Precious Diamond
JF-Expert Member
- Jun 9, 2023
- 400
- 1,004
Wakuu kwema?
Tumekuwa tukishuhudia wasanii na wanasiasa kutoka vyam vya upinzani kuchukiliwa hatua wakikosoa upinzani kwa kupewa kesi za ugaidi na uchochezi. Akina Nay Wamitego na aliyeimba wanatuona manyani tu (Tanzania yetu) walivyotaabishwa, akina Mbowe chama chao kimekuwa na nenda rudi za kutosha kutoka polisi, mashtaka ambayo wanapewa ili tu kuwanyamazisha na kukandamizia uhuru wa kujileza.
Sasa leo imetokea kwao, kiongozi wa vijana ametaka kweupe, wakiwapoteza wanaotukana serikali polisi wasiingilie. Hii ni kauli ya kutisha ukizingatia na historia ya matukio huko nyuma.
Nchimbi unakuja kutoa kauli eti haa vijana huwa wanajisahau, tuwakanye! Kwa kauli inayoashiria vitendo vya kiuaji? Kwanini hajafikishwa central mpaka sasa kuisaidia polisi? Na watu wakampigia makofi kabisa kuonesha ni jambo la kawaida kufanywa.
Jambo hili linapotezewa kivipi? Inaonesha vijana wa CCM wanaweza kufanya lolotebila actions zao kuchukuliwa hatua. Next time hatatamka, atatekeleza kimya kimya tusijue nini kimetokea watakati tumepewa hint ya watu wasiojulikana ni akina nani.
Polisi tunasubiri mfanye kazi yenu mnayoifanyaga kwa weledi ikitokea wasanii, wanasiasa wa vyama vya upinzani, na wananchi wa kawaida wamekosoa serikali. Tunasubiri kauli yenu iliyotukuka juu ya suala hili.
Kwenu Wakuu.
==
Pia soma
Dkt. Nchimbi apinga kauli ya Mwenyekiti wa UVCCM Kagera aliyeahidi "kuwapoteza" wakosoaji wa serikali
CCM ya sasa ingekuwa smart ingemkana Mwenyekiti UVCCM Kagera. Kwa kunyamaza ni kama wanathibitisha ni wauwaji
Mwenyekiti UVCCM Kagera, Faris Buruhan: Tukiwapoteza wanaomtukana Rais Samia mitandaoni, Polisi msiwatafute
Tumekuwa tukishuhudia wasanii na wanasiasa kutoka vyam vya upinzani kuchukiliwa hatua wakikosoa upinzani kwa kupewa kesi za ugaidi na uchochezi. Akina Nay Wamitego na aliyeimba wanatuona manyani tu (Tanzania yetu) walivyotaabishwa, akina Mbowe chama chao kimekuwa na nenda rudi za kutosha kutoka polisi, mashtaka ambayo wanapewa ili tu kuwanyamazisha na kukandamizia uhuru wa kujileza.
Sasa leo imetokea kwao, kiongozi wa vijana ametaka kweupe, wakiwapoteza wanaotukana serikali polisi wasiingilie. Hii ni kauli ya kutisha ukizingatia na historia ya matukio huko nyuma.
Nchimbi unakuja kutoa kauli eti haa vijana huwa wanajisahau, tuwakanye! Kwa kauli inayoashiria vitendo vya kiuaji? Kwanini hajafikishwa central mpaka sasa kuisaidia polisi? Na watu wakampigia makofi kabisa kuonesha ni jambo la kawaida kufanywa.
Jambo hili linapotezewa kivipi? Inaonesha vijana wa CCM wanaweza kufanya lolotebila actions zao kuchukuliwa hatua. Next time hatatamka, atatekeleza kimya kimya tusijue nini kimetokea watakati tumepewa hint ya watu wasiojulikana ni akina nani.
Polisi tunasubiri mfanye kazi yenu mnayoifanyaga kwa weledi ikitokea wasanii, wanasiasa wa vyama vya upinzani, na wananchi wa kawaida wamekosoa serikali. Tunasubiri kauli yenu iliyotukuka juu ya suala hili.
Kwenu Wakuu.
==
Pia soma
Dkt. Nchimbi apinga kauli ya Mwenyekiti wa UVCCM Kagera aliyeahidi "kuwapoteza" wakosoaji wa serikali
CCM ya sasa ingekuwa smart ingemkana Mwenyekiti UVCCM Kagera. Kwa kunyamaza ni kama wanathibitisha ni wauwaji
Mwenyekiti UVCCM Kagera, Faris Buruhan: Tukiwapoteza wanaomtukana Rais Samia mitandaoni, Polisi msiwatafute