ana option ya kuweza kupata mafunzo...

Serikali inachoweza kufanya ni kuzuia baadhi ya matangazo au muda wa hayo matangazo kama watazamaji ni watoto pia (mfano kamari, ulevi na vitu vya uongo na kupotosha)
 
Biashara isiyo na uthibiti ni hatari kwa taifa. Radio ndiyo zilikuwa chanzo cha machafuko Kenya na Rwanda. Lazima zithibitiwe na contents za maudhui lazima yapimwe na kuonekana kama yana faida kwa jamii. Huwezi tu kuanzisha radio na kutangaza mambo unayokata ambayo hayana faida kwa jamii
Faida ni nini ? Mpira, miziki na entertainment hazina faida ? Ni kweli matangazo ya kamari hayafai tena hata kipindi cha habari / prime time... hio inabidi ikatazwe lakini sio umpangie mtu aliyefungua TV / Radio sababu ya entertainment kwamba alete habari za Siasa..... Kipindi hiki cha Content on Demand huwezi kulazimisha watu kuangalia...

LAKINI ndio maana tuna alternative ambayo kazi yake ndio hio TBC na Radio Tanzania..., Lakini sio TV yangu ya Walokole utake niweke habari zako za Siasa au Kilimo na Uuzaji wa Karanga....
 
Back
Top Bottom