Deogratias Mutungi
Senior Member
- Oct 1, 2019
- 139
- 179
Nianze kwa kutoa salaam na heri za mwaka mpya kwa jamii ya wanajamii forum wote.
Baada ya Salaam nirejee kwenye mada husika, Kwa siku za hivi karibuni ajali za barabarani zimekuwa tatizo na kichwa cha mwendawazimu, tumepoteza ndugu, Jamaa na marafiki kwa sababu ya ajali ambazo pengine zinaepukika na wala si kwa mapenzi ya Mwenyezi Mungu, bali kwa mapenzi ya "madereva wahuni"
Zipo sababu za msingi ambazo mamlaka husika wanapaswa kuzimulika ili kupunguza janga hili, sababu hizo ni pamoja na; Mosi, Nidhamu mbovu ya madereva wawapo barabarani, Madereva wengi utumia simu janja 'smartphone" kufanya mawasiliano na aidha marafiki, ndugu au wenza wao huku wakiendesha vyombo vya moto.
Pili, Utumiaji wa vilevi kama, Pombe na madawa ya kulevya mfano: Bangi, Mirungi na Ugoro ni sababu kubwa inayochangia madereva walio wengi kushindwa kumudu vyombo vya moto na hivyo kusababisha ajali na kusababisha vifo na majeruhi.
Tatu, Msongo wa mawazo na mfadhaiko kwa baadhi ya madereva upelekea kusababisha ajali, Mara kadhaa nimeshuhudia madereva wengi wakiongea peke yao huku wakisikitika na kunungunika juu ya aidha ugumu wa maisha au uwepo wa migogoro ya kifamilia kati ya dereva na mke, au mchepuko wake.
Nne, Rushwa, Miundombinu mibovu ya barabara, ubovu wa magari, upatikanaji wa leseni kinyume na utaratibu na sheria za nchi, kutojali utu, ukosefu wa hofu ya Mungu na imani za kishirikina ni sehemu ya sababu zinazochangia madereva wengi wa Tanzania na bara la Afrika kusababisha ajali zinazogharimu uhai wa binadamu, Wakati ni sasa, Taifa na Watanzania kushikamana na kukemea madereva wanaokiuka miiko ya udereva.
Watanzania tupaze sauti, Tupaze sauti, Tupaze sauti, wakati ni sasa, tusipofanya hivyo tutakwisha na kuachwa na ulemavu wa kudumu kwa sababu ya uzembe wa mtu mmoja, ambaye anaitwa dereva.
Aidha ni wajibu wa serikali kuwachukulia hatua stahiki na kali sana madereva wote wahuni wanaoenda kinyume na sheria na utaratibu wa usalama barabarani, ni wakati sasa wa kutungwa sheria kali inayozuia matumizi ya simu wakati wa utumiaji wa chombo cha moto, sheria hii ije sasa na ndio wakati wake.
Baada ya Salaam nirejee kwenye mada husika, Kwa siku za hivi karibuni ajali za barabarani zimekuwa tatizo na kichwa cha mwendawazimu, tumepoteza ndugu, Jamaa na marafiki kwa sababu ya ajali ambazo pengine zinaepukika na wala si kwa mapenzi ya Mwenyezi Mungu, bali kwa mapenzi ya "madereva wahuni"
Zipo sababu za msingi ambazo mamlaka husika wanapaswa kuzimulika ili kupunguza janga hili, sababu hizo ni pamoja na; Mosi, Nidhamu mbovu ya madereva wawapo barabarani, Madereva wengi utumia simu janja 'smartphone" kufanya mawasiliano na aidha marafiki, ndugu au wenza wao huku wakiendesha vyombo vya moto.
Pili, Utumiaji wa vilevi kama, Pombe na madawa ya kulevya mfano: Bangi, Mirungi na Ugoro ni sababu kubwa inayochangia madereva walio wengi kushindwa kumudu vyombo vya moto na hivyo kusababisha ajali na kusababisha vifo na majeruhi.
Tatu, Msongo wa mawazo na mfadhaiko kwa baadhi ya madereva upelekea kusababisha ajali, Mara kadhaa nimeshuhudia madereva wengi wakiongea peke yao huku wakisikitika na kunungunika juu ya aidha ugumu wa maisha au uwepo wa migogoro ya kifamilia kati ya dereva na mke, au mchepuko wake.
Nne, Rushwa, Miundombinu mibovu ya barabara, ubovu wa magari, upatikanaji wa leseni kinyume na utaratibu na sheria za nchi, kutojali utu, ukosefu wa hofu ya Mungu na imani za kishirikina ni sehemu ya sababu zinazochangia madereva wengi wa Tanzania na bara la Afrika kusababisha ajali zinazogharimu uhai wa binadamu, Wakati ni sasa, Taifa na Watanzania kushikamana na kukemea madereva wanaokiuka miiko ya udereva.
Watanzania tupaze sauti, Tupaze sauti, Tupaze sauti, wakati ni sasa, tusipofanya hivyo tutakwisha na kuachwa na ulemavu wa kudumu kwa sababu ya uzembe wa mtu mmoja, ambaye anaitwa dereva.
Aidha ni wajibu wa serikali kuwachukulia hatua stahiki na kali sana madereva wote wahuni wanaoenda kinyume na sheria na utaratibu wa usalama barabarani, ni wakati sasa wa kutungwa sheria kali inayozuia matumizi ya simu wakati wa utumiaji wa chombo cha moto, sheria hii ije sasa na ndio wakati wake.